Natafuta wa kumrithisha mikoba, kilinge

Natafuta wa kumrithisha mikoba, kilinge

Hapana haikinzani bali sasa hizo ni aina za uchawi... Kumbuka hata kama ni nguvu hasi kiroho lakini bado haimzuii mtu kujifunza na kuelimika
Sasa haikonzani vipi wakati maana uliyoitoa inaonyesha hivyo.

Huko juu kama ulikuwa makini nilisisitiza juu ya maana na nikakupa maana ya maana na vijenzi vyake,lengo tusije kushughulika tena na maana ya Uchawi baada ya wewe kutoa maana ya tamko hilo. Lakini naona hali inakuwa kinyume. Sababu maana yako naona inaruhusu yaingie yasiyotakiwa kuingia na kuzuia yanayo takiwa kuingia.

Maana ulipose ni hasi...Maana yake vyote vinaangukia humo,ukivitoa baadhi ujue maana yako ina mushkeli.

Kwanini mtu ujifunze jambo ambalo hubadilisha uhalisia na kulifanya jambo baya kuonekana zuri na kufarakanisha watu ? Vipi uelimike kwalo ? Labda ujifunze ili uweze kuliepuka na si kulitendea kazi,ndiyo maana wale Malaika Harut na Marut,walikuwa wana watahahdarisha watu pale wanapo wafundisha Uchawi huo kwamba tunawafundisha lakini hii ni FITNA.

Sasa vipi ujifunze Uchawi kisha uelimike ?
 
Ndugu wana JF huu si utani..! Niko serious..
Najiona kabisa nazeeka sasa na nguvu zinanipungua, hivyo nimekuwa na limited movements japo mahitaji bado yako juu
Nimeamua kutangaza kufafuta mrithi wa kazi zangu.
  • Mkoba mkuu mmoja
  • Mkoba wa kati
  • Mkoba mdogo
Hii mikoba yote iko Mkoa wa Pwani kilingeni Msata
Kilinge kila kila kitu cha uganga, ugaguzi, ulozi, ushirikina na kuwanga.. Kina vifaa vyote muhimu vya kale na vya kisasa kwa shughuli zote hizo..!

Ukubwa wa eneo ni miguu 50 kwa 40. Najiandaa kurudi kumtumikia mola wangu..infact nitakuwa na kituo changu cha huduma za kiroho zisizochangamana tena na shirki.

Niliwahi kuwagusia kuhusu hiki kituo kitakachojulikana kama MULT FAITH RESEARCH SOCIETY. Naona muda wa kuwa umekaribia kabisa!
Nitakuja kutoa aina ya mrithi nimtakaye!

Asanteni.
Mkuu ila pombe usiache mkuu.
 
Sasa haikonzani vipi wakati maana uliyoitoa inaonyesha hivyo.

Huko juu kama ulikuwa makini nilisisitiza juu ya maana na nikakupa maana ya maana na vijenzi vyake,lengo tusije kushughulika tena na maana ya Uchawi baada ya wewe kutoa maana ya tamko hilo. Lakini naona hali inakuwa kinyume. Sababu maana yako naona inaruhusu yaingie yasiyotakiwa kuingia na kuzuia yanayo takiwa kuingia.

Maana ulipose ni hasi...Maana yake vyote vinaangukia humo,ukivitoa baadhi ujue maana yako ina mushkeli.

Kwanini mtu ujifunze jambo ambalo hubadilisha uhalisia na kulifanya jambo baya kuonekana zuri na kufarakanisha watu ? Vipi uelimike kwalo ? Labda ujifunze ili uweze kuliepuka na si kulitendea kazi,ndiyo maana wale Malaika Harut na Marut,walikuwa wana watahahdarisha watu pale wanapo wafundisha Uchawi huo kwamba tunawafundisha lakini hii ni FITNA.

Sasa vipi ujifunze Uchawi kisha uelimike ?
Nitakurejea
 
Ndugu wana JF huu si utani..! Niko serious..
Najiona kabisa nazeeka sasa na nguvu zinanipungua, hivyo nimekuwa na limited movements japo mahitaji bado yako juu
Nimeamua kutangaza kufafuta mrithi wa kazi zangu.
  • Mkoba mkuu mmoja
  • Mkoba wa kati
  • Mkoba mdogo
Hii mikoba yote iko Mkoa wa Pwani kilingeni Msata
Kilinge kila kila kitu cha uganga, ugaguzi, ulozi, ushirikina na kuwanga.. Kina vifaa vyote muhimu vya kale na vya kisasa kwa shughuli zote hizo..!

Ukubwa wa eneo ni miguu 50 kwa 40. Najiandaa kurudi kumtumikia mola wangu..infact nitakuwa na kituo changu cha huduma za kiroho zisizochangamana tena na shirki.

Niliwahi kuwagusia kuhusu hiki kituo kitakachojulikana kama MULT FAITH RESEARCH SOCIETY. Naona muda wa kuwa umekaribia kabisa!
Nitakuja kutoa aina ya mrithi nimtakaye!

Asanteni.
Vichome moto
Utasikia amani zaidi.
 
Nitakurejea
Kuna kanuni moja huwa naitumia nayo ni kujifunza kila kitu lakini wakati wa kutenda nachagua yanayofaa...
Katika maisha tambua(jua) unafanya nini lakini usifanye kila unachotambua (jua)...Elimu ya maarifa haina ukomo hivyo pokea kila fundisho kishapo chambua baya na zuri kisha fanya maamuzi
Elimu ya utambuzi wa vitu ni silaha kubwa sana kwenye kuufahamu ulimwengu,mambo yake na waja wake... Ukiwa mfinyu wa maarifa utateswa na mengi, na wengi

Kujifunza uchawi kwa maana ya kuelimika hakuna tatizo kabisa...Nimewatoa tongotongo wengi sana hapa JF ..nimefundisha sana ushirikina kiasi kwamba wengi leo hawababaishwi na kitu kinachoitwa uchawi ulozi nknk
Hivyo basi pamoja na uchawi kiasili kuwa nguvu hasi lakini kufahamu AA BEE CHEE zake ni muhimu sana
 
Vichome moto
Utasikia amani zaidi.
Naomba niseme kweli na niwe muwazi sana kwenye hili SITOWEZA! Moto unateketeza visible objects tuu.. Nguvu halisi itakugeukia na kuingia kwenye mapambano mapya na ukicheza vibaya tu umekwisha!
 
Naomba niseme kweli na niwe muwazi sana kwenye hili SITOWEZA! Moto unateketeza visible objects tuu.. Nguvu halisi itakugeukia na kuingia kwenye mapambano mapya na ukicheza vibaya tu umekwisha!
Unachoma huku umeokoka na kuita Nguvu ipitayo nguvu zote, Yesu Kristo.
Hakuna nguvu itakayo kushinda ukiwa na Yesu Kristo.
 
Unachoma huku umeokoka na kuita Nguvu ipitayo nguvu zote, Yesu Kristo.
Hakuna nguvu itakayo kushinda ukiwa na Yesu Kristo.
Kaka hizi sio tunguli wala hirizi tuu ni fully equipped kilinge..
 
Kuna kanuni moja huwa naitumia nayo ni kujifunza kila kitu lakini wakati wa kutenda nachagua yanayofaa...
Katika maisha tambua(jua) unafanya nini lakini usifanye kila unachotambua (jua)...Elimu ya maarifa haina ukomo hivyo pokea kila fundisho kishapo chambua baya na zuri kisha fanya maamuzi
Elimu ya utambuzi wa vitu ni silaha kubwa sana kwenye kuufahamu ulimwengu,mambo yake na waja wake... Ukiwa mfinyu wa maarifa utateswa na mengi, na wengi

Kujifunza uchawi kwa maana ya kuelimika hakuna tatizo kabisa...Nimewatoa tongotongo wengi sana hapa JF ..nimefundisha sana ushirikina kiasi kwamba wengi leo hawababaishwi na kitu kinachoitwa uchawi ulozi nknk
Hivyo basi pamoja na uchawi kiasili kuwa nguvu hasi lakini kufahamu AA BEE CHEE zake ni muhimu sana
Nimekupata vyema.

Mimi kuna elimu kwangu ni haramu kujifunza.

1. Uchawi
2. Falaki
3. Falsafa

Na mfano wa hizo...
 
Nimekupata vyema.

Mimi kuna elimu kwangu ni haramu kujifunza.

1. Uchawi
2. Falaki
3. Falsafa

Na mfano wa hizo...
Uharamu unatokana na
Wewe mwenyewe?
Asili?
Imani?
 
Mkuu hujajua Ukuu wa Mungu kupitia Yesu Kristo.
Mkiri na utaona nguvu hizo zinavyo legea na kupukutika.
Amini.

Flp 3:12-13 SUV
Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu. Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele
 
Uharamu unatokana na
Wewe mwenyewe?
Asili?
Imani?
Uharamu unatokana na Imani na uhalisia,jambo lenye kudhuru afya ya akili yako na kukufanya ukawa mjinga na muovu hilo huwa haramu.

Nikikuuliza wewe marejeo yako ya kujia kipi kinafaa na kipi hakifai ni wapi ? Yaani umetumia vigezo gani au umerejea wapi mpaka ukaona kujifunza uchawi ni jambo lenye kufaa ?
 
Uharamu unatokana na Imani na uhalisia,jambo lenye kudhuru afya ya akili yako na kukufanya ukawa mjinga na muovu hilo huwa haramu.

Nikikuuliza wewe marejeo yako ya kujia kipi kinafaa na kipi hakifai ni wapi ? Yaani umetumia vigezo gani au umerejea wapi mpaka ukaona kujifunza uchawi ni jambo lenye kufaa ?
Uharamu unatokana na Imani na uhalisia,jambo lenye kudhuru afya ya akili yako na kukufanya ukawa mjinga na muovu hilo huwa haramu.

Hapo juu kuna shida kidogo, haramu ni hisia ya kiimani zaidi kuliko uhalisia. Na haramu inatofautiana toka imani moja hadi nyingine, haramu kwako ni halali kwa mwingine na kinyume chake

...Na si kila haramu inadhuru afya ya akili na kukufanya mjinga! Naomba nikusahihishe pia kwenye neno mjinga...labda ungetumia mpumbavu, kwakuwa mjinga ni asiyejua akijua ujinga humtoka, lakini mpumbavu ni yule aliyepewa maarifa lakini asiyatumie
Haramu ziko nyingi kiimani, kisheria na kijamii pia
Nyama haramu
Pesa haramu
Dini haramu
Mapenzi haramu
Dawa haramu nknk
Haramu maana yake si halali... Kinachoharamisha ama kuhalalisha kitu ni hayo mambo niliyotaja hapo juu IMANI, SHERIA NA JAMII,ukitaka kwenda ndani zaidi unakuta kuna mila, desturi na tamaduni pia ... Lakini hivi tunaweza kuviingiza kwenye jamii

Haramu haimfanyi mtu kuwa muovu...uovu ni tabia ni hulka... Mtu mwema anaweza kufanya haramu (kwa tafsiri ya jamii yake kiimani na kisheria) lakini asiwe mwovu.. Uovu una vinasaba vyote vya rohombaya

Sasa nikikujibu marejeo yangu ya juu ya kipi kinafaa na kipi hakifai ni hivi
Jambo lolote ambalo halina madhara kwangu wala kwa wengine hilo kwangu ni halali kujifunza na kulitumia
Jambo lolote ambalo lina madhara yoyote kwangu na kwa wengine nitajifunza kwa tahadhari ili nielimike nalo lakini sitaeza kulitumia popote

Faida moja kubwa nitakayojivunia daima kwa kujifunza kwangu USHIRIKINA (uchawi, ulozi, uganga wa kienyeji na kuwanga) ni mimi kuwa mkufunzi mahiri wa kuwapa watu elimu n maarifa ya bure kuhusu hayo mambo na kuwachomoa wengine wasipigwe ama kuingizwa kwenye viapo na maagano mabaya

Leo hii wana JF na wasomaji wengine wengi wako fully equipped na mambo ya kishirikina na wanatembea kifua mbele hawababaishwi kwa sababu yangu Ninapoachana na mikoba naachana nayo kwa mafanikio makubwa ya kujivunia na ninapotafuta mrithi ninajua kwa hakika kwanini nafanya hivyo
 
Back
Top Bottom