Kwa wenyeji wa Ukara hata mie naweza kukumegea japo hukuniuliza mimi: kwanza ni kisiwa ambacho kiko ndani ya Kisiwa cha Ukewere, ni tarafa ya Ukara, ina vivutio vya asili mfano kuna jiwe ambalo wazee wakiliimbia nyimbo wanazozijua wao linacheza lakini wewe mtu mtu hata ungeimba hadi miaka 100 halichezi! wenyeji wa kule wanapenda mchezo wa kupiganisha madume ya ng'ombe kiasi kwamba dume lako likishinda ni sawa na Yanga au Simba wakishinda au kushindwa, pia akina dada wa Ukara kwa utaratibu wao ikifika usiku ndio wanaruhusiwa na wazazi wao kwenda kutembea, mchana marufuku kuzurura ni KAZI TU. Vile vile Ukara kuna wazee wanafuga Mamba, kiasi kwamba hata wakiwa ziwani wanajua huyu ni mamba wa mzee Fulani kama wewe unavyoweza kujua huyu ni ng'ombe wa Fulani, sasa hao mamba huwa wanawatumia kwa mambo ya kiutamaduni! kwa mfano wewe kijana unaweza kumpa msichana wa kikara mimba halafu ukajidai kumtosa, kinachofanyika anatumwa mamba kuja kukuchukua huko uliko hata kama ni Mbeya lazima siku hiyo utajisogeza tu karibu na ziwa au bwawa na huyo mamba anakumeza atakupeleka hadi kwa mzazi wa msichana anakutapika halafu hapo utajibu mashitaka yako ya uharibifu wa binti yao: