Natafuta muwekezaji kwenye Biashara ya Photography, Video Production na Graphics Design

Professor X

Member
May 29, 2020
45
60
Mimi ni kijana wa kitanzania Lengo La Kuja hapa ni kuomba msaada wa uwekezaji katika biashara ya VIDEO PRODUCTIN, PHOTOSHOOT and GRAPHICS DESIGN ili aweze kusaidia upatikanaji wa vifaa vitakavyo wezesha kufanya kazi vyenye thamani ya shilingi 6M (Million Sita).

Mtaji wangu utakuwa ni Uaminifu, wazo, Nguvu ma Muda Halafu Boss yeye Atawekeza katika hii project alafu tupange , nikae kama Business partner (tufanye Kazi alafu tuwe tunagawana faida Kulingana na mzunguko wa biashara Katika Asilimia ) Au niwe mwajiliwa wake nikisimamia kila kitu katika kazi alafu ye anilipe mshahara wangu wa kila mwezi

1.Video Light kit

2.CAMERA Canon 60D 1,500,000 na Canon mark 3 5D

3.Boya mic

4.Speed light

5.Strobe

6.Background

7.lens

8.memorycard

9.Stand

10.Compute

11.Reflactor

12.Printer

KUHUSU MIMI

Mimi ni kijana wa kiume nina miaka 23 Elimu yangu ni kidata cho sita (siyo kwamba nilifeli hapana nimeshindwa kwenda chuo kutokana na changamoto za kifedha kuzimudu) Ni mzaliwa wa MBEYA MJINI na ndipo ninapo ishi kwa sasa

UZOEFU WA KAZI

Ni Mjuzi wa maswala ya VIDEOGRAPHY, PHOTOGRAPHY, FILMMAKING, GRAPHICS DESIGN, STORY WRITTER, Nimejifunza aya kwa mda wa miaka mi nne sasa sijaingia darasani ila nimekuwa nikijufunza kutoka kwa watu mbali mbali wenye ujuzi na aya maswala na kwa hapa nilipo nimefika sehemu naweza fanya kitu mwenyewe kwa uzoefu nilio nao

MAWASILIANO YANGU

0743150860 Voda 0688176045 Airtel

Natangulisha shukurani zangu za zati kwenu
 
Mkuu ungeambatanisha na baadhi ya kazi ulizokwisha fanya, itarahisisha kupata muwekezaji
Hapa ndo changamoto inapo kuja nimekuwa mwanafunzi wa hii fani na kusaidiana na watu tu katika kufanya kazi lakini mimi mwenyewe sina kazi nilio wahi fanya kasi ninazo fanya kwa sasa ni graphics na photshoot lakini nina ujuzi wa kutosha wa hayo niliyo yaolozesha hapo japo sina kazi nilio wahi fanya nikutokana na changamoto za vifaa .kama utapata mda pita insta #TeteMwamba
 
Mkuu ungeambatanisha na baadhi ya kazi ulizokwisha fanya, itarahisisha kupata muwekezaji
Izi ni baadhi ya kazi nilizo wahi kufanya
FB_IMG_1626233992232.jpg
FB_IMG_1626233974858.jpg
FB_IMG_1626233951478.jpg
tetemwamba-20210714-0009.jpg
tetemwamba-20210714-0008.jpg
tetemwamba-20210714-0005.jpg
tetemwamba-20210714-0002.jpg
tetemwamba-20210714-0006.jpg
tetemwamba-20210714-0004.jpg
 
Safi sana na kila la kheri kwenye tasnia (carrier) yako hiyo.

Ila kwa ushauri wangu nadhani ungejikita kwenye eneo hili la Video na Photograph na ufanye bidii uwe mahiri haswa...hapo naona umejumuisha 'storywriting' ingawa nadhani unamaanisha 'script writing'...si mbaya ingawa hili nalo ni eneo linalojitegemea na si kama wengi tunavyojaribu kulipa wepesi.

Ila kama pia unatamani kuwa Sript Writer basi ujue kuna kazi ya kufanya ili kupata umahiri huo tofauti na kutanguliza tu kipaji.

Pambania Video production uwe Mahiri kama kina Adam Juma n.k...then baadae unaongeza na hizo kada nyingine unazozitamani.
 
Jitahidi Kushiriki vizuri katika matukio ya kijamii. Huku ndipo connection zinapatikana kwa haraka.
Usisubiri kuambiwa nenda Kanisani.
Pub & restaurant by
Attend sherehe mbalimbali
We foc tu connection na kama utapata camera yako we zuga nayo itakutengenezea jina
Asante mku ulichosema ni kweli huwa najitahidi kushiriki matukio mbali mbali, lakini changamoto imekuwa ni vifàa, umekutana na mtu anakwambia haàaaa ungekuwa na vifaa tungefanya kazi hapo cha zaidi unajitahidi tu kujenga ukaribu nae ujifunze mawili matatu ila changamoto kubwa kwa sasa upande wangu ni VIFÀA kwo yoyote aliye tayari ata kunidhamini , ntamlipa taratibu kuendana na mzunguko wa kazi
 
Safi sana na kila la kheri kwenye tasnia (carrier) yako hiyo.

Ila kwa ushauri wangu nadhani ungejikita kwenye eneo hili la Video na Photograph na ufanye bidii uwe mahiri haswa...hapo naona umejumuisha 'storywriting' ingawa nadhani unamaanisha 'script writing'...si mbaya ingawa hili nalo ni eneo linalojitegemea na si kama wengi tunavyojaribu kulipa wepesi.

Ila kama pia unatamani kuwa Sript Writer basi ujue kuna kazi ya kufanya ili kupata umahiri huo tofauti na kutanguliza tu kipaji.

Pambania Video production uwe Mahiri kama kina Adam Juma n.k...then baadae unaongeza na hizo kada nyingine unazozitamani.
Shukrani mkuu hili nalo ntalifanyia kazi japo kwa upande wangu natamani kujikita sana na video and photo japo changamoto ndo izo ndogo ndogo vitendea kazi ila asante kwa ushauri mkuu
 
Back
Top Bottom