Natafuta kiwanja cha milioni 4 Dar, nitapata wapi?

Natafuta kiwanja cha milioni 4 Dar, nitapata wapi?

Njoo mpiji magoe huku Viki vingi
 
Sogea hapo panaitwa MBZ Barabara ya Goba
 
Mpiji mbali sana kutoka Morogoro road (10km+).
Kumepakana na pori la Mabwe (usalama mdogo).
Hapafai.
Nafkir hujaenda siku za hv karibuni
Katikat ya lile pori kunajengwa hotel kubwa sana ,na pia wanatengeneza mazingira yawe ya kitalii

Afu pia Barabara ya lami mda c mrefu itapita kule ,hii itaongeza movements ambazo zitapunguza uhalifu kwa asilimia kubwa
 
Km 10+ ni mbali? Hili jiji ukiwa na usafiri hakuna mbali
Mwambie huyo aache uoga

Kutoka stand ya magufuli mpaka bunju B kupitia njia ya mpiji ni 25km tuu .....Hii Barabara ikijengwa kiwango Cha lami .... itaongeza sana thamani ya maeneo ya kule

Na ni Barabara ambayo ni lazima ije kujengwa kiwango Cha lami coz kuna vitu vingi vinachangia hilo

1) Ma bus yaendayo kaskazini ndo itakua Barabara yao
2) Kuna hospital kubwa ya rufaa imejengwa pale mabwepande... Mkuu wa wilaya aligoma kuizindua coz Barabara ni mbovu
3) Daladala zimegoma kufanya route kutokana na ubovu wa Barabara
4) Kuna kituo Cha Ma bus ya kaskazini kinatakiwa kijengwe pale bunju ...ili kurahisisha usafiri ....(km wanavyofanya kule vikindu kwa ajili ya magari ya kusini)


Haya yote yanachangia Serikali iweke mipango ya kujenga Barabara kule
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom