Natafuta Variable Frequency Drive

Khalid91

Member
Joined
Feb 2, 2020
Posts
65
Reaction score
47
Habari wadau,

Ninatafuta kifaa ambacho kitaweza kunibadishia umeme single phase kwenda three phase kwa ajili ya mashine ya kusaga. Mahala kulipo na mashine hakuna umeme mkubwa, upo wa kawaida wa matumizi ya nyumbani.
Kwa anaejua napoweza kupata hiki kifaa ambacho kinaitwa variable frequency drive(VFD) naomba tuwasiliane zaidi PM. Ahsante sana wakuu
 
Sema horsepower,amperage na voltage zipo kwenye motor nameplate, nitakuambia exact what to buy kabla hujaikaanga machine yako
 
Nenda kariakoo mataa wa Gogo na Narung'ombe utapata
ila tegemea power ya motor kupungua
 
Sema horsepower,amperage na voltage zipo kwenye motor nameplate, nitakuambia exact what to buy kabla hujaikaanga machine yako
Horsepower ya kinu cha kukoboa/kusaga ni 25 HP na horsepower ya kinu cha kukamua alizeti ni 20 HP
Voltage 380 - 415 volt.
 
Horsepower ya kinu cha kukoboa/kusaga ni 25 HP na horsepower ya kinu cha kukamua alizeti ni 20 HP
Voltage 380 - 415 volt.
25 HP ni kubwa sana mazee kwa VFD kufanya kazi, nyingi za kubadilisha single phase to three phase ni kwa motor za chini ya 10HP zaidi ya hapo main breaker itakata instantly, solution waite TANESCO wakuwekee three phase au diesel generator, labda wengine wana solution zaidi watasaidia
 
Ahsante sana kwa ushauri mkuu. TANESCO ndio hivyo tena haijulikani wataweka lini na generator ya diesel running cost ni kubwa haitalipa faida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…