hakuna binadam chini ya jua aliye mkamilifu hata kidogo..yawezekana nilimkwaza mwenzi wangu kwa namna moja au nyingine.. Lakini nakiri itakuwa bila makusudio ya kumuumiza..labda kwa bahati mabaya.. Na nilikuwa mwepesi wa kuomba msamaha....nasema yawezekana nilimkosea bila kukusidia( kwasababu katika makosa ya wazi wazi sikuwahi kumtenda hata moja....( sikuwahi kumtukana hata nyokoo,sukuwahi kumsukuma japo kwa ukucha..ingawa alikuwa akinihamakisha kwa maneno mpaka..ila nilikuwa nampuuza na kuondoka zangu)..sikuwahi kumwendea kinyume...napale alipokuwa na mashaka na mienendo yangu niliweka wazi kila kitu(simu yangu,angeweza kuipekua hata na kukaa nayo apendavyo namimi haikuwa shida kwangu)..! Nadhani dhambi kubwa niliyomtendea tena bila kukusudia ni kutokuwa na kipato kinacholingana na hadhi yake..( maana siku zote umvi wetu ulikuwa huo,,, kwanini hatuendelei,..kwanini hatuwezi kununu gari kama wanaume wenzio,kwanini huwezi kujenga nyumba kama wanaume wenzio? Na ukumbuke pato langu yeye ndiye alikuwa mpangaji wa matumizi..nini kinunuliwe nini kisinunuliwe..! Nakiri kuwa ktk upande wa kipato sikutimiza ndoto zake za magari na majumba mazuri..lakini nilikuwa nikijitahidi na nikimweleza kuwa avute subra..maana tumo tunatafuta..>!