Mapolomoko
JF-Expert Member
- Feb 16, 2013
- 1,751
- 422
Nisaidieni jamani mateso bado yanaendelea
Hapo owa mke wa pili unaondoka kwenda kwa B mdogo bila kuaga, atanyooka kama lula
Nisaidieni jamani mateso bado yanaendelea
na kwa hiyo avatar uliyoweka, ningekuwa jirani ningekuongeza makofi mawili!
Nisaidieni jamani mateso bado yanaendelea
ukiona maisha yanaziiiidi kuwa magumu...achaana nayo,tafuta shughuli ingine ya kufanya mangiiii!!!ndoa naiona chungu na sijui la kufanya.
Mke wangu ananichukulia kama mtoto, aninaamrisha, ananitumikisha na pia huwa ananipiga.
Nimejaribu kupambana naye lakini nimejikuta nikiambulia maumivu na majeraha.
Sina pa kwenda kwani naishi naye kwenye tuliyoijenga wote.
Amekuwa na tabia ya kunikataza kuongea na baadhi ya marafiki zangu, na pia simu yangu amekuwa akinipora na kuangalia watu ninaowasiliana nao.
Nimezaa naye watoto wawili.
Mkubwa ana umri wa miaka tisa na mdogo wake ana umri wa miaka mitano.
Kibaya zaidi mtoto wetu mkubwa amekuwa akiwasilimulia wenzake jinsi ninavyokula kipondo.
Majirani wote wanajua taabu ninayoipata kutoka kwa mwanamke huyu wa kinyiha.
Unyumba ni hadi atake mwenyewe na nikimaliza kabla yake napigwa sana halafu naambiwa tuendelee na tendo la ndoa ambalo kwangu naona adhabu.
Nifanyeje kujinusuru na mateso haya?
...Samahani mtoa mada....imebidi nicheke kwanza aiseee....is this true mkuu? au ni fiction story?
pale aliposema ananyimwa kuongea na rafiki zake, ndipo paliponiaminisha kuwa huu uzi ni real. Hii imekuwa ni tabia ya baadhi ya wanawake. Na hii trick huwa wanafundishwa na mama zao kwani inapofanikiwa inammaliza kabisa mwanaume.
Endapo akitii amri hii haramu ya kutokuongea na rafiki zake, atahamia kwa ndugu na hapo utakuwa mwisho wa kila kitu!