Kwa miaka hiyo Moshi ulikuwa mji uliodumaa.
Kwa sasa sina uhakika sana inafananaje,ila kwa kifupi ni mji uliopangika.
Miaka hiyo usafiri wa kwenda Arusha zilikuwa ni Ford, na kuna basi lilikuwa linaitwa Kindokyakombe, kwa wanaokwenda Marangu na Rombo Investment kwa wa Rombo.Kiborloni ilikuwa maarufu kwa kuuza mitumba,na nyama ya nguruwe na pombe aina ya mbege.
Nakumbuka sehemu iliyokuwa inaitwa YMCA karibu na keep left...sijui kama bado ipo.
Kwa msimu wa joto Moshi ni mkoa wenye joto kali kuliko Mikoa yote ya Tanzania,Hivyo hivyo kwa kipindi cha baridi.