Natafuta wa kumrithisha mikoba, kilinge

Natafuta wa kumrithisha mikoba, kilinge

Kama kweli unataka kumtumikia Mungu , choma mikoba yote uhakikishe imekuwa majivu . Kumuachia mtu Ni sawa na kuendeleza ushetani .
 
Dah... Sa itakuwaje
Kwahiyo sahivi unapambana na pensheni tu!!
sitaki shida na wanadamu tena.. Nahitaji upweke na amani na maombi kwa sana huku nikifundisha mambo ya kiroho kwenye center yangu
 
Kama kweli unataka kumtumikia Mungu , choma mikoba yote uhakikishe imekuwa majivu . Kumuachia mtu Ni sawa na kuendeleza ushetani .
Moto utaunguza vibuyu na mapembe tuu.. Dhana itabaki salama salimini
 
Ndugu wana JF huu si utani..! Niko serious..
Najiona kabisa nazeeka sasa na nguvu zinanipungua, hivyo nimekuwa na limited movements japo mahitaji bado yako juu
Nimeamua kutangaza kufafuta mrithi wa kazi zangu.
  • Mkoba mkuu mmoja
  • Mkoba wa kati
  • Mkoba mdogo
Hii mikoba yote iko Mkoa wa Pwani kilingeni Msata
Kilinge kila kila kitu cha uganga, ugaguzi, ulozi, ushirikina na kuwanga.. Kina vifaa vyote muhimu vya kale na vya kisasa kwa shughuli zote hizo..!

Ukubwa wa eneo ni miguu 50 kwa 40. Najiandaa kurudi kumtumikia mola wangu..infact nitakuwa na kituo changu cha huduma za kiroho zisizochangamana tena na shirki.

Niliwahi kuwagusia kuhusu hiki kituo kitakachojulikana kama MULT FAITH RESEARCH SOCIETY. Naona muda wa kuwa umekaribia kabisa!
Nitakuja kutoa aina ya mrithi nimtakaye!

Asanteni.
Nitume mimi hapa
 
Safi kabisa. Kwako wewe Uchawi ni nini hasa na historia yake ilianzia wapi ?

Tuanzie hapo...
Uchawi uliaza tangu kuumbwa ulimwengu kiimani... Na asili yake ni Mola mwenyewe
 
Vitie moto, huwezi mpa mtu uchawi wako akateswe na mizimu yako.

Najua imefikia zamu yako ya kutoa damu yenye kukupa uchungu. Toa.

Ndo utajua uchawi siyo deal.
 
Back
Top Bottom