Nashukuru Mungu Tanzania nimeimaliza

Nashukuru Mungu Tanzania nimeimaliza

nzalendo

Platinum Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,901
Reaction score
14,611
Si kitu rahisi,Kwa umri wangu wa miaka sitini na...++ namshukuru mwenyezi Mungu saana,manake nchi hii nimejaaliwa kukaa angalau kila wilaya ya Tanzania Bara kwa kipindi kirefu.

Nina uhakika hakuna Mtanzania yeyote anayeifahamu nchii hii vizuri kuliko mimi.

Hivyo basi namkaribisheni kwa anayehitaji ushauri kuhusu sehemu yeyote ya nchi ya Tanzania.

Namshukuruni sana.
 
Si kitu rahisi,Kwa umri wangu wa miaka sitini na...++ namshukuru mwenyezi Mungu saana,manake nchi hii nimejaaliwa kukaa angalau kila wilaya ya Tanzania Bara kwa kipindi kirefu.

Nina uhakika hakuna Mtanzania yeyote anayeifahamu nchii hii vizuri kuliko mimi.

Hivyo basi namkaribisheni kwa anayehitaji ushauri kuhusu sehemu yeyote ya nchi ya Tanzania.

Namshukuruni sana.


The paragraphy two ya maelezo yako haiwezi kuwa na ukweli au kuandikwa na mtu anayejielewa.....
 
Nimehamishiwa kikazi NKASI Rukwa, naomba unisaidie tabia za wenyeji wa huko, tamaduni zao nakadhalika
Ni waungwana sana, pia shukuru Mungu maeneo ya huko kuna fursa nyingi hasa kilimo na ufugaji.
Wenyeji ni wachapa kazi na pia hupenda kujiburudisha na kinywaji cha nafaka baada ya kazi.
Baadhi ya watu watakutisha kuusu imani giza..ipo lakini mpaka umuanze mtu.
Pia wenyeji wana ngoma zao za tofauti na sehemu nyingine,hutumia chungu.... kina geuzwa upside down halafu kigoda cha kukalia hutumiwa ku scratch na kutoa mlio wa kipekee....
ni raha sana.
 
Labda aeleze alikuwa anazunguka kwa uhamisho, utafiti, biashara au kwa sababu gani ndipo tutaweza kumjaji anavyostahili. Ila kwa kweli kujinasibu hakuna anayeijua hii nchi kamq yeye ni kujidanganya.
Naomba unipe mfano wa mtu mwingine yeyote mwenye uhakika wa kuijua nchi hii.
 
Si kitu rahisi,Kwa umri wangu wa miaka sitini na...++ namshukuru mwenyezi Mungu saana,manake nchi hii nimejaaliwa kukaa angalau kila wilaya ya Tanzania Bara kwa kipindi kirefu.

Nina uhakika hakuna Mtanzania yeyote anayeifahamu nchii hii vizuri kuliko mimi.

Hivyo basi namkaribisheni kwa anayehitaji ushauri kuhusu sehemu yeyote ya nchi ya Tanzania.

Namshukuruni sana.
Acha ujinga wa kujisifia wewe. Eti hakuna mtanzania anayefahamu nchi hii kuliko wewe? Sasa umefanya kitu gani cha maana kama hii nchi unaifahamu kuliko mtu mwingine? Kama huna topiki ya maana nyamaza kimya. Tulia kabisa.
 
Nzalendo uko Vizuri sana. Kuhusu hiyo ngoma ya Wafipa ya kugeuza chungu na kukiparaza kwa kigoda inaitwa KIZANGALA. Kuhusu Nkasi aliyepelekwa huko ukifika upunguze dharau kwa wenyeji, usijependekeze kwa binti zao maana atajitangazia ndoa ndani ya mwezi tuuu tangu umlale. Usiwe mlafi wa vyeo pia
 
Mkuu naomba unijulishe kuhusu tabia za wenyeji wa Ukara. Na zipi fursa za huko?
Mkuu sifa kuu ya huku ni kuna mchanga usio na vumbi waweza oga ziwani ukatembea peku mpaka gheto.
Wenyeji hawana noma na wageni ila kama ukiwachokoza kuna zile imani fulani za kijadi.
Fursa huko ni uvuvi,kama utaweza kuwekeza kwenye mahoteli ya kitalii si mbaya na kuna eneo zuri la kutengeneza golf course
 
Mkuu, kutokana na majukum yangu ya kikandarasi mimi pia nimezunguka sana nchi hii yote pamoja na majiran zake..
Sema ckua mtu wa kukaa muda mrefu kama wewe (Now I am 25 yrs).

Sasa baba (au we ni mama??) nimabie maeneno haya chini yako wilaya gani mkoa gani:

Mshikamano, Ndemdezi, Bushushu, Mwasele na Lubaga.

#Chief Eng.
Hayo unajibiwa hata na mtu aliopo Pyongyang.
 
Back
Top Bottom