Napitia wakati mgumu sana naombeni ushauri na msaada kwa kadri utakavyolipokea linalonisibu

Nichukue nafasi hii kuwashukuru nyote katika changamoto yangu ngumu sana nayopitia.

Wako baadhi wamenifata inbox na kunisaidia kwa chochote kile walichonacho nawashukuru sana.

Wako pia ambao wamenitia moyo na kunishauri mawazo mazuri nao pia nawashukuru.

Naami wako ambao hata kama hatukuwasiliana nao lkn baada ya kuliona hili huko waliko kwa namna moja ama nyingine wakaguswa na kuniombea kheri nao pia nawashukuru sana.

Wako ambao tumebahatika kuonana nao ana kwa ana na kufahamiana pia nawashukuru.

Kwa pamoja Mungu awabariki sana.

Sikuwa na pesa ya kumpeleka hata mke wangu hospital lakin kupitia walionichangia siku ya jana nilimpeleka na alipata vipimo na matibabu na sasa anaendelea vzr, kwa hilo nawashukuruni sana.

Ingawa bado naendelea kupambana na mengine ya kutoka kwenda kutafuta vibarua ili sasa kupata chochote kwaajili ya familia kula, huku afya ya mke wangu ikiwa inaendelea vzr, naamin haya yote kwa uweza wa Mungu ntayavuka.

Wako watu wamekuwa wakinishauri kuweka no ya Simu hapa hapa kwa yeyote mwenye ushauri, kibarua huko aliko au hata chochote anachowiwa kusaidia ili iwe rahisi. Nimeona ni wazo zuri na mm naiweka hapa hiyo no ambayo tunaweza kuwasiliana. Ambayo ni: 0742843490. Inapatikana na tutawasiliana moja kwa moja.
...good.

...amani ya Mungu idumu kwako,idumu na kwa wengine/kwetu pia.
 
Niko Mbezi hapa Dar nimepanga chumba kimoja nina mke na mtoto mmoja mchanga. Ingawa haukuwa wakati sahihi wa kuishi na mke ila kwakuwa ilitokea akabeba ujauzito na hakuwa na namna nyingine ya kuishi ikabidi tu niishi nae.

Nilikuwa nafanya kazi mahali kwa mtu ambapo nilikuwa nikilipwa kwa mwez ingawa malipo yalikuwa kiduchu sana. Wakati huo mke baada ya kubeba ujauzito alipokuja tuishi wote akawa anajishughulisha na kazi ndogo ndogo za kutembeza mboga za majani.

Baadae nilipokuwa nafanya kazi kulingana na hali ya biashara kuwa mbaya tulipunguzwa baadhi ya wafanyakazi wa pale na mimi nikiwa miongoni mwao. Na ni tangu mwezi wa 1 mwanzon mwaka huu.

Tangu hapo maisha yakaanza kuwa magumu ikanibidi sasa niwe natoka asubuhi nyumbani kwenda huko kutafuta vibarua vya kufanya. Maisha yameendelea hivo hivo kwa kupata na kukosa maana c kila siku utafanikiwa kupata kibarua.

Sasa hivi navyoandika hapa mke wangu anaumwa na mtoto tuliye nae ni mchanga sana na mimi hii inaenda kuisha wiki kila nikitoka sipati kibarua.

Nawaza sana sijui chakufanya ingawa wapo wanaonishauri kuitelekeza familia yangu lkn ni kitu ambacho sifikirii hata kidogo na siwezi kukifanya maana nampenda sana mke wangu na mtoto wetu.

Naombeni ushauri wenu na msaada wenu nifanye nini katika huu wakati mgumu nilionao. Ambao mm naamini ni kipindi kigumu sana nachopitia.

Niko tayari kufanya kazi yoyote ile ilimradi tu iwe halali hata iwe ni kibarua kwa siku kama kuna mahali kunahitajika kibarua mm niko tayari ili tu nihudumie familia yangu.

Sijasoma sana Elimu yangu ni kidato cha nne fairule nina miaka 27.
Wahi kiwanda cha pepsi pale Nyerere Rd...kila asubuhi na jioni wana vibarua wanapanga foleni kuingia na kupiga mzigo...

Ingia toka na elfu 15 yako.
 
mkuu sorry kwa mfano ukiwa na hivyo vitoroli ukiwapa watu wafanyie kazi wanalipa kiasi gani kqa siku kila kimoja?
Jiulize wanavipata wapi, sio kila mtu ni cha kwake. Vile vitoroli kuna watu wanavinunua kwa wingi (matajiri) kisha vijana wanakuja kuchukua kwa makubaliano ya hesabu ya siku. Jiongeze mzee.

Mie niliwahi kuwa na mikokoteni zaidi ya mitano wakati ndio naanza kazi benki moja hivi nikawa nakubaliana na vijana wanabebea mizigo soko la Tandale na faida yake ndio nilinunulia kiwanja ambapo ndio makazi yangu kwa sasa

Nimekwambia yote hayo ili ujue kuwa fursa zinatafutwa na zipo ni akili yako tu
 
Back
Top Bottom