natafuta kifaa cha kujanga hatch kama hii ya mwezi mchanga
Kiongozi hapo tunatumiaga plywood na mbao tu, hakuna hicho kifaa (na hata ukipata unaweza ukakuta vipimo haviendani)
Chukua plywood, kata vipande vinavyolingana na unene wa tofali ulizotumia uviloweke kwenye maji
Laza ubao wa 1x6 au 1x5 usawa wa nguzo zinapoishia, ambapo chini yake utapigilia mirunda kuushikilia.
Kata vibao kulingana na vipimo vya Arch yako, anza na ubao wa kati kati (unapima urefu kutoka kati kati ya ubao uliolaza mpaka kwenye arch hapo juu)
Utapigilia hivyo vibao kutengeneza pattern inayofanana na spoku za tairi la baiskeli kisha ukimaliza utalaza kipande cha plywood juu ya hivyo vibao na kugongea misumari.
Ni bora umeuliza, maana kama ndio ungekuwa unajenga mbali kwa kupiga simu, fundi angeweza kukudanganya kwamba kifaa kipo na kinakodishwa 50,000/=
Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane