Nashawishika kutafuta demu wa pembeni

Nashawishika kutafuta demu wa pembeni

Kipenzi Changu

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
59,220
Reaction score
138,656
Wakuu nimeoa nina mwaka mmoja.

Shemeji/wifi yenu ana mimba,kwa kweli kipindi fulani akawa na mapenzi mazito sana na mimi,kiasi kwamba nikiwa field,wikendi lazima anifate,usiku tunaongea na simu mpaka saa 6.

Bandugu amebadilika ghafla,simu anampa house girl kupokea,text hajibu.

Akichoka kelele za ring tone anazima.

Hata sijui nifanyeje,kazi haziendi huku mbali nilipo.

Daaaah,majanga
 
Anahisi una demu wa pembeni tayari!
 
ni ujauzto tu unaomfanya afanye hayo.. akishusha injini...utaona mabadiliko!
 
Haya mambo yapo tena sana sana...katika dunia hii..
 
Akili zako kama za Boban, sasa utafute mpango wa pembeni kisa hapokei simu, kwani hujui mwenzio homa ya mimba inamsumbua
 
Hovyooo!fanya uzinzi wako ila akijua kusamehe ni ngumu,na uwe tayari kuvumilia kisasi chake,mfanyie unyama mwanamke akiwa mZima,lkn akiwa kwny hyo hali usithubutu,maumivu yake hayasahauliki na ndoa yko bado changa,jiheshim!
 
Vumilia hizo ni hulka za wajawazito wengi, ni kawaida subiri akulete mtoto utafurahi kuitwa BABA !!!!!
 
Wakuu nimeoa nina mwaka mmoja.

Shemeji/wifi yenu ana mimba,kwa kweli kipindi fulani akawa na mapenzi mazito sana na mimi,kiasi kwamba nikiwa field,wikendi lazima anifate,usiku tunaongea na simu mpaka saa 6.

Bandugu amebadilika ghafla,simu anampa house girl kupokea,text hajibu.

Akichoka kelele za ring tone anazima.

Hata sijui nifanyeje,kazi haziendi huku mbali nilipo.

Daaaah,majanga
We usisumbue kichwa, we fanya yanayotakiwa kama wajibu!
kuhusu simu we piga akipokea au asipokee poa! Siku akipokea mwambie unahitaji kuongea na house girl na siye yeye!
 
We usisumbue kichwa, we fanya yanayotakiwa kama wajibu!
kuhusu simu we piga akipokea au asipokee poa! Siku akipokea mwambie unahitaji kuongea na house girl na siye yeye!

ni kama kakusikia mkuu,amenibip ila haongei,anaitika tu.mbona umenichunia?anasema cjakuchunia,ila we ndo upo busy na wanawake wa halmashauri,daaah
 
Haukujiandaa vizuri,jiulize ni kitu gani umekifanya cha kumkera manake mimba za digital zina hasira sana na kuzira..

haah,haah inabidi nicheke,ananambia alipiga cm jana sa 3 uck akakuta nipo busy,eti nilikuwa naongea na wanawake zangu.daah huruma
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom