Tajiri Tanzanite
JF-Expert Member
- Oct 23, 2016
- 2,966
- 5,558
Hapo vip!
Hii hali ya kuichafua nchi imekuwa biashara kwa wanasiasa na wanaharakati fulani fulani.
Kuichafua Nchi ni kitendo cha uhaini na watu hao wanafaa waweke Kwenye list ya maadui wa taifa letu.
Kuichafua nchi inapelekea nchi kujengewa mashaka na wawekezaji ambao walikuwa na nia ya kuja kuekeze kwenye taifa letu..maana yake ni kupotea kwa fursa za ajira ambazo zilikuwa zitolewe kwa Watanzania.
Nchi kukosa ushirikiano wa maendeleo, na misaada kutoka katika mataifa mengine. Haya madhara yote yanamkuta mwananchi na sio mtawala.
Ni wazi hizi sarakasi za akina Lema na watu wanaofanana na yeye zinatokana na aibu ya kukataliwa na wananchi na kwakufanya hivyo wanapata misaada ya kifedha katika mataifa husika waliowapatia hifadhi na watoto wao wanasomeshwa bure.
Nashauri serikali yetu sikivu kwasababu hii tabia inamea na inakuwa kwa kasi. Na watu wenyewe wanaochafua nchi wamechuma sana ndani ya nchi wanaoichafua basi serikali ichunguze mali walizonazo huku kisha wafilisiwe ili wanaposababisha maisha magumu kwa wananchi kwa kuisema na kutangaza nchi vibaya naye asiwe salama kiuchumi.
Sijawahi kusikia wala kuona mataifa ya Ulaya na America wananchi wake wakichafua nchi zao. Mfano mzuri China na Russia hamna Mzungu anayekimbia nchi yake na kujidai mkimbizi.
Hii hali ya kuichafua nchi imekuwa biashara kwa wanasiasa na wanaharakati fulani fulani.
Kuichafua Nchi ni kitendo cha uhaini na watu hao wanafaa waweke Kwenye list ya maadui wa taifa letu.
Kuichafua nchi inapelekea nchi kujengewa mashaka na wawekezaji ambao walikuwa na nia ya kuja kuekeze kwenye taifa letu..maana yake ni kupotea kwa fursa za ajira ambazo zilikuwa zitolewe kwa Watanzania.
Nchi kukosa ushirikiano wa maendeleo, na misaada kutoka katika mataifa mengine. Haya madhara yote yanamkuta mwananchi na sio mtawala.
Ni wazi hizi sarakasi za akina Lema na watu wanaofanana na yeye zinatokana na aibu ya kukataliwa na wananchi na kwakufanya hivyo wanapata misaada ya kifedha katika mataifa husika waliowapatia hifadhi na watoto wao wanasomeshwa bure.
Nashauri serikali yetu sikivu kwasababu hii tabia inamea na inakuwa kwa kasi. Na watu wenyewe wanaochafua nchi wamechuma sana ndani ya nchi wanaoichafua basi serikali ichunguze mali walizonazo huku kisha wafilisiwe ili wanaposababisha maisha magumu kwa wananchi kwa kuisema na kutangaza nchi vibaya naye asiwe salama kiuchumi.
Sijawahi kusikia wala kuona mataifa ya Ulaya na America wananchi wake wakichafua nchi zao. Mfano mzuri China na Russia hamna Mzungu anayekimbia nchi yake na kujidai mkimbizi.