Natafuta chumba magomeni mapipa

Natafuta chumba magomeni mapipa

integral sign

Senior Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
160
Reaction score
13
Vifuatavyo mi muhimu sana.
1. Maji yakiwa ya dawasco itakuwa poa zaidi
2. Umeme
3. Masharti magumu yasiwepo kwani utalipwa pesa yako yote tutakayokubaliana.
4. Kisiwe mbali na main road hasa morogoro road.
5. Kisiwe bondeni hasa ktk maeneo ambayo yamezuiwa na City(yanafahamika).
6. Sehemu iwe na utulivu kiasi yaani isiwe karibu na bar,kumbi za starehe.

Asanteni, nipeni ofa zenu.
 
Unaenda kwa wauza unga na matapeli mapipa utaweza? Kama una mke usipange maeneo hayo
 
Duh, yaani nakuonea huruma na sijuwi tu nianzie wapi maana Magomeni bwana kuna ya hajabu kwani karibia kila mtu ana sifa za kiharamia. Zifuatazo ni sifa za Magomeni na vitongoji vyake: Karibia kila nyumba ina (ma)teja ama muuza unga, makahaba, majambazi, punda, vibaka, wauza matap tap, danguro la ngono (guest bubu), waganga wa kienyeji, maji ya mto msimbazi yenye kila aina ya maradhi wakisingizia ya Dawasco, na maajab mengi tu ya kuifanya Magomeni kuwa jehanam ya kisasa. Pole lakini.
 
Back
Top Bottom