Watu mna maswali ya kiwaki kichizi.
Dogo hata uandishi tu ni kamzozo, mtu anamletea jitabu la page 400, mwingine nae anakuja na mswali kibao mpaka hesabu.
Kama umeamua kumsaidia msaidie, mawasiliano kaweka hapo, mpigie mfanyie interview, ukiridhika nae mchukue.
Sio mnaanza kujichukulia point 3 kwa dogo alaa.
Kijana viwanda daily vinahitaji watu ni nguvu zako tu.
Bakhresa pale ni tin na barua ya mtendaji tu.
Ubungo garage kiwanda cha sabuni ni account ya crdb tu.
Kiwanda cha nguo external pale ni nida na kitambulisho cha mpiga kura.
Pepsi pale vingunguti ni kuwahi kwako nadhani jumamosi ndo huwa wanachukua vibarua.
Na kama huna namba ya nida fanya uitafute na uwe nayo ni muhimu sana hapa mjini, uwe na tin namba bila kusahau paspot zakp hata 6, siku kikinuka popote unapeleka nyaraka zako hizo.
Ukijipata tafuta leseni.