Napenda Kufahamu Wana JF

Napenda Kufahamu Wana JF

Laa HawaLaa wala Quwata iLaa BiLLah... Kila nafsi yataonja mauti !!
ikiwa kweli basi yatakayomfaa na kumsaidia amali zake, na wala sii JF wala members !!
 
Gogle?? i never know so sad, lkn mbona kuna ID nyengine kama hyo bado ina post?? ni mutiple ID au kuna mtu anatumia account yake??
 
Last edited by a moderator:
Kwani tukijua flani amefariki tutafanyaje? Kumpa pole? Au kuandika r.i.p flani?
 
attiiiii! unasema Gogle amefariki huyu huyu wa jf au mwingine???? mbona umeshtua bestito jamani???
eheeee Mungu wangu!!!
Kuna uzi nimeuona wa kuwakumbuka waliofariki mle ndan ya uzi kuna post inasema kua Gogle amefariki pia kuna uzi ulitolewa wa kuhusu kifo chake kua alizikwa kisutu
Mwenye kujua atuambie maana wengine hatufahamu kama ni kweli inasikitisha sana namuomba utafiti pia na wengine mnaojua
Tutammiss sana Gogle
 
Last edited by a moderator:
attiiiii! unasema Gogle amefariki huyu huyu wa jf au mwingine???? mbona umeshtua bestito jamani???
eheeee Mungu wangu!!!

Shost na mie kuna sehemu nimeona ndio nikaona niulizie tu humu
 
Last edited by a moderator:
Aisee, Kama ni kweli Mungu amlaze pema peponi kijana mwenye umri wa miaka 25.
 
ID ya Gogle ilituletea thread humu na mtu alijitambulisha kua yeye sio Gogle tunayemjua ila ni mjomba wake na alituletea taarifa ya msiba wa Gogle. Mimi niliuliza umejuaje password yake? Nikajibiwa ukitumia application ya jf haina haja yakuingiza password kila unapoingia, kitu ambacho ni kweli ata mimi natumia app kwaio mtu akishika simu yngu anaweza kuingia jf kwa ID yngu

Mkuu utafiti huyo gogle anaeongelewa ni yule kijana mwenye avatar kama picha ya Orochi? (Kabeba mbuzi mgongoni?)
 
Last edited by a moderator:
Mkuu utafiti huyo gogle anaeongelewa ni yule kijana mwenye avatar kama picha ya Orochi? (Kabeba mbuzi mgongoni?)

Kama huyu mkuu
1402326109252.jpg
 
Aisee mbona nami kama siamini, nakumbuka kuna uzi wake mmoja tuliuchakachua sana,tulikuwa na kina Karucee, Munkari mwingine nimemsahau. Kama ni kweli apumzike panapostahili kwa amani.
 
Gogle alikuwa na mbwembwe zake ila kuna siku watu walimgalagaza vibaya humu. RIP Gogle.
 
atakuwa amekufa bado mdogo tuuu... miaka25... dah!
 
ID ya Gogle ilituletea thread humu na mtu alijitambulisha kua yeye sio Gogle tunayemjua ila ni mjomba wake na alituletea taarifa ya msiba wa Gogle. Mimi niliuliza umejuaje password yake? Nikajibiwa ukitumia application ya jf haina haja yakuingiza password kila unapoingia, kitu ambacho ni kweli ata mimi natumia app kwaio mtu akishika simu yngu anaweza kuingia jf kwa ID yngu

sasa alileta taarifa za msiba ili iweje!!! mtu ambae aliamua kutojulikana iweje akifa ndo tutangaziwe???
 
Last edited by a moderator:
Kuna member mmoja alipofariki nakumbuka hadi picha yake halisi tuliletewa (naomba nisijekufanyiwa mimi tafadhali)

vimbelembele tu vya watu. kama mtu kashakufa ukimfaham inasaidia nini! hao ndio wale kwenye ugonjwa hawatoi hata sh tano ila kwenye kifo mamilion yanawatoka kugharamia msiba.
 
Back
Top Bottom