Natafuta muwekezaji(investor) wa Shilingi milioni 2.5 tu

Habari wana JF!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Natafuta mtu wa kuja kuwekeza Milioni 2.5 tu katika biashara ya kusaga na kukoboa mahindi pamoja na kuuza viroba vya sembe na dona, Viroba vitakuwa kwa mfumo wa 25kg, 10kg, 5kg. Kila kitu kipo cha kuweza kusagisha na kukoboa mahindi na kuufunga katika viroba. Ufuatao ni mtiririko wa manunuzi, mauzo na mgao wa pesa kwa muwekezaji na mmiliki wa mashine;

Manunuzi:
Tani 2(kg 2,000) za mahindi kwa wiki
Bei ya kg moja ni Tshs 500
Bei ya kg 2,000 ni Tshs 500×2,000= Tshs 1,000,000/=

Uzalishaji:
Kwa Tani mbili zinatoa,
Wastani wa viroba vya 25kg= 56
Magunia 6 ya Pumba

Mauzo:
Viroba 56
Kila kiroba kwa sasa ni Tshs 19,000/=
56 X 19,000/=1,064,000/=
Magunia 6 pumba@15,000=90,000/=
Jumla kwa Tani mbili ni 1,064,000+90,000=1,154,000

Usagishaji:
Kusagisha kwa siku wastani Tshs 20,000/=
Kwa wiki 120,000/=
Kwa mwezi 480,000/=

Faida:
Unga kwa Tani mbili kwa wiki ni Tshs. 154,000/=
Kwa mwezi ni Tshs. 616,000/=
Usagishaji kwa mwezi ni Tshs.480,000
Jumla faida wastani ni 1,096,000/=

Matumizi:
Umeme+Ushuru kwa mwezi ni Tshs. 50,000/=
Mfanyakazi fundi kwa wiki ni Tshs. 50,000/=
Kwa mwezi ni Tshs. 200,000
Mfanyakazi wa kupepeta wiki ni Tshs. 21,000/=
Kwa mwezi ni Tshs. 84,000/=
Fremu kwa mwezi Tshs. 200,000/=
Jumla Tshs. 534,000/=

Faida Halisi (Net Profit ):
Tshs. 1,096,000-Tshs.534,000 = Tshs. 562,000/=

Mgao:
Mgao kwa investor Tshs. 250,000/=@mwezi
Kwa miezi 15 ni Tshs. 3,750,000/=
Net Profit yake:
Tshs. 3,750,000- Tshs. 2,500,000= Tshs. 1,250,000/=
Mgao kwa mmiliki wa mashine kwa mwezi ni Tshs. 312,000/=

Note:
Huo ni mgao wa mtaji wa Tani mbili ambao ni Tshs. Milioni moja. Milioni 1.5 inayobakia itatumika kuhamishia mashine kuipeleka barabarani-kwenye soko zaidi (Nyerere road-Barabara ya Gongo la Mboto hadi Chanika)na ayo ni mahesabu pindi ilipokua majohe (Gongo la Mboto kwa ndani) ambapo haya ni makadirio ya chini ya mauzo kuliko uko inapopelekwa/itapopelekwa (hivyo tegemea kua kwa ongezeko la mgao wa faida kwa muwekezaji kwa kila mwezi). Lengo ni wote wafaidike-Muwekezaji na Mmiliki.

Pia kutakua na kuingia mkataba wa kimaandishi wa miezi 15 na kushuhudiwa na mashahidi wa pande zote mbili.

Namkaribisha Muwekezaji
Mambo sio rahisi namna hii kwenye nchi ambayo Waziri anaweza akaamka na kujitungia Tozo za ajabu ajabu kwa kuziita za kizalendo!

Kwa nchi ambazo government policies ziko imara ningekubaliana na hii assesment!
 
Mambo sio rahisi namna hii kwenye nchi ambayo Waziri anaweza akaamka na kujitungia Tozo za ajabu ajabu kwa kuziita za kizalendo!

Kwa nchi ambazo government policies ziko imara ningekubaliana na hii assesment!
Kwanza unatakiwa ufahamu hii ni biashara ya chakula sio biashara ya miamala yenye tozo za ajabu ajabu (kama ulivyoziita)
Pili nina uzoefu wa mwaka mmoja na hii biashara, ayo mahesabu sijakurupuka najua nn nafanya.
Anyway nashukuru kwa mchango wako
 
Dah.
Hiyo biashara week hii nimeiwaza sana. Kuna eneo kiwanja kinauzwa nilitaka kununua ili nifunge mashine nianze hiyo kazi. Tatizo upo mbali sana japo nipo Dar. Ningeweza hata mara 3 ya 2.5.
Mkuu kama unaona kuwekeza inaweza kuishia kwny kugombana, unaweza ukaja nikakuuzia kila kitu kuhusu hii mashine pamoja na vifaa vyake pia na kukukabidhi umeme wa three phase. Nitakuuzia Milioni 5 na ukiwa unataka kuihamisha nitakupunguzia bei.
Karibu tuzungumze!
 
Kwanza unatakiwa ufahamu hii ni biashara ya chakula sio biashara ya miamala yenye tozo za ajabu ajabu (kama ulivyoziita)
Pili nina uzoefu wa mwaka mmoja na hii biashara, ayo mahesabu sijakurupuka najua nn nafanya.
Anyway nashukuru kwa mchango wako
Mkuu mm nakuunga mkono asilimia 100 watu wanaogopa kukuuliza swali la msingi hapa
kama una uzoefu na hii biashara kwanini ulishindwa kutoboa ama Ku reis 2500000, am sorry for that bad question.....
 
Mkuu mm nakuunga mkono asilimia 100 watu wanaogopa kukuuliza swali la msingi hapa
kama una uzoefu na hii biashara kwanini ulishindwa kutoboa ama Ku reis 2500000, am sorry for that bad question.....
Nashukuru, ni ivi mtaji umeyumba kwa 75% na kutokana na majukum ya familia nilonayo nisingependa nichukue mkopo badala yake ni hii hapa plan a na plan b ni kutafuta mteja wa kuinunua jumla!
 
Habari wana JF!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Natafuta mtu wa kuja kuwekeza Milioni 2.5 tu katika biashara ya kusaga na kukoboa mahindi pamoja na kuuza viroba vya sembe na dona, Viroba vitakuwa kwa mfumo wa 25kg, 10kg, 5kg. Kila kitu kipo cha kuweza kusagisha na kukoboa mahindi na kuufunga katika viroba. Ufuatao ni mtiririko wa manunuzi, mauzo na mgao wa pesa kwa muwekezaji na mmiliki wa mashine;

Manunuzi:
Tani 2(kg 2,000) za mahindi kwa wiki
Bei ya kg moja ni Tshs 500
Bei ya kg 2,000 ni Tshs 500×2,000= Tshs 1,000,000/=

Uzalishaji:
Kwa Tani mbili zinatoa,
Wastani wa viroba vya 25kg= 56
Magunia 6 ya Pumba

Mauzo:
Viroba 56
Kila kiroba kwa sasa ni Tshs 19,000/=
56 X 19,000/=1,064,000/=
Magunia 6 pumba@15,000=90,000/=
Jumla kwa Tani mbili ni 1,064,000+90,000=1,154,000

Usagishaji:
Kusagisha kwa siku wastani Tshs 20,000/=
Kwa wiki 120,000/=
Kwa mwezi 480,000/=

Faida:
Unga kwa Tani mbili kwa wiki ni Tshs. 154,000/=
Kwa mwezi ni Tshs. 616,000/=
Usagishaji kwa mwezi ni Tshs.480,000
Jumla faida wastani ni 1,096,000/=

Matumizi:
Umeme+Ushuru kwa mwezi ni Tshs. 50,000/=
Mfanyakazi fundi kwa wiki ni Tshs. 50,000/=
Kwa mwezi ni Tshs. 200,000
Mfanyakazi wa kupepeta wiki ni Tshs. 21,000/=
Kwa mwezi ni Tshs. 84,000/=
Fremu kwa mwezi Tshs. 200,000/=
Jumla Tshs. 534,000/=

Faida Halisi (Net Profit ):
Tshs. 1,096,000-Tshs.534,000 = Tshs. 562,000/=

Mgao:
Mgao kwa investor Tshs. 250,000/=@mwezi
Kwa miezi 15 ni Tshs. 3,750,000/=
Net Profit yake:
Tshs. 3,750,000- Tshs. 2,500,000= Tshs. 1,250,000/=
Mgao kwa mmiliki wa mashine kwa mwezi ni Tshs. 312,000/=

Note:
Huo ni mgao wa mtaji wa Tani mbili ambao ni Tshs. Milioni moja. Milioni 1.5 inayobakia itatumika kuhamishia mashine kuipeleka barabarani-kwenye soko zaidi (Nyerere road-Barabara ya Gongo la Mboto hadi Chanika)na ayo ni mahesabu pindi ilipokua majohe (Gongo la Mboto kwa ndani) ambapo haya ni makadirio ya chini ya mauzo kuliko uko inapopelekwa/itapopelekwa (hivyo tegemea kua kwa ongezeko la mgao wa faida kwa muwekezaji kwa kila mwezi). Lengo ni wote wafaidike-Muwekezaji na Mmiliki.

Pia kutakua na kuingia mkataba wa kimaandishi wa miezi 15 na kushuhudiwa na mashahidi wa pande zote mbili.

Namkaribisha Muwekezaji

Bei ya kilo ya mahindi inategemea pia ni yawapi...na saivi kilo ni 420 mpk 460 ambayo hapo umeapproximate to 500...kwaiyo investor anaeza pata more kutokana kwamba umempa General view tu....watu wachangamkie fursa hii ni nzuri sana
 
  • Thanks
Reactions: hnp
Hiv kwann watu wanaotafuta wawekezaji hapa JF huwa hawataki wawekezaji wa kudumu ? Yan wanatafuta wawekezaji wa muda mfupi kuanzia mwaka had miaka miwili then mwekezaji aondoke aache kila kitu kwako , nadhan sio fair na haivutii kwa kiasi fulan kama ikiwa permanent nadhani ingevutia zaid uwekezaji
 
Back
Top Bottom