Dada yangu kama kweli unasoma biblia utajua ni jukumu la mwanaume kumfuata/kumfuata mwanamke ambaye anataka kumuoa.
Kwenye biblia mwanamke yoyote ambaye alikuwa anafuata mwanaume lazima alikuwa na kasoro fulani kubwa
Pia Chema chajiuza, kibaya chajitembeza
Dada yangu sikufahamu ila kwa kuwa tuna imani moja, nikwambie kuwa wewe ni wa thamani sana.
Mwombe Mungu akuletee mwanaume ambaye anaweza kusimama kama mume katika nyumba yako.
Jitathmini je wewe una sifa za kuwa mke wa mtu
Unamtegemea Mungu, unavaa kiheshima, una tabia njema, unaweza kuwa mama na kulea watoto, unafahamu biblia inasema nini kuhusu kuwa mwanamke n.k
Ukija humu unaweza ukapata mwanaume anayefaa lakini chance kubwa zaidi utakutana na vibwengo waliokataliwa huko na wengine kwa kushindwa kuwa na vigezo vya Kichwa cha familia,
Akaja akakufanya upoteze hata hiyo imani uliyo nayo
Piga maombi na jitathmini kama umesimama katika imani
Amini katika muda aliokutengea Mungu nawe utapata bdoa nzuri usiwe na pupa
Habari,
Mim ni msichana 31 natafuta mume wa kunioa. Nimeokoka na mpenda Yesu, sina mtoto nina elimu ya chuo kikuu ila nimejiajiri mwenyewe nafanya biashara.
Sifa za mume awe na hofu ya Mungu na kuishi katika njia zimpendazo Mungu, awe amejiajiri au anafanya kazi.
Karibu pm kwa maelezo zaidi.