Nashangazwa na wanaoendelea kuumizwa

Nashangazwa na wanaoendelea kuumizwa

muhala.jr

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2014
Posts
751
Reaction score
657
Tangu nilipoumizwa mara ya kwanz Na ya mwisho 2013 cjawah kuumizwa tena.kwann watu wanapenda tena with so much love kulko Ile previous afu wanakuja kuumia tena yan unakuta mtu analia katika relationship hata nne.
 
kila kuumizwa kuna viwango vyake, ukiona hujaumia kabisa hata kidogo ujue basi ulishapoteza sifa ya kibinadamu,

Tunachojitahidi kufanya ni kupunguza kiwango cha maumivu ya mapenzi kutoka maumivu ya miezi au miaka kadhaa na kuwa maumivu ya dakika kadhaa au masaa ama siku kadhaa tu.
 
Tangu nilipoumizwa mara ya kwanz Na ya mwisho 2013 cjawah kuumizwa tena.kwann watu wanapenda tena with so much love kulko Ile previous afu wanakuja kuumia tena yan unakuta mtu analia katika relationship hata nne.
Uliathirika kisaikolojia ulipoumizwa, ndo maana unawashangaa wenzako leo, hata hivyo unajifariji tu, kuumia kuko palepale, sema maumivu yanakuwa ya kiwango cha chini ukilinganisha na ulivyoumizwa 2013, au umeondoka katika ubinadamu yaani unakuwa na mpenzi /mke lakini humpendi na lengo lako umuumize wewe, utakufa ukiwa na dhambi nyingi sana
 
unapompenda mtu unakuwa umempa uwezo wa kukuumiza...haijlishi ni mpenzi ama mzazi wako.
cha msingi tafuta mwenye thamani ya wewe kuumia juu yake A.K.A everybody will hurt u, just find a person worth hurting over
 
kila kuumizwa kuna viwango vyake, ukiona hujaumia kabisa hata kidogo ujue basi ulishapoteza sifa ya kibinadamu,

Tunachojitahidi kufanya ni kupunguza kiwango cha maumivu ya mapenzi kutoka maumivu ya miezi au miaka kadhaa na kuwa maumivu ya dakika kadhaa au masaa ama siku kadhaa tu.
Hakika! Kuumia katika mapenzi ni sawa na ajali kazini. Maisha lazima yaendelee
 
Hakika! Kuumia katika mapenzi ni sawa na ajali kazini. Maisha lazima yaendelee
kabisa best yangu, na kupenda lazima kuwepo tu hadi mwisho wa dahari ila jambo la msingi ni kupenda kwa akili.
 
kabisa best yangu, na kupenda lazima kuwepo tu hadi mwisho wa dahari ila jambo la msingi ni kupenda kwa akili.
Kuna wakati huwezi kupenda kwa akili maana mapenzi ni upofu, unajikuta ushazama penzini pasipo kujali yawezayo kujitokeza mbele ya safari.
 
Kuna wakati huwezi kupenda kwa akili maana mapenzi ni upofu, unajikuta ushazama penzini pasipo kujali yawezayo kujitokeza mbele ya safari.
Duuh unapenda mzima mzima! hongera sana kwa wanawake au wanaume wa aina hiyo
 
Kuna wakati huwezi kupenda kwa akili maana mapenzi ni upofu, unajikuta ushazama penzini pasipo kujali yawezayo kujitokeza mbele ya safari.
Ni lazima Safari ianze ndipo ujue unakoelekea kuna umbali gani
 
tatizo la kuumizwa kila mtu wa jinsia tofauti unamuona mbaya,hapo ndio utasikia mtu anakuambia "wanaume wote ni mbwa" huwa nacheka sana
 
Back
Top Bottom