Pole mkuu natumaini wale maharamia wa somalia wamekupitia lakini ndio maisha...nenda duka la mastercard pale opp na bigbon shell ukiuliza ukikosa nenda ukanunue hizo zako pale pemben ya bigbon kuna mlango ukiingia ndan uchelewi kuzikuta na namba zako kuzipata usipige kelele just muelewane...aka gerezani...tuliibiwa kioo cha mbele mark2 enzi hizo asbh mzee akaanza kuchchawa kweli ilimuuma maana ilikuwa gari yake kifutajacho..loh....,nikaelekezwa wahi gerezani saa moja niko pale nikakuta muungwana mmoja nkamweleza ukweli akaniambia tulia nikupeleke kwa boss...ana ofisi kabisa ndan nikaenda akaniuliza swali mmoja umetokea wapi nikajbu kimara bucha akasema mzigo wa bucha uko faya subiri dk 10...mzigo ukaingia nikaitwa nikaambiwa una sh ngapi nikajibu 25 nisaidien wakadai 70tukamalizana kwa 45..nikapaata kioo changu kikiwa na namba...jaribu kati ya hizo