Natafuta vijana wa kufyatua matofali

Natafuta vijana wa kufyatua matofali

Kama kichwa Cha habari kinavyosema hapo juu natafuta vijana watatu nitaowaajiri waje wafyatue matofali malipo ni 5000 Kwa siku kula juu Yao Kwa waliotayari waje pm mda huu Kwa mnaohitaji nimeamua kutoa ajira Kwa vijana wenzangu Ili tuweze kusonga mbele
Hahaha.
Hata kwa bakharesa ni nafuu sana mkuu
 
Kama kichwa Cha habari kinavyosema hapo juu natafuta vijana watatu nitaowaajiri waje wafyatue matofali malipo ni 5000 Kwa siku kula juu Yao Kwa waliotayari waje pm mda huu Kwa mnaohitaji nimeamua kutoa ajira Kwa vijana wenzangu Ili tuweze kusonga mbele
Duuh mnajua kuwatumia na kuwaibia watito wa wenzenu.
Tofali mfuko mmoja wa cement ni 5000
 
Sio lazima lakini
Pamoja na kwamba si lazima, 5,000/- ni ndogo sana..!!
Anyway;
1. Unatarajia afyatue matofali mangapi kwa siku?
2. Maji yanapatika site?
3. Site ipo wapi?
4. Malipo ni kila siku anapewa 5,000/- yake, au unamkusanyia na kumlipa baada ya muda gani?
 
That's too much bro, mtu akila tangu asbh mpaka jion anabaki na nn hapo? jamn hebu tuwe na utu na hawa vijana wetu. Kama unaweza wape offer ya chakula au walipe per unit, Kila tofali moja mpe mtu mia ili watu wajipimie kazi..natanguliza shukrani.
Umeongea ukweli, kazi ni utu sio utumwa. Ni vema kumuwekea mtu standards za kibinadamu ili afanye kazi kwa weledi sio kumuwekea standards za kipunda punda.
 
Sio lazima lakini
Usiseme sio lazima, umepewa angalizo. Ndio maana hizi biashara zenu zinakuwa hazina maisha marefu sababu ndani yake zimebeba machozi na manung'uniko ya wanyonge ambao wamejikuta wanalazimika kufanya kazi kwa lazima bila kutaka.
 
Hata mim nafahamu hivyo kwamba kufyatua tofauli kwa Gharama ya mfuko mmoja, Mfano huku kwetu mfuko mmoja wa saruji ni 4000- 5000 kutokana na maelewano. Kwahyo raia wakikupigia mifuko 20 ya wanaondoka kama na 80k mpaka 100k.
Yeye anazungumzia tofali zile wazungu wanaita bricks sio tofari za block
 
That's too much bro, mtu akila tangu asbh mpaka jion anabaki na nn hapo? jamn hebu tuwe na utu na hawa vijana wetu. Kama unaweza wape offer ya chakula au walipe per unit, Kila tofali moja mpe mtu mia ili watu wajipimie kazi..natanguliza shukrani.
Halafu tunasema wahindi wanyonyaji daaaah
 
Kama kichwa Cha habari kinavyosema hapo juu natafuta vijana watatu nitaowaajiri waje wafyatue matofali malipo ni 5000 Kwa siku kula juu Yao Kwa waliotayari waje pm mda huu Kwa mnaohitaji nimeamua kutoa ajira Kwa vijana wenzangu Ili tuweze kusonga mbele
Naomba ninunue hiyo biashara yako kila kitu, then nikuajiri uwe mfetua matofali nitakulipa 6500/= kwa siku utajitegemea chakula.
 
Back
Top Bottom