Natafuta wa kumrithisha mikoba, kilinge

Natafuta wa kumrithisha mikoba, kilinge

Si kweli ndiyo maana nilianza kwa kumuiluliza maswali ya asili ya uchawi na historia yake. Kama umefatilia mjadala utaona. Hakuna sehemu ambayo imedhibiti haya mambo kuliko dini,ila hawa unakuta wanajishughulisha na haya mambo lakini hata asili na chimbuko la haya mambo hawajui.

Dini kuiepuka ni muhali na dini ni muongozo wa kuyajua ya kweli. Ndiyo maana nikamwambia apite mapito yake na mimi nipite mapito yangu,sababu ukweli uko wazi,mkweli atajulikana.

Sasa hii kazi nakuachia wewe uifanye emhu toka nje ya dini kisha uongelee huu uchawi kama utapatia.

Tunaishi katika maisha yetu yote ya kila siku kuitafuta kweli na haki. Sasa kama dini inayo huo ukweli,huo ukweli tuuache kisa imesema Dini ? Huu utakuwa ni uhayawani sasa.

Jambo lingine ni kuwa,ukisimama kwenye kuna vitu huwezi kupigwa, hasa haya mambo ya uchawi na ndoto. Nimesoma vitabu kadhaa,nikaja kuona kwamba watu wanapigwa kutokana na ujinga hasa.

Shukrani....

Sawa Dini hizo hizo tunazoamini zina elezea uchawi kwa mitazamo tofauti sasa tutaamini ipi?

No offense kwa mfano mkristo anaamini majini wote wabaya na wanatumika kufanya mabaya,Muislamu anaamini majini kuna wabaya na kuna wazuri na hindu watakuwa na imani yao tofauti na hizi.
Sasa ukianza kujadili uchawi kwa kutegemea dini,moja kwa moja utafikia point mtatoka nje ya mada na kuanza kujadili dini ipi inaelezea uchawi vzr.

Nadhani mada ya uchawi inaweza kutumia vipande kadhaa vya vitabu vya dini km reference tu na sio kama guide ya kuutambua uchawi.

Uchawi km uchawi ni taaluma inayojitegemea ndo mana kabla hata dini hazijaja uchawi ulikuwepo ingawa vitabu vyetu vya dini ambavyo vimekuja hivi karibuni vinajaribu kuwatuliza waumini kwa kuwaambia chimbiko la uchawi ili walau waumini wapunguze curiosity.
 
Kwa hiyo huwezi kuachana navyo kama unataka kuacha haya mambo ndiyo sababu unatafuta mrithi? Bila mrithi huna hujanja.
Wale wachomaji ni wapigaji tuu... Vilinge ni maroho hayachomeki kwa hii mioto ya kibinadamu
 
Sawa Dini hizo hizo tunazoamini zina elezea uchawi kwa mitazamo tofauti sasa tutaamini ipi?
Sababu kila jambo liko wazi,rudi katika asili na marejeo.
No offense kwa mfano mkristo anaamini majini wote wabaya na wanatumika kufanya mabaya,Muislamu anaamini majini kuna wabaya na kuna wazuri na hindu watakuwa na imani yao tofauti na hizi.
Sasa ukianza kujadili uchawi kwa kutegemea dini,moja kwa moja utafikia point mtatoka nje ya mada na kuanza kujadili dini ipi inaelezea uchawi vzr.
Unapo sema wakristo wanaamini hivyo,nitakuuliza hayo ndiyo mafundisho ya Yesu,kama si ya Yesu,kwanini yafanyiwe kazi mafundisho ambayo si ya Yesu na mnasema Yesu ndiyo ameleta Ukristo.

Ndiyo maana mjadala uko huru toa hoja yako kwa vyanzo vyako na mimi natoa vyangu kisha watu wanaamua.
Nadhani mada ya uchawi inaweza kutumia vipande kadhaa vya vitabu vya dini km reference tu na sio kama guide ya kuutambua uchawi.
Unapotumia kama marejeo ujue ndiyo inakuelezea jambo husika. Uchawi unajulikana tangu zamani na athari zake zinajulikana.
Uchawi km uchawi ni taaluma inayojitegemea ndo mana kabla hata dini hazijaja uchawi ulikuwepo ingawa vitabu vyetu vya dini ambavyo vimekuja hivi karibuni vinajaribu kuwatuliza waumini kwa kuwaambia chimbiko la uchawi ili walau waumini wapunguze curiosity.
Uchawi ni nini na ulianza lini ? !
 
Ndugu wana JF huu si utani..! Niko serious..
Najiona kabisa nazeeka sasa na nguvu zinanipungua, hivyo nimekuwa na limited movements japo mahitaji bado yako juu
Nimeamua kutangaza kufafuta mrithi wa kazi zangu.
  • Mkoba mkuu mmoja
  • Mkoba wa kati
  • Mkoba mdogo
Hii mikoba yote iko Mkoa wa Pwani kilingeni Msata
Kilinge kila kila kitu cha uganga, ugaguzi, ulozi, ushirikina na kuwanga.. Kina vifaa vyote muhimu vya kale na vya kisasa kwa shughuli zote hizo..!

Ukubwa wa eneo ni miguu 50 kwa 40. Najiandaa kurudi kumtumikia mola wangu..infact nitakuwa na kituo changu cha huduma za kiroho zisizochangamana tena na shirki.

Niliwahi kuwagusia kuhusu hiki kituo kitakachojulikana kama MULT FAITH RESEARCH SOCIETY. Naona muda wa kuwa umekaribia kabisa!
Nitakuja kutoa aina ya mrithi nimtakaye!

Asanteni.
Mkuu usife tu.
 
Kwa hiyo huwezi kuachana navyo kama unataka kuacha haya mambo ndiyo sababu unatafuta mrithi? Bila mrithi huna hujanja.
Hapana uwezekano wa kuachana navyo upo kabisa , nilichokuwa najaribu kuonesha ni kuwa moto utateketexa vinavyoonekana tuu
Hii haina tofauti na kumchoma mtu moto, huyu atakufa mwili tu sio roho.. Vilinge vina maroho , hayo ndio engine .. Na kanuni ya roho inasemaje!? A soul once created CAN NEVER be destroyed.. ( rather can be restored.... Into another form/ body)

Sasa safe exit ya haya mambo ni ninini? Utaratibu uliotumia kuingilia ndio huohuo utaotumia kutokea,ni kama tu kuwasha na kuzima ile mitambo mikubwa sana... Kuna mchakato wa kuwasha na kuna mchakato wa kuzima.. Usipofuata huo mchakato utaleta damage kubwa
 
Hili nalijua lakini,tunaishi maisha yetu yote kuutafuta ukweli,na hili nilikuuliza huko nyuma lakini hukulijibu,je kama dini ndiy zina ukweli huo ukweli tuuache ?

Lakini dini haipingani na uhalisia wala akili iliyo salama.

Sasa je nikiacha dini unaweza kutupa au kunipa ukweli wa hili jambo nje ya dini ? Kama uwezo huo unao,itifaki izingatiwe fanya hivyo.
Nimerejea
Bado tunapishana hapo kwenye dini na ukweli... Labda utumie neno 'dini yangu' hapo naweza kukuelewa, lakini shida itakuja moja pale utakapodhani ya kuwa dini yako ndio imani ya 'kweli' na ndio sahihi
Imani ni jambo la kiroho zaidi na ni jambo la kuaminishwa zaidi kuliko kuhoji na kupata ithibati.. Lakini dunia haina imani moja wala dini moja na karibia kila mmoja anadhani kuwa dini na imani yake ndio sahihi kuliko za wengine
Ni wachache wenye mtazamo mpana zaidi kuliko huo, na hawa wachache ndio wana harmonize dunia na kuleta amani la sivyo pangekuwa hapatoshi
Tumeshuhudia mauaji ya kutisha kwa ajili ya dini na imani
Tumeshuhudia ukatili wa kutisha kwa ajili tu eti kulinda dini, kulinda imani
Tumeshuhudia mifarakano na migongano kila kona ya dunia kuhusu dini na imani pia

Uchawi pamoja na ubaya wake wote unaosingiziwa haujaua mamilioni kama dini
Haujafitinisha mamilioni kama dini
Haujafanya ukatili wa kutisha sana kuliko dini
Kuna uchafu na ubaya wa kutisha ndani ya dini kuliko kwenye ushirikina ndio maana unapoongelea 'ukweli' wa dini napata ukakasi fulani

Sijui tuko pamoja?
 
Msingi hapa ni kupima kwa akili zetu na uhalisia. Nitakuuliza je haya niliyo yaandika yako sahihi au si sahihi yanatokea au kinyume chake,unajua dini kuiepuka ni jambo muhali sana,hasa katika kutafuta ukweli na maslahi.

Unachotakiwa wewe pita katika mapito yako unayo yaamini na mimi nipite yangu kisha tuna nakishi hoja zetu mkweli atabainika tu. Ukweli una sifa nzuri sana,wenyewe siku zote huwa uko juu wala hakuna cha juu yake na ukweli kadhalika una mea kokote.

Kwahiyo wewe kuwa huru na jifarague unavyotaka na ukosoe ninachokiandika kwa hoja na ubainifu kisha mimi nitafanya vivyo hivyo. Huu ndiyo uhuru katika mjadala. Mathalani juzi kati humu ndani kuna mtu alikuwa ana dai ya kuwq Ibrahiim alikuwa Myahudi,nikamuomba ushahidi toka katika vitabu anavyo viamini lakini hakuwa na ushahidi huo,maana yake yeye ni uongo sababu nimempa uhuru katika jambo la kihistoria na tena la kiimani. Mimi nikamwamba Ibrahiim alikuwa Muislamu na ushahidi nikampa. Kwahiyo hivi ndivyo mambo yanavyo enda.

Mathalani katika uliyo kuwa unayaandika yapo tunayo afikiana na hayo nakubali,sasa katika yale tunayotofautiana wewe pita mapito yako na mimi nipite mapito yangu naamini tutakutana katika ile njia ya apanda (njia panda).

Tuendelee...
Mathalani katika uliyo kuwa unayaandika yapo tunayo afikiana na hayo nakubali,sasa katika yale tunayotofautiana wewe pita mapito yako na mimi nipite mapito yangu naamini tutakutana katika ile njia ya apanda (njia panda).

Hapo nimekupata vema tunaweza kukubaliana kutokubaliana katika baadhi ya hoja lakini kwa hoja pia
 
Hapana uwezekano wa kuachana navyo upo kabisa , nilichokuwa najaribu kuonesha ni kuwa moto utateketexa vinavyoonekana tuu
Hii haina tofauti na kumchoma mtu moto, huyu atakufa mwili tu sio roho.. Vilinge vina maroho , hayo ndio engine .. Na kanuni ya roho inasemaje!? A soul once created CAN NEVER be destroyed.. ( rather can be restored.... Into another form/ body)

Sasa safe exit ya haya mambo ni ninini? Utaratibu uliotumia kuingilia ndio huohuo utaotumia kutokea,ni kama tu kuwasha na kuzima ile mitambo mikubwa sana... Kuna mchakato wa kuwasha na kuna mchakato wa kuzima.. Usipofuata huo mchakato utaleta damage kubwa
Hii ni ngende hii mkuu ni mbaya sana ukiacha bila protocol soon tutakuzika...ni lele hii ukionja ila ni very risk unaweza kukuta mali zako zinaungua moto from no where.

.au ukafa kama Ginimbi...
 
Nimerejea
Bado tunapishana hapo kwenye dini na ukweli... Labda utumie neno 'dini yangu' hapo naweza kukuelewa, lakini shida itakuja moja pale utakapodhani ya kuwa dini yako ndio imani ya 'kweli' na ndio sahihi
Katika usanifu wa lugha na kumjua mtu,kuna kauli mtu akiitumia hufidisha maana nyingine na huweza baadhi ya muda ukaondosha tamko kabisa,na ukajua hapa anakusudia nini au linakusudiwa nini,mfano "naenda kuoga maji" hii kauli si fasaha sababu ulitakiwa uondoshe tamko "maji" sababu kawaida mtu akienda kuoga ujue kabisa anaenda kuoga maji. Mimi ninapo ongelea dini ujue ni dini yangu mimi.

Hiyi unayo isema shida si shida endapo ukiwa mkweli na una hoja na ubainifu,sijui huwa mnaogopa wapi ? Au labda hamjui nguvu ya ukweli ilivyo. Mimi kwa jinsi nilivyo naweza kujadiliana na yeyote maadamu nina hoja na ubainifu.

Tukirudi kwako kama ulivyo bainisha huko nyuma ya kuwa uliweka vigezo vyako vya kuona jambo fulani ni sawa,sasa tukienda mbali tunatakiwa tuhakiki tunayo yaamini au kuyaegemea maadamu mizani ipo. Sasa mnapoleta kisingizio hiki mnaonekana hamuwezi kukosoa kile ambacho mtu yuko dhidi yako,na hili linaonyesha udhaifu wa unacho ona unakijua.
Imani ni jambo la kiroho zaidi na ni jambo la kuaminishwa zaidi kuliko kuhoji na kupata ithibati.. Lakini dunia haina imani moja wala dini moja na karibia kila mmoja anadhani kuwa dini na imani yake ndio sahihi kuliko za wengine
Hii siyo kweli,huwezi kuitenganisha imani na matendo imani na uhalisia. Huu mtazamo si wa kweli na unaonyesha ya kuwa kuna mambo huyajui mengi kuhusu imani. Mathalani mimi katika imani yetu,tumetunukiwa elimu ya uhakiki wa habari hasa za mtume na nyingine kwa ujumla,elimu hii kiistilahi inaitwa "Mustwalahul Hadithi", ukitaka kujua kuna miujiza katika elimu basi ni elimu hii. Elimu hii kuhoji na utafiti ndiyo msingi mama wa elimu hii. Lakini kadhalika Mola wetu anatutaka tuhoji mno na kifikiria mno. Sasa unaposema imani ni jambo la kuaminishwa hakuna kuhoji hakuna ithibati wewe unakuwa Muongo,labda uainishe mathalani Imani fulani wao hufata mambo kichwa mchunga,lakini si imani zote hasa imani yangu.

Sahihi kabisa kuna imani nyingi na dini nyingi kadhalika,lakini akili ya kawaida tu inakataa ya kuwa imani zote hizo na dini zote hizo kwamba ziko sahihi zote. Haya ni matumizi mabaya ya akili na ni kujidanganya kuliko pea zaidi.

Mathalani mimi nina uwezo wa kutoka mbele na kujifaragua juu ya imani yangu ndiyo ya kweli zaidi kuliko nyingine na huu ndiyo ukweli na ushahidi upo na uko wazi. Sasa hamtakiwi kuogopa kuonyesha ukweli wa imani zenu,la sivyo mtakuwa mnaishi maisha yenu yote katika uongo na upotofu na huu ni uzembe.
Ni wachache wenye mtazamo mpana zaidi kuliko huo, na hawa wachache ndio wana harmonize dunia na kuleta amani la sivyo pangekuwa hapatoshi
Huu ni uongo ambao mpaka unakufa huwezi kuthibitisha ukweli wa kauli hii. Huwezi kuwa na mtazamo pana zaidi nje ya imani sahihi,huko ni kujidanganya. Hili halipo.Unao wasema wewe ni wajinga ambao wanaona maisha ni hapa na hakuna cha ziada na ndio hao hao hawajui kwanini wanaishi.

Hakuna watu wanao jua umuhimu wa amani kama watu wa dini hasa dini yangu,sababu wanaiangalia amani katika uhalisia wake.

Mimi nakupa kazi ndogo ili nikuonyeshe udhaifu wa hiki ukichokiandika,nitajie watu wawili tu wenye mtazamo huo mpana (unao dai) kisha tuwajadili japo kwa uchache wenye kukidhi haja.

Watu wa dini ndiyo wanasimamia amani ipasavyo sababu wanajua vijenzi na misingi yake.
Tumeshuhudia mauaji ya kutisha kwa ajili ya dini na imani
Tumeshuhudia ukatili wa kutisha kwa ajili tu eti kulinda dini, kulinda imani
Tumeshuhudia mifarakano na migongano kila kona ya dunia kuhusu dini na imani pia
Suala hilo linazungumziwa katika hali mbili,moja sahihi na nyingine si sahihi kwa msingi wa ufitini na ujinga. Tumeshuhudia fitina nyingi za nchi za magharibi katika umwagaji wa damu kwa ajili ya maslahi ya kidunia na haya ndiyo mauaji mengi na yana shamiri sana,lakini kwa wahusika kuficha ukweli na kuitangaza batili. Lakini wasahau ya kuwa "Japokuwa wao wanapanga na Mola naye ana panga na Allah ndiye mjuzi wa kupanga mambo". Hakika hali wa shani laiti ulimwengu ungefata dini hasa ya Uislamu,ulimwengu ungekuwa sehemu salama sana.

Ama nukta ya pili,katika usahihi kwenye dini kuna ibada inayo itwa Jihadi hii ni ibada na nguzo na msharti yake,na haipiganwi tu kiholela holela bali mpaka mashart na nguzo zidirikiwe. Sasa unachokiona katika mapigano yanayo husisha imani fulani mengi huwa hayaja kidhi vigez vya imani husika.

Sasa tujadili katika uhalisia nitajie mapigano au umwagaji damu ambao hauna mkono wa wafitini nawazungumzia nch za magharibi kisha mimi nakutajia vita ambavyo havina mkono wa wamagharibi,hizi akili tulipewa bure tuzitumie na tuseme haki popote tulipo.

Kaka hakuna kitu kizuri kama elimu,ili uamini ya kuwa elimu ni kitu kizuri,mpaka mjinga huwa unapenda aitwe msomi na mjuzi wa mambo wakati hana anacho miliki katika elimu husika.
Uchawi pamoja na ubaya wake wote unaosingiziwa haujaua mamilioni kama dini
Haujafitinisha mamilioni kama dini
Haujafanya ukatili wa kutisha sana kuliko dini
Kuna uchafu na ubaya wa kutisha ndani ya dini kuliko kwenye ushirikina ndio maana unapoongelea 'ukweli' wa dini napata ukakasi fulani
Ni kosa kubwa sana hasa kiakili kulinganisha mambo mawili ambayo kwa dhati yake kabisa hayafanani.

Ubaya wa uchawi si tu kufarakanisha watu,au kuua watu bali ni kutafuta msaada nje ya yule anayestahiki kuombwa msaada yaani Allah mtukufu,kwahiyo idadi hapa haina nguvu mzee bali athari. Mambo hayapimwi kwa wingi isipokuwa machache sana na ukifatilia sana uchache umesifiwa mno.

Kaka vipimo vyako dhaifu mno na havikupeleki katika kupatia ndiyo maana nakutaka ujenge hoja kwa mapito yako na mimi nijenge hoja kwa mapito yako. Mathalani kosa kubwa ambalo uko nalo ni kuwa msingi wa upimaji wa usahihi kwa mtazamo wako wewe ni wewe mwenyewe,sasa nitakuuliza wewe ni mwanadamu dhaifu mno,kuanzaia mwili,milango ya fahamu mpaka akili. Ndiyo maana si ajabu ukaona Ushirikina ni sawa huku historia ya ushirikina hijui. Hili tatizo kubwa mno.

Nakuja kuendelea hapa nilipo ishia...m
 
unapoongelea 'ukweli' wa dini napata ukakasi fulani
Hili huwezi kulithibitisha. Ndiyo maana nachotaka ukosoe jambo la dini kwa hoja na ubainifu kisha uweke usahihi,unaposema ukakasi bila ushahidi hapa unaonekana muongo na unafanya nipate maswali mengi ya kukuuliza.
 
Hili huwezi kulithibitisha. Ndiyo maana nachotaka ukosoe jambo la dini kwa hoja na ubainifu kisha uweke usahihi,unaposema ukakasi bila ushahidi hapa unaonekana muongo na unafanya nipate maswali mengi ya kukuuliza.
UKWELI kwenye DINI una ukakasi mkubwa kwakuwa kila dini inadai kuwa ndio DINI ya kweli na waamini wake huwezi kuwaambia kitu kwenye hilo... Lakini je huo ndio UHALISIA?
Nina mada kuhusu dini nadhani huko utaniuliza vizuri maana hapa ni kama tumepoteza kabisa muktadha wa mada hii..
Ikishakuwa tayari nitakualika.. Nitafurahi kukuona huko
 
Nimerejea
Bado tunapishana hapo kwenye dini na ukweli... Labda utumie neno 'dini yangu' hapo naweza kukuelewa, lakini shida itakuja moja pale utakapodhani ya kuwa dini yako ndio imani ya 'kweli' na ndio sahihi
Imani ni jambo la kiroho zaidi na ni jambo la kuaminishwa zaidi kuliko kuhoji na kupata ithibati.. Lakini dunia haina imani moja wala dini moja na karibia kila mmoja anadhani kuwa dini na imani yake ndio sahihi kuliko za wengine
Ni wachache wenye mtazamo mpana zaidi kuliko huo, na hawa wachache ndio wana harmonize dunia na kuleta amani la sivyo pangekuwa hapatoshi
Tumeshuhudia mauaji ya kutisha kwa ajili ya dini na imani
Tumeshuhudia ukatili wa kutisha kwa ajili tu eti kulinda dini, kulinda imani
Tumeshuhudia mifarakano na migongano kila kona ya dunia kuhusu dini na imani pia

Uchawi pamoja na ubaya wake wote unaosingiziwa haujaua mamilioni kama dini
Haujafitinisha mamilioni kama dini
Haujafanya ukatili wa kutisha sana kuliko dini
Kuna uchafu na ubaya wa kutisha ndani ya dini kuliko kwenye ushirikina ndio maana unapoongelea 'ukweli' wa dini napata ukakasi fulani

Sijui tuko pamoja?

Mkuu Kwa mujibu wa Biblia Imani ya kweli inapaswa kuwa moja.
Waefeso4:4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.
Sasa imani kama zipo nyingi, zitakuwepo fake au za uongo
Hata hizi siku za kuabudu zilivyobananishwa hapa lazima zipo fake na ya kweli. Maana utakuta kuna ijumaa, jumamosi na jumapili. hazipo kibahati mbaya. zimewekwa hapo kutuchanganya.
Tusidanganyane kwamba imani zote ni sawa
 
UKWELI kwenye DINI una ukakasi mkubwa kwakuwa kila dini inadai kuwa ndio DINI ya kweli na waamini wake huwezi kuwaambia kitu kwenye hilo...
Hayo hubaki kuwa madai tu mpaka pale watakapo thibitisha ukweli juu ya madai hayo.

Ndiyo maana nikasema hivi akili inakataa kwamba din zote au imani zote zikawa zimepatia,hili halipo. Yuko mmoja tu ni sahihi. Kwahiyo wingi si hoja mzee.
Nina mada kuhusu dini nadhani huko utaniuliza vizuri maana hapa ni kama tumepoteza kabisa muktadha wa mada hii..
Ikishakuwa tayari nitakualika.. Nitafurahi kukuona huko
Kwangu mimi mada hii ilishaisha,pale tu nilipo jua uhalisia wako juu ya asili ya uchawi na maana ya uchawi.

Hiki kimekuja tu kama ziada.

Ukinialika huko nitakuja ila mtindo huu wa mjadala usiwe katika mada hii,inaonekana una udhaifu wa kuthibitisha mambo na kuthibitisha kile unacho kiamini.

Ila kingine uhakikishe ya kuwa una maarifa mapana juu ya dini,ila kama utaanzisha mada kwa kuuliza swali hilo halina shida hata ukiwa una maarifa madogo au huna kabisa haina shida.


Tuko pamoja,utanistua huo uzi ukiwa tayari.

Tuko pamoja.
 
Ndugu wana JF huu si utani..! Niko serious..
Najiona kabisa nazeeka sasa na nguvu zinanipungua, hivyo nimekuwa na limited movements japo mahitaji bado yako juu
Nimeamua kutangaza kufafuta mrithi wa kazi zangu.
  • Mkoba mkuu mmoja
  • Mkoba wa kati
  • Mkoba mdogo
Hii mikoba yote iko Mkoa wa Pwani kilingeni Msata
Kilinge kila kila kitu cha uganga, ugaguzi, ulozi, ushirikina na kuwanga.. Kina vifaa vyote muhimu vya kale na vya kisasa kwa shughuli zote hizo..!

Ukubwa wa eneo ni miguu 50 kwa 40. Najiandaa kurudi kumtumikia mola wangu..infact nitakuwa na kituo changu cha huduma za kiroho zisizochangamana tena na shirki.

Niliwahi kuwagusia kuhusu hiki kituo kitakachojulikana kama MULT FAITH RESEARCH SOCIETY. Naona muda wa kuwa umekaribia kabisa!
Nitakuja kutoa aina ya mrithi nimtakaye!

Asanteni.
Mm nipokee kaenye hiho kituo maana ni muumini wako
 
Back
Top Bottom