Nashukuru Mungu Tanzania nimeimaliza

Nashukuru Mungu Tanzania nimeimaliza

We Kiboko Mkuu.Sasa Ebu Niambie Tabia Za Wanawake Wa Kipogoro,maana Demu Wangu Ni Kabila Hlo,
 
Nzalendo; Heshima yako Mkuu. Kuna maswali mengine hukuyajibu, sijui hukuyaona ama la? Ila lipo moja naomba nikukumbushe liliulizwa na mdau mmoja hivi, aliuliza, 'ni mabinti wa mkoa/wilaya ipi wazuri kwa kuoa? Yeye anatafuta wa kuoa!' Nahisi nimelipatia swali lake, nawe utalijibu kwa hekima zote, maana ni kijana wako huyo anahitaji mke (kijana wako, kwa umri wako ulioutaja).

Nami naomba niulize hili, labda utaunganisha majibu na nitashukuru ukiunganisha. Ni hili, 'Mkoa wa Mara, eneo linaloitwa Shirati, lipo Rorya ama Nyancha? Maana nachanganya haya, na vipi kuhusu tabia ama ukaribu wa watu wa huko? Nao ni wa kabila gani, wasurwa ama wagire?'

Nimemaliza Mkuu, nitafurahi ukinijibu, naamini umenipata.

Ahsante!
 
Ila nashukuru nimejifunza mengi kupitia maada hii, kwa waliouliza na kujibiwa, na kwa waliojibu pia, hasa majibu yako mleta maada, nimeyakubali sana.

Kwa waliotukana ama kukashifu, niwe mkweli tu, sikujifunza lolote tokea kwao.

Ahsante!
 
Mkuu sio nia yangu kufanya haya ninayoyafanya. Ninachojaribu kufanya ni kuwa "watch dog", kuwasaidia moderators katika kurekebisha tabia za baadhi ya wanachama hapa JF. Wanachama wengine wanakera sana. Wanaanzisha topiki ambazo hazina kichwa wala miguu.
Moja ya nyuzi bora kabisa ya mwezi huu.
 
Nzalendo; Heshima yako Mkuu. Kuna maswali mengine hukuyajibu, sijui hukuyaona ama la? Ila lipo moja naomba nikukumbushe liliulizwa na mdau mmoja hivi, aliuliza, 'ni mabinti wa mkoa/wilaya ipi wazuri kwa kuoa? Yeye anatafuta wa kuoa!' Nahisi nimelipatia swali lake, nawe utalijibu kwa hekima zote, maana ni kijana wako huyo anahitaji mke (kijana wako, kwa umri wako ulioutaja).

Nami naomba niulize hili, labda utaunganisha majibu na nitashukuru ukiunganisha. Ni hili, 'Mkoa wa Mara, eneo linaloitwa Shirati, lipo Rorya ama Nyancha? Maana nachanganya haya, na vipi kuhusu tabia ama ukaribu wa watu wa huko? Nao ni wa kabila gani, wasurwa ama wagire?'

Nimemaliza Mkuu, nitafurahi ukinijibu, naamini umenipata.

Ahsante!
Naam kuhusu kuoa
Kwa ujumla wanawake wengi wa kitanzania karibu wote wanafanana...hasa jamii ya kibantu.
Hivyo basi ki ujumla cheki moyo wako uko wapi,hapa angalizo angalau awe kapata Elimu lakini asiwe ameathiriwa na mambo ya ki magharibi.Katika kupita pita kwangu kuna sehemu za Mkoa wa Njombe wapo Wabena ni wavumilivu sana.

Kuhusu shirati ni muda mrefu nilipita huko,wakati Kanali Mlay yuko Buhemba..sina kumbukumbu vizuri ila ninachokumbuka,kuhusu watu wa huko ni mapanga,watu hawapendi masihara sana,ukiwazingua wanakugecha...pia nilikula ugali wa rangi ya brown kama vile umepikwa kwa ulezi na kwa mbali unavutika kama muhogo,kwa mazingira niliyokuwepo wakati huo gongo na bangi ilikuwa ni jambao la kawaida,kuhusu kabila sikumbuki vizuri ila rafiki zangu wengi walikuwa ni wajaluo na wana jamaa zao kenya.
 
Naomba kuifahamu moshi

Kwa miaka hiyo Moshi ulikuwa mji uliodumaa.
Kwa sasa sina uhakika sana inafananaje,ila kwa kifupi ni mji uliopangika.
Miaka hiyo usafiri wa kwenda Arusha zilikuwa ni Ford, na kuna basi lilikuwa linaitwa Kindokyakombe, kwa wanaokwenda Marangu na Rombo Investment kwa wa Rombo.Kiborloni ilikuwa maarufu kwa kuuza mitumba,na nyama ya nguruwe na pombe aina ya mbege.
Nakumbuka sehemu iliyokuwa inaitwa YMCA karibu na keep left...sijui kama bado ipo.
Kwa msimu wa joto Moshi ni mkoa wenye joto kali kuliko Mikoa yote ya Tanzania,Hivyo hivyo kwa kipindi cha baridi.
 
Hongera sana. Ni rekodi nzuri. Mi natamani kabla ya miaka 30 niwe nimekanyaga mikoa yote ya Tz. Nimebakiza Manyara, katavi na Rukwa, Mtwara, Lindi na Pemba.
Hongera sana,nakuombea dua Mungu akuwezeshe ili ufanikiwe.
Ukienda Lindi unganisha na Mtwara kwa safari moja,Pia Katavi na Rukwa ziweke pamoja.
Ni jambo jema sana kuielewa nchi yako.
That's Bravo keep it up.
 
Daaah! Sawa Mkuu Nzalendo, ninashukuru kwa jibu lako kwangu hapo juu.

Ila nilicho-note kutoka kwako (Nahisi lakini), ulikuwa MwanaJeshi, na kwa kazi hiyo, nina imani kweli umeizunguka nchi hii vya kutosha..

Ahsante!
 
Nimejifunza mambo mengi hapa .
Nzalendo hongera sana, pia Nikutakie maisha mema na marefu yenye furaha tele. Zaidi, leta mambo mengi kuhusu uzuri wa nchi yetu uliyoyaona ili tujifunze zaidi.
Nami naomba nifikie hatua hii maana ni fursa chache sana kutokea kwetu.
Hata walio sema vibaya nao tunajifunza tabia zao hapa hapa katika jamvi [JF].
 
Si kitu rahisi,Kwa umri wangu wa miaka sitini na...++ namshukuru mwenyezi Mungu saana,manake nchi hii nimejaaliwa kukaa angalau kila wilaya ya Tanzania Bara kwa kipindi kirefu.

Nina uhakika hakuna Mtanzania yeyote anayeifahamu nchii hii vizuri kuliko mimi.

Hivyo basi namkaribisheni kwa anayehitaji ushauri kuhusu sehemu yeyote ya nchi ya Tanzania.

Namshukuruni sana.
Mkuu unapafahamu kabhulanzwili naomba unielekeze njia ya kwenda huko. Ipo Kasulu. Pua Nelekeze Nyankoronko na kitanga palivyo maana nna reseach huko nataka nijue jinsi ya kufika na watu wa huko wakoje. Natanguliza shukrani
 
Naam swali zuri sana mkuu.
Safari ya kuizunguka nchi hii inaanzia miaka ya hamsini katikati..Mzazi wangu alikuwa mwalimu enzi za mkoloni.
Kwa kifupi mpaka nafikisha miaka 12 nilishakaa Burka(Arusha),Mpwapwa,Mbulu,Korogwe,Pugu,Tabora,na Iringa.
...Kuanzia hapo nikapata shetani wa kupenda nchi hii.....Wakati nafanya kazi nilikwisha kanyaga kila Ardhi ya Wilaya unayoifahamu nchi hii.(kuna siku nililala kwenye nyumba aliyo lala mwalimu nyerere akiwa kwenye harakati za kutafuta uhuru.....nyumba hii ipo Ruvuma Barabara inayokwenda Namtumbo Upande wa kulia kabla hujafika njia panda ya Chengena)
Hii nyumba naifahamu na hili uko sahihi, vipi lakini kuhusu Nyamahana unaweza kueleza tabia za wakazi wa huko? Ikishindikana nieleze kuhusu tabia za watu wa Njalamatata.
 
Mkuu unapafahamu kabhulanzwili naomba unielekeze njia ya kwenda huko. Ipo Kasulu. Pua Nelekeze Nyankoronko na kitanga palivyo maana nna reseach huko nataka nijue jinsi ya kufika na watu wa huko wakoje. Natanguliza shukrani
Nyankoronko-Nyakitonto
Kitanga-Kwitanga
Kabhulanzwii-???
 
Hakuna namna utakuwa umeshiriki mbio za mwenge toka uhuru! mtanzania wa kawaida hawezi zurura hivyo hata kampeni za uraisi tu wagombea hawakufika wilaya zote!
 
Mkuu Nzalendo Hongera Sana ... Ila Kuna Watu Tanzania Hii Wanaijua Kuzidi Hata Wewe Na Hilo Halina Ubishi ... Kuna Mwalimu Anaitwa SHESHUNDA Pale LITI -MOROGORO Wala Humfikii ...
 
Back
Top Bottom