Kwanza salamu, pia niwatakie heri ya Christmas na mwaka mpya.
Hoja ya msingi ni MALIPO YA LEMA YANAONYESHA UDHAIFU WA MFUMO WETU.
Lema atalipwa milion 85 Tsh/= kama malimbikizo kwa kusimamishwa baada ya kusimamishwa ubunge,
( kwa mchanganuo zaidi soma hapa Lema kuzoa Sh85 Milioni - Siasa - mwananchi.co.tz )
kama mwananchi nina tatizo na Lema kulipwa hiyo pesa, sioni Value for money kwa sisi kuwa na mfumo dhaifu kiasi hicho.
Tatizo nililonalo Lema kulipwa hiyo pesa ni maeneo yafuatayo:
1.) Milion 20 za mafuta kama Mbunge, Lema aliposimamishwa ubunge shughuli zake zilikoma, hivyo matumizi ya mafuta kwa shughuli za kibunge yalikoma pia!!! kwangu mimi kumlipa Mbunge Milion 20 za mafuta bila kuwa kazini au kufanya kazi ni kudhurumu wananchi, huu ni mfumo onevu, hiyo pesa haipashwi kulipwa,
kwa maelezo zaidi ni kwamba Lema atarudishiwa ghalama za kesi, ni ghalama zipi hizo? hakuna nauli alizokuwa anatumia? na kama ndio balance ipo itakuwaje tukimlipa tena kama umma pesa ya mafuta?
lakini Je Lema kwa wakati huo alikuwa anafanya shughuli zipi? sio M4C ( i embrace M4C but TAIFA kwanza) huko akulipwa chochote?
2.) posho ya jimbo Sh40 milioni ....... jimbo lipi hali kazi ilisimamishwa? jimbo la Arusha alikuwa na mbunge kwa wakati wote wa kesi? lema akufanya shughuli za kibunge jimboni mwake.
Lakini pia kwa kwenda mbali ni kwamba Lema alikuwa na shughuli maalumu ya chama yaani M4C ( no problems) lakini je hapa kuna tofauti gani na wale wafanyakazi hewa? mtu ayupo kwenye kituo cha kazi analipwa tu? hivi sisi tunalipa majina au shughuli/kazi ya mtu? where is the value for my TAX?
3.) Posho nyingine Sh6.6 milioni Kwa kazi ipi analipwa posho? ubunge ulikoma nimeshaeleza hapo juu, ofisi ya mbunge haikuwa na kazi tena kwa kukosa mbunge, na kama ilikuwepo na ina fanya kazi vipi amri ya mahakama kusimamisha ubunge wa Lema, kwa misingi hiyo nina amini hakukuwa na shughuli ya sisi kama taifa kulipa posho.
<<<<<<
Nakubaliana kwamba Lema alipwe malimbikizo ya mshahara wake yanafikia Sh18.4 milion, hii ni haki pekee kwa Lema, sikupaliana kwamba kama mtu umesimamishwa wazifa wako basi umma uendelee kukulipa pesa bila kuutumikia.
CHOMBEZO
HITIMISHO:
Hoja yangu ni tuwe na kanuni zenye macho, zinazothamini kodi yetu, malipo lazima yenye thamani ya kazi, malipo holela ni hatari kwa taifa, napinda haya malipo regardless nani anapewa, msingi ni kuwa na taifa imala lenye uchumi unaonufaisha wote.
Kama kuna sheria zinatoa mwanya huu zifutwe mara moja ili kuongeza thamani ya pesa yetu katika matumizi (VALUE FOR MONEY)
Binafsi naguswa na huu moyo wa kuumizwa na matumizi yasiyo stahiki ya kodi za wananchi. Hata hivyo ni vema ikakumbukwa kuwa tunachoongelea hapa ni
1.Lema alikuwa mbunge halali kwa KUCHAGULIWA na KWA RIDHAA YA WANANCHI WA JIMBO LAKE. Kwa hiyo kitendo kilichofanywa cha kuitoa mahakama nje ya utaratibu na kulazimisha hukumu, kilimnyang'anya haki yake ya kisheria ya kuwawakilisha wananchi kupitia KODI hizo na mengineyo.
2.Matakwa ya sheria yanakubaliana na uhalali wa ubunge wa Lema ndiyo maana baada ya kureview hukumu wameona bado ana haki hiyo.
Kwa hiyo:
Kwa kuwa Lema alichaguliwa kwa kura halali kuwa Mbunge, na kwa kuwa uamuzi wa kumsimamisha haukuwa wa haki, na kwa kuwa hukumu ya rufaa imemrudisha tena Kuwa mbunge, Hii nisawa na kusema: kwa mujibu wa sheria Lema alikuwa MBUNGE HALALI TANGU KUCHAGULIWA MPAKA SASA NA MPAKA WANANCHI WATAKAPOAMUA VINGINEVYO.
Kutokana na hilo Lema anastahili kila posho aliyotakiwa kupata akiwa mbunge HALALI kwa sababu hakuomba kusimamaishwa wala hakuwa na Matatizo ya kiutendaji. Kama kuna lawama za matumizi mabaya ya Kodi yanaweza kuelekezwa kunakostahili uchunguzi ufanywe, ipatikane SABABU ya kusimamishwa Lema at first place. Huyo aliyepika hilo ndo ALAUMIWE KWA UFUJAJI WA KODI ZA WANANCHI. Vinginevyo Lema, Kwa mujibu wa taratibu anatakiwa ALIPWE STAHILI YAKE KWANZA halafu, kama itaonekana sheria zinahalalisha ufujaji wa KODI kwa maana hiyo, ZIFANYIWE MAREKEBISHO ili kesho lisirudie hilo.
Kwa upande wa pili ikumbukwe kuwa Lema kama Binadamu, Mtanzania, Mwanamageuzi na Mzalendo, ana maoni na utashi wake. Hivyo badala ya kuanzisha mijadala kama hii tumpe nafasi ya kuamua anataka nini. Naamini atakuja na uamuzi wa busara kama ambavyo amekuwa anafanya. Nina imani kuwa Matumizi ya pesa hizo (KAMA ATALIPWA) yatakuwa kwa manufaa ya wanachi bado na HAITAKUWA HASARA KWA VYOVYOTE KUCHUKUA FEDHA KWENYE MFUKO WAKO WA KUSHOTO KWENDA WA KULIA........
Hivi Ndivyo nionavyo mimi:smiling: