Wana JF,
Asubuhi hii wakati nakuja ofisini, nimesikia wimbo mpya kwenye radio clouds, unaoitwa Bungeni Kariakoo, ukimnukuu Spika Makinda akimwagiza Mh. Wenge kufuta kauli yake akiwa anakataa, wabunge wa CCM kumwambia atoke na Mh. Zitto kumtetea kuwa asitoke ndipo zogo likaanza. Na hivi karibuni kauli ya Mh. Kafulila kusema kuwa serikali ni legelege na kuamriwa afute kauli naye kukataa na zogo likaanza tena. Kwa kweli mwimbo unafundisha sana na pengine wabunge wakiusikia watajirekebisha na kuachana na ushabiki usio na tija.
Atakayeusikia aniambie unapatikana wapi. Shukrani!
Asubuhi hii wakati nakuja ofisini, nimesikia wimbo mpya kwenye radio clouds, unaoitwa Bungeni Kariakoo, ukimnukuu Spika Makinda akimwagiza Mh. Wenge kufuta kauli yake akiwa anakataa, wabunge wa CCM kumwambia atoke na Mh. Zitto kumtetea kuwa asitoke ndipo zogo likaanza. Na hivi karibuni kauli ya Mh. Kafulila kusema kuwa serikali ni legelege na kuamriwa afute kauli naye kukataa na zogo likaanza tena. Kwa kweli mwimbo unafundisha sana na pengine wabunge wakiusikia watajirekebisha na kuachana na ushabiki usio na tija.
Atakayeusikia aniambie unapatikana wapi. Shukrani!