Napendekeza CCM ifutwe

Lukolo

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
5,143
3,196
Ndugu zangu,
Usiku wa leo nimekosa kabisa usingizi kwa kuufikiri mstakabali wa nchi yangu chini ya chama filisi cha CCM. Msongo huu wa mawazo ulinifikisha mahali pa kujiridhisha kwamba chama hiki yafaa kifutwe nchini. Nina sababu moja au mbili kuu za kuwaza hivyo kama ifutavyo:

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilisajiriwa kama ni chama cha wakulima na wafanyakazi na katika bendera ya CCM kuna alama za jembe na nyundo kama uwakilishi wa wakulima na wafanyakazi. Lakini hivi sasa CCM imekiuka mkataba wake wa usajili kwa kuwatosa wakulima na wafanyakazi na kuamua kuwa chama cha kifamilia, cha wafanyabiashara, matajiri wakubwa, mafisadi, majangiri, wahujumu uchumi na majambazi. Wapo watakaoubishia mtazamo huu. Lakini napenda kuwapa vielelezo vifuatavyo:
  • Muundo wa chama: Ni nani walioshika nafasi za juu za chama, nani ni wachangiaji wakubwa wa chama, ni kwa kiasi gani familia ya Kikwete na Makamba imeweka mizizi ndani ya chama? Baba mwenyekiti, mama mjumbe wa kamati kuu, mtoto mjumbe wa halmashauri kuu ya UVCC, mtoto ni mwenyekiti wa vijana chipukizi: Baba ni katibu mkuu wa chama, mtoto mshauri wa raisi na mgombea ubunge: Baba rais mstaafu, mtoto waziri. Hii ni mifano michache tu wapo wengi ndani ya CCM ambao utasikia historia zao zinaanzia kwa wazazi wao.

  • Uendeshaji wa chama: Ni akina nani wenye sauti ya mwisho ndani ya CCM? Naamini hakuna atakayenibishia juu ya hili. Wahindi na wafanyabiashara wakubwa ndio wanaoiongoza CCM na nchi kwa ujumla. Hao ndo wanaopanga nani awe nani na wapi? Hao ndo ambao Rais alisema wakikamatwa kwa wizi wa fedha za EPA, na kupelekwa mahakamani nchi itayumba. Hao ndo mabosi na waajiri wa Kikwete na CCM kwa ujumla wake. Si wakulima na wafanyakazi tena. Kwa kuwa wakulima na wafanyakazi hawana tena nafasi ya kuhoji wala kudai haki yao kutoka katika chama kinachojiita ni cha kwao.

  • Nafasi za uongozi: Ukifuatilia kwa umakini utagundua kwamba uongozi katika nafasi ya ubunge na udiwani, kwa kiasi kikubwa zimechukuliwa na watu maarufu, wenye pesa za kutosha kununua kura, huku wakulima na wafanyakazi wa kawaida wa serikali wenye kipato cha kawaida na wasio na uwezo wa kununua kura wakiambulia patupu. Sehemu kubwa ya wagombea kupitia CCM ni matajiri waliojijenga kiuchumi na wafanyabiashara wakubwa, wakulima na wafanyakazi hawana chao.

  • Mwenyekiti wa CCM aliwakataa wafanyakazi kweupe alipowahutubia wazee wa Dar es salaam. Kwanza nauona huu kama ulimbukeni: wanaodai maslahi bora ni wafanyakazi, lakini wanaohutubiwa ni wazee wastaafu, kuna uhusiano gani hapo? Lakini kikubwa ni kwamba huyu mwenyekiti alisema wazi kwamba serikali yake haina uwezo wa kuboresha maslahi ya wafanyakazi (ambao kiujumla ndio wanaochangia kuinua hali ya kilimo kutokana na kugawana kipato chao na wa kwao huko vijijini ambao ni wakulima). Wakati akikataa kuwatekelezea wafanyakazi mahitaji yao, alikuwa anajua kabisa kwamba ana msululu wa makampuni ambayo ameyasamehe kodi kwa miaka kadhaa ili yachume ambapo hayakupanda. Alikuwa anajua kabisa kwamba kuna meli ya Kinana inabeba magogo na pembe za ndovu kijangiri, alikuwa anajua kabisa kwamba kuna Rostam aziz ambaye amekalia mabilioni ya watz. Kwa hiyo aliwakataa wafanyakazi akawalinda wafanyabiashara, wageni, mafisadi, majangiri na majambazi wa uchumi wetu.

  • Naamini pia kwamba CCM si chama cha wakulima na wafanyakazi kwa kuwa serikali ya CCM ndiyo ilishiriki katika kuviua viwanda vyote vilivyokuwa vinasindika mazao yetu ya kilmo, ndiyo iliyoua kiwanda cha mbolea, ndiyo hiyo iliyoingia mikataba mibovu ya kuimaliza nchi. Wakati CCM ikiingia mikataba ya TANGOLD, Meremeta, Deep Green, IPTL, RICHMOND na mingineyo ya hivyo, iliwashirikishaje wakulima na wafanyakazi? Wakati CCM inaidhinisha wizi wa mabilioni ya fedha EPA kuyapeleka kwa wafanyabiashara wakubwa nchini ilikumbuka kwamba kuna zaidi ya asilimia 60 ya watanzania wasiokuwa na ajira wala mitaji? Na iliwashirikishaje hawa wote ambao ndio wanachama wa CCM?
Kwa kuwa chama hiki kimekiuka mkataba wa uandikishaji wake ambao unaonyesha kwamba ni chama cha wakulima na wafanyakazi, na kikajikita katika kulinda na kusimamia maslahi ya wafanyabiashara, wanafamilia, mafisadi, matajiri na majambazi. Napendekeza kifutwe, na kuanzisha chama halali cha wakulima na wafanyakazi, na hao wafanyabiashara, mafisadi, matajiri na wengine wanaofanana nao waanzishe chama chao kingine.
 
Tendwa na Lweis Mkame watakula wapiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
Ni sawa na kmfukuza kazi bosi wako unaitaji moyo wa chuma kufanya hayo
 
Kwa scale yeyote ile, CCM ilitakiwa si tu ifutwe, bali viongozi wake wote wapelekwe jela na kufunguliwa kesi za uhaini. Yaani ilitakiwa kuwepo na man to man crackdown ya watu wote waliowahi kuwa associated na CCM, kuanzia viongozi wakuu, wafanyibiashara na makumpuni makubwa (mengi). Pande hizi zote zinahusika moja kwa moja na kuwahujumu watz.

CCM inatakiwa ifutwe kwa sababu imedhihirisha wazi kwamba ni CRIMINAL ORGANISATION. Ndio maana watu wanakwiba hela halafu rais mzima (apparently ambaye ndio alitakiwa awe kamanda wa kwanza wa kuilinda katiba) anasema ati the culprits wanapewa muda warejeshe hizo hela walizokwiba! Sasa huezi ukahitaji kuwa sceintist wa NASA kuona who CCM is made of.
 
Duu! Lukolo umemaliza yote Maneno ni makali yenye kutia uchungu! tumepoteza hope ya maisha yetu na familia zetu ktk utawala huu usio na haya wala huruma, tunateswa na wachache wenye power na pesa, hatuna pa kukimbilia the justice system is highly corrupted, polisi wanatutesa, Wanajeshi wanatutesa na kutuua, shule zetu za kata kwa watoto wetu hazina walimu wala resources zakutosha, we have been neglected katika ardhi yetu wenyewe na CCM bado inatuburuza katika mateso ya kusaga meno Mungu ailaani na Mungu Ibariki Tanzania:mad2:
 
Ndugu zangu,
Usiku wa leo nimekosa kabisa usingizi kwa kuufikiri mstakabali wa nchi yangu chini ya chama filisi cha CCM. Msongo huu wa mawazo ulinifikisha mahali pa kujiridhisha kwamba chama hiki yafaa kifutwe nchini. Nina sababu moja au mbili kuu za kuwaza hivyo kama ifutavyo:

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilisajiriwa kama ni chama cha wakulima na wafanyakazi na katika bendera ya CCM kuna alama za jembe na nyundo kama uwakilishi wa wakulima na wafanyakazi. Lakini hivi sasa CCM imekiuka mkataba wake wa usajili kwa kuwatosa wakulima na wafanyakazi na kuamua kuwa chama cha kifamilia, cha wafanyabiashara, matajiri wakubwa, mafisadi, majangiri, wahujumu uchumi na majambazi. Wapo watakaoubishia mtazamo huu. Lakini napenda kuwapa vielelezo vifuatavyo:

  • Muundo wa chama: Ni nani walioshika nafasi za juu za chama, nani ni wachangiaji wakubwa wa chama, ni kwa kiasi gani familia ya Kikwete na Makamba imeweka mizizi ndani ya chama? Baba mwenyekiti, mama mjumbe wa kamati kuu, mtoto mjumbe wa halmashauri kuu ya UVCC, mtoto ni mwenyekiti wa vijana chipukizi: Baba ni katibu mkuu wa chama, mtoto mshauri wa raisi na mgombea ubunge: Baba rais mstaafu, mtoto waziri. Hii ni mifano michache tu wapo wengi ndani ya CCM ambao utasikia historia zao zinaanzia kwa wazazi wao.

  • Uendeshaji wa chama: Ni akina nani wenye sauti ya mwisho ndani ya CCM? Naamini hakuna atakayenibishia juu ya hili. Wahindi na wafanyabiashara wakubwa ndio wanaoiongoza CCM na nchi kwa ujumla. Hao ndo wanaopanga nani awe nani na wapi? Hao ndo ambao Rais alisema wakikamatwa kwa wizi wa fedha za EPA, na kupelekwa mahakamani nchi itayumba. Hao ndo mabosi na waajiri wa Kikwete na CCM kwa ujumla wake. Si wakulima na wafanyakazi tena. Kwa kuwa wakulima na wafanyakazi hawana tena nafasi ya kuhoji wala kudai haki yao kutoka katika chama kinachojiita ni cha kwao.

  • Nafasi za uongozi: Ukifuatilia kwa umakini utagundua kwamba uongozi katika nafasi ya ubunge na udiwani, kwa kiasi kikubwa zimechukuliwa na watu maarufu, wenye pesa za kutosha kununua kura, huku wakulima na wafanyakazi wa kawaida wa serikali wenye kipato cha kawaida na wasio na uwezo wa kununua kura wakiambulia patupu. Sehemu kubwa ya wagombea kupitia CCM ni matajiri waliojijenga kiuchumi na wafanyabiashara wakubwa, wakulima na wafanyakazi hawana chao.

  • Mwenyekiti wa CCM aliwakataa wafanyakazi kweupe alipowahutubia wazee wa Dar es salaam. Kwanza nauona huu kama ulimbukeni: wanaodai maslahi bora ni wafanyakazi, lakini wanaohutubiwa ni wazee wastaafu, kuna uhusiano gani hapo? Lakini kikubwa ni kwamba huyu mwenyekiti alisema wazi kwamba serikali yake haina uwezo wa kuboresha maslahi ya wafanyakazi (ambao kiujumla ndio wanaochangia kuinua hali ya kilimo kutokana na kugawana kipato chao na wa kwao huko vijijini ambao ni wakulima). Wakati akikataa kuwatekelezea wafanyakazi mahitaji yao, alikuwa anajua kabisa kwamba ana msululu wa makampuni ambayo ameyasamehe kodi kwa miaka kadhaa ili yachume ambapo hayakupanda. Alikuwa anajua kabisa kwamba kuna meli ya Kinana inabeba magogo na pembe za ndovu kijangiri, alikuwa anajua kabisa kwamba kuna Rostam aziz ambaye amekalia mabilioni ya watz. Kwa hiyo aliwakataa wafanyakazi akawalinda wafanyabiashara, wageni, mafisadi, majangiri na majambazi wa uchumi wetu.

  • Naamini pia kwamba CCM si chama cha wakulima na wafanyakazi kwa kuwa serikali ya CCM ndiyo ilishiriki katika kuviua viwanda vyote vilivyokuwa vinasindika mazao yetu ya kilmo, ndiyo iliyoua kiwanda cha mbolea, ndiyo hiyo iliyoingia mikataba mibovu ya kuimaliza nchi. Wakati CCM ikiingia mikataba ya TANGOLD, Meremeta, Deep Green, IPTL, RICHMOND na mingineyo ya hivyo, iliwashirikishaje wakulima na wafanyakazi? Wakati CCM inaidhinisha wizi wa mabilioni ya fedha EPA kuyapeleka kwa wafanyabiashara wakubwa nchini ilikumbuka kwamba kuna zaidi ya asilimia 60 ya watanzania wasiokuwa na ajira wala mitaji? Na iliwashirikishaje hawa wote ambao ndio wanachama wa CCM?

Kwa kuwa chama hiki kimekiuka mkataba wa uandikishaji wake ambao unaonyesha kwamba ni chama cha wakulima na wafanyakazi, na kikajikita katika kulinda na kusimamia maslahi ya wafanyabiashara, wanafamilia, mafisadi, matajiri na majambazi. Napendekeza kifutwe, na kuanzisha chama halali cha wakulima na wafanyakazi, na hao wafanyabiashara, mafisadi, matajiri na wengine wanaofanana nao waanzishe chama chao kingine.
Mkuu Lukolo umenistua sana na hii post
sikufikiri hata siku moja kama kuna jasiri atakuja kuyasema haya hadharani. Nimepitia post yako nimeona upo sahihi naunga mkono hoja ila nina machache hapa.
Kwa kuwa CCM imegeuka na kukengeuka huku ikikumbatiwa na vyombo vya dola vilivyoapa kufa na mafisadi, inatubidi sisi wakulima na wafanyakazi tuchakatue BONGO zetu how to erase this dubwasha.
Pia ieleweke kwamba wanasiasa wanatumia matatizo ya wanachi kama mtaji wa kisiasa, hivyo katikati yetu wapo wasaliti kadhaa ambao inabidi tukae chonjo kuuzwa kwa vijisenti vichache (walishawahi kutuuza enzi za kugombea uhuru).

Tuuvue uoga wetu na kujivika ujasiri kwa ajili ya vizazi vijavyo kwani bila hivyo sisi tutakuwa manamba wa enzi tu.

Kikubwa ni kupiga kura nyingi kwa wagombea nje ya ccm kuanzia urais mpaka udiwani.

Mwaka huu tuseme YES WE CAN kwa vitendo
 
Uchaguzi mkuu ndio wakati ya kukiacha njia panda chama kinachozingua - lakini iwapo tu wapiga kura walio wengi wataelewa tatizo lililopo.
 
Kwa scale yeyote ile, CCM ilitakiwa si tu ifutwe, bali viongozi wake wote wapelekwe jela na kufunguliwa kesi za uhaini. Yaani ilitakiwa kuwepo na man to man crackdown ya watu wote waliowahi kuwa associated na CCM, kuanzia viongozi wakuu, wafanyibiashara na makumpuni makubwa (mengi). Pande hizi zote zinahusika moja kwa moja na kuwahujumu watz.

CCM inatakiwa ifutwe kwa sababu imedhihirisha wazi kwamba ni CRIMINAL ORGANISATION. Ndio maana watu wanakwiba hela halafu rais mzima (apparently ambaye ndio alitakiwa awe kamanda wa kwanza wa kuilinda katiba) anasema ati the culprits wanapewa muda warejeshe hizo hela walizokwiba! Sasa huezi ukahitaji kuwa sceintist wa NASA kuona who CCM is made of.

mheshimiwa upo serious kweli? maana sijakuelewa, mbona na hata wengi katika upinzani walitokea CCM (walikuwa "associated") including Dr. Slaa ambaye baada ya kuenguliwa kwenye kura za maoni akahamia CHADEMA na wengine wengi au unamaanisha nini?
chama hakiwezi kuwa na matatizo, wenye matatizo ni some individuals - hivyo lazima tuwe focused
 
Uchaguzi mkuu ndio wakati ya kukiacha njia panda chama kinachozingua - lakini iwapo tu wapiga kura walio wengi wataelewa tatizo lililopo.
Mi nadhani hata beyond uchaguzi, watz wote, kila mmoja kwa nafasi yake, ahakikishe siasa haiharibu nchi. Tumechoshwa kushikiwa na kufilisiwa nchi yetu na maharamia wanaotumia siasa kama smoke-screen ktk kutafuta uhalali wa kutupora na kutubaka na kuchukua utu wetu. Ukombozi wa mara ya kwanza wa nchi yetu ulikuwa dhidi ya mgeni mwenye ngozi nyeupe, ukombozi wa mara ya pili wa nchi yetu ni kutoka mikononi mwa mabeberu wa ndani, ambao ni wabaya zaidi maana wanatoka miongoni mwetu na himaya yao ina umri wa mtu mzima sasa. Shime watz, tuamke na tuweke fikra zetu nje ya siasa, tuwekeze kuwaondoa wote wanaotumilia nchi hii kwa manufaa binafsi.
 
mheshimiwa upo serious kweli? maana sijakuelewa, mbona na hata wengi katika upinzani walitokea CCM (walikuwa "associated") including Dr. Slaa ambaye baada ya kuenguliwa kwenye kura za maoni akahamia CHADEMA na wengine wengi au unamaanisha nini?
chama hakiwezi kuwa na matatizo, wenye matatizo ni some individuals - hivyo lazima tuwe focused

Nipo very serious.
 
Asante Lukolo kwa hoja ulizozichambua kwa umakini mkubwa. Huo ndio ukweli kuhusu CCM, chama ambacho miaka ya 70 kilianzishwa kikidhamiria kuleta mapinduzi kwa mtanzania.

Inasikitisha, ila hakuna njia. Tukitaka kupata mapinduzi yaliyodhamiriwa na Waasisi wa chama hicho, inatubidi kuisahau kwanza. Tufanye maamuzi 31.10 kupitia kura zetu.

Naungana na Abdulhalim pia kuwa baada ya CCM kupunziswa viongozi wake na mafisadi wote wapelekwe mbele ya sheria pamoja na marafiki zao wahindi wahujumu uchumi.
 
Mkuu hupo sahihi lakini huyo CCM anamiliki serikali wakiwemo wakuu wa mikoa na wilaya,anamiliki jeshi,anamiliki polisi,anamiliki mahakama,anamiliki usalama wa Taifa, anamiliki TRA, anamiliki TBC,Daily news,vigogo hao wanamiliki njia karibu zote za uchumi.Kazi ya kuwayanganya viranja wa chama tonge mdomoni ni ngumu lakini inawezekana.
 
You are right sblades! kazi ya kuwang'oa hawa CCM ni ngumu sana, But lets not be too pessimistic, i'm sure together we can do it!
 
Mi nadhani hata beyond uchaguzi, watz wote, kila mmoja kwa nafasi yake, ahakikishe siasa haiharibu nchi. Tumechoshwa kushikiwa na kufilisiwa nchi yetu na maharamia wanaotumia siasa kama smoke-screen ktk kutafuta uhalali wa kutupora na kutubaka na kuchukua utu wetu. Ukombozi wa mara ya kwanza wa nchi yetu ulikuwa dhidi ya mgeni mwenye ngozi nyeupe, ukombozi wa mara ya pili wa nchi yetu ni kutoka mikononi mwa mabeberu wa ndani, ambao ni wabaya zaidi maana wanatoka miongoni mwetu na himaya yao ina umri wa mtu mzima sasa. Shime watz, tuamke na tuweke fikra zetu nje ya siasa, tuwekeze kuwaondoa wote wanaotumilia nchi hii kwa manufaa binafsi.
Pole sana Abdulhalim, maandishi yako yanadhihirisha kwamba una uchungu mkubwa na ubadhirifu uliopo nchini. Kiukweli inauma sana pale unapotambua kwamba thamani ya mtanzania mzalendo ni second priority kuliko thamani ya wageni, mafisadi na wanyonyaji wa uchumi wa nchi yetu.

You can just imagine kwamba wakati Mwakalebela anatoswa ubunge kwa kutoa rushwa ya pengine laki moja, Endrew Chenge anapitishwa na kamati kuu hata baada ya kudhihirika wazi kwamba alikula rushwa ya mabilioni ya fedha kutoka BAE system ili kuitia hasara Tanzania katika ununuzi wa Rada. Basil Mramba anapitishwa kugombea ubunge pamoja ya kwamba ndiye aliyekuwa waziri wa fedha wakati mabilioni ya shilingi yalipochotwa kutoka EPA, na tayari amefunguliwa kesi mahakamini. Hii haiingii akilini kabisa. Haya nayo ni ushahidi kwamba mtanzania mkulima ua mfanyakazi wa kawaida hana nafasi ndani ya CCM.

Ndugu zangu, tuna kazi kubwa mbele yetu, kazi hiyo ni kuirudisha nchi mikononi mwa watanzania wazalendo, kuikomboa nchi kutoka kwa mafisadi wachache wanaojinufaisha kwa kuwakandamiza masikini walio wengi. Tujipange, tuamue, tunaweza! Yes we can!!! Say no to CCM in 31st October.
 
sasa ikifutwa CCM.. hii nchi itakuwa Njia panda .. bado hakuna chama chenye uzoefu wa kuongoza tanzania yetu
 
sasa ikifutwa CCM.. hii nchi itakuwa Njia panda .. bado hakuna chama chenye uzoefu wa kuongoza tanzania yetu

Hivi TANU ilipopokea nchi kutoka kwa wakoloni ilikuwa na uzoefu gani wa kuongoza? Tuweni na moyo wa ujasiri watanzania. Tuache kuaminishwa kwamba CCM ndo chama pekee kinachoweza kuongoza nchi ilihali kinaendelea kutufilisi na kutuongezea machungu ya maisha. Tujipange, Tuamue, Tunaweza!!!! Aliyeijenga Rome ni wa Romani wenyewe. Walioijenga Paris ni waparisi (wafaransa) wenyewe, hakutoka mtu wa nje kwenda kuwasaidia kujenga. Vivyohivyo ni sisi wenyewe watanzania tutakayeweza kuikomboa nchi yetu na kuleta mgawanyo sawa wa raslimali zetu nchini. Yes we can! Tuamue!!
 
Lukolo ulipaswa kuungana na Mwenye kiti wa kampeni wa CHADEMA. CCM wamekuwa wakiponda vyama vya upinzani kuwa ni vya kikabila, vya kidini na vya kikanda. LAKINI CCM sasa kimekuwa chama cha KIFAMILIA na KIRAFIKI. Naamini wale wote wasio wanafiki ndani ya chama wanaumia sana kuona FAMILIA Inapigania kuingia ikulu badala ya kutumia jitiada ya chama.
 
Lukolo ulipaswa kuungana na Mwenye kiti wa kampeni wa CHADEMA. CCM wamekuwa wakiponda vyama vya upinzani kuwa ni vya kikabila, vya kidini na vya kikanda. LAKINI CCM sasa kimekuwa chama cha KIFAMILIA na KIRAFIKI. Naamini wale wote wasio wanafiki ndani ya chama wanaumia sana kuona FAMILIA Inapigania kuingia ikulu badala ya kutumia jitiada ya chama.

Mkuu nashukuru sana kwa ushauri huo. Nitajaribu kuwasiliana na Dr Slaa kuona kama ataniruhusu nishirikiane naye katika kampeni.
 
Mkuu Lukolo yote uliyosema ni ya kweli CCM imepoteza welekeo CCM ya leo si ile ya Nyerere tuliyoijua, kuna watu walifurahia kuondoka kwa Nyerere waliona sasa wamepata nafasi ya kuchuma nafikiri hata Kikwete alifurahia kuondoka kwake ingawa najua wengi hamtakubaliana nami. CCM ya leo ni ya kifamilia zaidi.
 
sasa ikifutwa CCM.. hii nchi itakuwa Njia panda .. bado hakuna chama chenye uzoefu wa kuongoza tanzania yetu
Mhh..mmezoea nyonyo za bure eehh? nchi itakuwa njia panda au mafisadi na wapambe wao watakuwa njia panda? sema vizuri usikike dugu..
 
Lukolo,
Mkuu waneno mazito sana haya. Hata kama Chadema au Dr.Slaa hatakubali uungane ktk msafara wake basi atumie aya zako kwani zimegomga hali halisi ambayo kusema kweli Wadanganyika wengi wameshindwa kutazama CCM ilipotoka na leo ni chama gani?
 
Back
Top Bottom