Natafuta Nyimbo za zamani za Taarab

Natafuta Nyimbo za zamani za Taarab

Mman'gati huo wimbo wa moyo kwa kweli hata mimi naupenda sana. Kama haujaupata online basi huwa zinapatikana ktk maktaba ya TBC Taifa huwa zinauzwa hapo. Kam. ulivyosema ni kweli ulipigwa sana wakati wa uchaguzi wa 95 nafikiri siku hiyo RTD walikesha kwa mara ya kwanza kabisa.
 
Last edited by a moderator:
mwenye wimowa kijungumarehmu Prof mohamed rsho na marehemu leila khatibu kama maneno risasi
 
Nani kapiga hii ngoma?nilidhani wewe Chanda na mimi Pete yake

marehemu issa matola alokuwa mumewe Hadija kopa wa kwanza kabisa na ndo alomfunza kazi kisha akabwagwa.
ndipo alipomuimba kwenye huu wimbo
 
hauvumi lakin umo lilikuwa dongo kwa nasma hamis kidogo baada ya nasma kuvuma sana na nyimbo taarab imo humo ambapo lilikuwa dongo kwa kh. Kopa
 
ni moyo ooh ulonichongea, ulinihadaa kuwa wanipenda, ukanichanganya mwishowe ukaniachwa pweke! maumivu umeniachia...
 
100.5 Times fm jumapili saa tatu asubuhi mpaka tano mwambao asilia
 
wallah nyimbo za zamani nzuri zina ujumbe hasa...mie naipenda nyimbo moja ya Babloom MWAMBIENI,na band nyengine za znz Amin nnakupenda,Chanda na pete,Pita,kukupenda sana ndio kosa langu,Kwangu amepoa,Nimpende nani? maneno yake matamuuuuuuuuuuuu.............
 
hauvumi lakin umo lilikuwa dongo kwa nasma hamis kidogo baada ya nasma kuvuma sana na nyimbo taarab imo humo ambapo lilikuwa dongo kwa kh. Kopa

lakini kwa wakati ule hadija mwenyewe alimkubali Nasma kumbuka "kinyago cha mpapaure" Nakumbuka TOT walivunja Jukwaa Vijana Hall kinondoni ilikuwa "twaarab" sio rtusha roho matusi matupu
 
kuna ule Wimbo wa Sanamu la MICHELIN wa Nasma Khamis Kidogo lilikuwa Dongo kwa Hadija Koppa,pia kuna Usikalifishe Nafsi,Riziki Mafunga Saba,Zoa Zoa,Msabasi hizi zote ni za East Africa Melody za miaka mwanzoni wa 2000,na hawa ndio waanzilishi/walioleta hii Modern Taarab ya sasa japokuwa imechakachuliwa sana sasa hivi.
 
marehemu issa matola alokuwa mumewe Hadija kopa wa kwanza kabisa na ndo alomfunza kazi kisha akabwagwa.
ndipo alipomuimba kwenye huu wimbo

Nilikuwa sijui kumbe ndo alikuwa mume wa khadija?ila napenda sana nyimbo za huyo baba
 
Sina link ila Bongoradio wana Taarab channel, ambayo kama unalipia kwa data itakuwa haikufai.

Mdudu eeeee, mdudue ee, kaingiaje x 2
Mdudu ndani ya kokwa la embe, kaingiajeee?
 
Times FM wana kipindi cha Mwambao Asilia kila Jumapili kuanzia saa tatu asubuhi. Huwa wanacheza nyimbo za Taarab za zamani.
 
Asalaam... naomba km kuna mwenye nyimbo za taarab za zamani anitumie link
Huu sio wa zamani sana, lakini naupenda kuliko maelezo. Furahia...

 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom