Uharamu unatokana na Imani na uhalisia,jambo lenye kudhuru afya ya akili yako na kukufanya ukawa mjinga na muovu hilo huwa haramu.
Nikikuuliza wewe marejeo yako ya kujia kipi kinafaa na kipi hakifai ni wapi ? Yaani umetumia vigezo gani au umerejea wapi mpaka ukaona kujifunza uchawi ni jambo lenye kufaa ?
Uharamu unatokana na Imani na uhalisia,jambo lenye kudhuru afya ya akili yako na kukufanya ukawa mjinga na muovu hilo huwa haramu.



Hapo juu kuna shida kidogo, haramu ni hisia ya kiimani zaidi kuliko uhalisia. Na haramu inatofautiana toka imani moja hadi nyingine, haramu kwako ni halali kwa mwingine na kinyume chake
...Na si kila haramu inadhuru afya ya akili na kukufanya mjinga! Naomba nikusahihishe pia kwenye neno mjinga...labda ungetumia mpumbavu, kwakuwa mjinga ni asiyejua akijua ujinga humtoka, lakini mpumbavu ni yule aliyepewa maarifa lakini asiyatumie
Haramu ziko nyingi kiimani, kisheria na kijamii pia
Nyama haramu
Pesa haramu
Dini haramu
Mapenzi haramu
Dawa haramu nknk
Haramu maana yake si halali... Kinachoharamisha ama kuhalalisha kitu ni hayo mambo niliyotaja hapo juu IMANI, SHERIA NA JAMII,ukitaka kwenda ndani zaidi unakuta kuna mila, desturi na tamaduni pia ... Lakini hivi tunaweza kuviingiza kwenye jamii
Haramu haimfanyi mtu kuwa muovu...uovu ni tabia ni hulka... Mtu mwema anaweza kufanya haramu (kwa tafsiri ya jamii yake kiimani na kisheria) lakini asiwe mwovu.. Uovu una vinasaba vyote vya rohombaya
Sasa nikikujibu marejeo yangu ya juu ya kipi kinafaa na kipi hakifai ni hivi
Jambo lolote ambalo halina madhara kwangu wala kwa wengine hilo kwangu ni halali kujifunza na kulitumia
Jambo lolote ambalo lina madhara yoyote kwangu na kwa wengine nitajifunza kwa tahadhari ili nielimike nalo lakini sitaeza kulitumia popote
Faida moja kubwa nitakayojivunia daima kwa kujifunza kwangu USHIRIKINA (uchawi, ulozi, uganga wa kienyeji na kuwanga) ni mimi kuwa mkufunzi mahiri wa kuwapa watu elimu n maarifa ya bure kuhusu hayo mambo na kuwachomoa wengine wasipigwe ama kuingizwa kwenye viapo na maagano mabaya
Leo hii wana JF na wasomaji wengine wengi wako fully equipped na mambo ya kishirikina na wanatembea kifua mbele hawababaishwi kwa sababu yangu

Ninapoachana na mikoba naachana nayo kwa mafanikio makubwa ya kujivunia na ninapotafuta mrithi ninajua kwa hakika kwanini nafanya hivyo


