Natafuta vijana wa kufyatua matofali

Natafuta vijana wa kufyatua matofali

Kama kichwa Cha habari kinavyosema hapo juu natafuta vijana watatu nitaowaajiri waje wafyatue matofali malipo ni 5000 Kwa siku kula juu Yao Kwa waliotayari waje pm mda huu Kwa mnaohitaji nimeamua kutoa ajira Kwa vijana wenzangu Ili tuweze kusonga mbele
🤣🤣Matofali ya aina gani mana kama ni ya cement na mchanga huwa wanalipwa 5000 moka 6000 kwa mfuko na kwa siku wanaweza kupiga mifuko mpka 20 wakiwa watu sita au watano kwamba kila mtu anaondoka na 20000 mpaka 25000 sasa sijui we utapata wapi mtu wa kumlipa 5000 kwa kazi ya siku..
 
Hata mim nafahamu hivyo kwamba kufyatua tofauli kwa Gharama ya mfuko mmoja, Mfano huku kwetu mfuko mmoja wa saruji ni 4000- 5000 kutokana na maelewano. Kwahyo raia wakikupigia mifuko 20 ya wanaondoka kama na 80k mpaka 100k.
Upo sawa huku ni mpka 6000 inategemea na unatoa matofali mangapi kwa mfuko..
 
Maskini hatunywi chai braza naona wewe hujapita huko ndio maana unaongea nadharia
🤣🤣we hujui kazi ya kukimbia na tofali unakunywa chai na chapati 4 ikifika saa nne unasikia njaa kama mama anaenyonuesha mkuu ndomna watu wanalipwa 6000 kwa mfuko mkuu ile kazi ni ngumu hakuna kusimama tokea 12 mpaka 12
 
niliwahi kubeba tofali mia saidia fundi ilikua kidogo nipasuke nyongo.. malipo ilikua 10,000 jioni saa moja😅😅

nilikimbia kazi saa nne asubuhi😅😅😅
 
🤣🤣we hujui kazi ya kukimbia na tofali unakunywa chai na chapati 4 ikifika saa nne unasikia njaa kama mama anaenyonuesha mkuu ndomna watu wanalipwa 6000 kwa mfuko mkuu ile kazi ni ngumu hakuna kusimama tokea 12 mpaka 12
Hahaha
 
Hiyo ni bei ya kila mfuko na si malipo boss
 
Kama kichwa Cha habari kinavyosema hapo juu natafuta vijana watatu nitaowaajiri waje wafyatue matofali malipo ni 5000 Kwa siku kula juu Yao Kwa waliotayari waje pm mda huu Kwa mnaohitaji nimeamua kutoa ajira Kwa vijana wenzangu Ili tuweze kusonga mbele
Fyatua mwenyewe tu kaka ili kutunza pesa...
 
Back
Top Bottom