Nape si mzima!!

Nape si mzima!!


nisingependa lakini nalazimika kukuita mjinga kwa sababu chache!
1.Wewe unawezaje kufananisha kadi ya chama na funguo za nyumba ya mapadre? ni wazi ujue kuwa nyumba ya mapadre ni mali ya kanisa na hata baadhi ya vifaa vya kuendeshea ibada ni mali ya kanisa sasa wewe ulitaka aondoke navyo kivipi? kumbukumbu za upadre wake anaweza kuwa nazo kama biblia,,vitabu mbalimbali na hata baadhi ya mavazi kama kanzua ambayo sio mali ya kanisa

2.Unasema kuwa Dr, amezoea uwongo na uzushi mwingi, fine hebu tuorodheshee uwongo wake? unakumbuka list of shame ya mwembe yanga? unakumbuka kashfa ya EPA unakumbuka meremeta na Deep green? wote huo uwongo na uzushi wa doctor??

3.Umefikia hata hatua ya kuingilia privacy na maisha ya mtu kibinafsi? unajua ni sababu zipi za msingi zilizoshabaisha doctor akaacha upadre? na kitu cha ajabu unasema kuwa kamuasi mungu? kuasi maana yake asingeendelea kuwa muumini badala yake angeanza kuwa mfuasi wa shetani na kufanya maovu, kuhusu familia sio jambo la ajabu watu kutengana! Nelson Mandela baba wa Africa alitengena na Winnie and still amekuwa ni rasi bora mno Africa,ungefuatilia ujue chanzo na slaa na rose kutengena sio unarusha lawama za jumla

3.Unamnukuu Mwadhama akisema wapinga ufisadi nao ni mafisadi hapa sijakuelewa kwamba basi wewe unatetea mafisadi Pengo nae aliwatetea? Siamini Pengo nayemfahamu kama kiongozi wangu wa kanisa angeweza kuongea utumbo huu wewe ndio umemlisha maneno!

4.Viongozi wengi wa CCM ambao wana kadi moja tu ya ccm mbona ndio hao sasa wanaongoza kwa kuuza nchi, rasilimali na kuhamisha mabilioni na kuyaficha nje!

Mwisho*CCM ni janga la kimataifa ni kansa inatafuna watanzania ni kirusi kinachosababisha ugonjwa wa umaskini na kunenepesha wagonjwa wa ufisadi, lazima tuiong'oe sasa na haraka
 
DR. SLAA NA KADI YA CCM, NA UNAFIKI WA WATETEZI *WAKE

Kwa muda sasa wa karibu wiki tatu au nne pamekuwa na mjadala mkubwa juu ya kumiliki kadi ya CCM kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA na padri aliye asi Dr. Wilbroad Slaa.Mjadala huu umeingiza watu wengi sana kwenye maeneo mbalimbali lakini ukigawa wajadiliji kwenye makundi matatu makubwa, kundi la kwanza la wanaoona Dr. Slaa kateleza hasa majibu yake juu ya kwanini anayo kadi ya CCM, kundi la pili la watetezi wake na kundi la tatu la watazamaji wasiokuwa na upande maalum.

Nikiri wazi kuwa pamoja na kuwa mimi ndie niliyeanzisha mjadala huu, namheshimu sana Dr. Slaa kama mtu mzima sana kwangu na ndo maana huwa namuita babu,lakini bila kumumunya maneno ana mchango katika demokrasia ya nchi yetu bila kujali ni chanya au ni hasi.

Nilipo hoji umiliki wake wa kadi ya CCM nikiri kuwa sikutegemea kama angekiri haraka kiasi kile kuwa kweli anamiliki kadi, tena anaitunza kama kumbukumbu. Ndio maana mara baada ya kukiri haraka sana nilitoka hadharani na kumpongeza kwa mara ya kwanza toka nimfahamu ameamua kuwa mkweli. Nikasema ameanza vizuri kujifunza kuwa mkweli,baada ya orodha ndefu ya uongo na uzushi mwingi aliouzoea katika maisha yake ya siasa na yale ya utumishi wa Mungu yaliyomfikisha kwenye kumuasi Mungu na kanisa achilia mbali familia yake yaani mke na watoto.

Jambo kubwa hapa ambalo wapambe wake wanalifanyia unafiki ni kuwa nilipohoji SIKUHOJI UANACHAMA WAKE, NILIHOJI KUWA NA KADI YA CCM MPAKA LEO, TOKA ATOKE CCM KWA MAKEKE. Natambua vizuri sana kuwa uanachama wa CCM kwa mujibu wa Katiba ya CCM ya mwaka 1977 matoleo yote, moja ya sababu ya kukoma uanachama ni kuwa mwanachama wa chama kingine cha siasa. Kwa tafsiri rahisi inatosha kujua kuwa Dr. Slaa si mwanachama wa CCM tena. Swali langu likawa kwanini anamiliki kadi ya CCM mpaka leo?

Watetezi wake hebu muulizeni Dr. Slaa alipoasi upadri nyumba ile ya utawa aliyokuwa akiishi kama padri aliondoka na funguo za ile nyumba au vifaa vingine vya upadri kwa madai kuwa ni kumbukumbu kuwa alikuwa padri wakati flani katika maisha yake? Tusikurupuke kumtetea tukadhani tunamsaidia ,kumsaidia kwa kweli ni kumwambia ukweli kuwa hapa babu umeteleza.

Wapo wanaodai hoja hii haina mashiko eti kwasababu hawaoni kama itabadili maisha ya watu masikini. Hawana makosa kusema haya kwasababu ndipo uwezo wao wa kufikiri walipoamua uishie. Lakini hebu fumbueni macho mtazame ukweli huu, moja ya tatizo kubwa la binadamu wengi na hasa viongozi ni kuwa wazuri sana wa kusema wasiyoyaamini wala kuyaishi ndo maana nchi nyingi masikini, rasilimali zake hazifaidishi walio wengi bali wachache sana,huku wakidai tufunge mkanda wakati wao wanaongeza ukubwa wa suti kwani zinawabana zilizopo.

Wakati flani Kardinali Pengo aliwa kusema, wengi wa wanaopigia kelele ufisadi ni mafisadi watarajiwa lakini kwasasa kwasababu hawajapata furusa za kuwa mafisadi ndo maana wana piga kelele.

Ikumbukwe Dr. Slaa amekuwa akipiga kelele na kuwataka wana CCM waliochoka CCM warudishe kadi za CCM na mfano mzuri ni pale Jangwani ambapo baada ya kulewa ujinga akaamua kuubatiza jina jingine uwanja wa Jangwani, bahati mbaya watanzania wana akili wakampuuza na wakaendelea kuenzi historia nzuri ya uwanja wa Jangwani kwa kuuita jina lake la asili, nadhani ulevi ule ulipoisha wa babu na wapambe wake akagundua kuwa alikuwa amelewa tu ndio maana hawajakumbushia tena jina lile.

Kwanini kama ni mkweli wa nafsi yake asiwaambie wanaorudisha kadi za CCM ukweli kuwa hata yeye katunza yake kama kumbukumbu kwahiyo nao watunze zao kama kumbukumbu, badala ya kuwahimiza warudishe wakati yeye katunza yake? Wapambe wake hili pia mnalifanyia unafiki!!!

Wakati yeye akimiliki kadi ya CCM amekuwa bingwa wa kuwashutumu wenzake *kuwa ni mamluki eti wa CCM ndani ya Chama chake wakati kati ya hao anaowashutumu na wengine kuwafukuza wengine hawajawahi hata kuwa na kadi tu za CCM. Watetezi wa babu hebu tuwe wa kweli kama kadi hii angekiri anayo Zitto hali ingekuaje? Mngetoka kumtetea pia dhidi ya hasira za babu na wafuasi wake dhidi ya Zitto au hasimu wake yeyote mwingine?

Babu anatofauti gani na wanaohimiza watu kujikinga na ukimwi wakati wao hata kinga hawaijui? Wanahutubia mkutano wa kupinga rushwa mpaka mapovu yanawatoka wakishuka wao ndo wanaulizia rushwa tena kwa ukali mkubwa? Anatofauti gani na msimamizi wa hospitali anayehimiza watu wakatibiwe kwenye hospitali hiyo na huku yeye mwenyewe hana imani na tiba za pale matokeo yake hata homa tu anakwenda ng'ambo kuitibu? Huyu ndo mnataka awe kiongozi mkuu wa nchi yetu? Anasema asiyoyaamini na kuishi asiyoyasema??!!

Mnasema ni hoja ya kipuuzi huku bado kucha kuchwa mnaijadili? Kwanini mjadili hoja ya kupuuzi kama kweli ni ya kipuuzi? Huu ni unafiki haupaswi kufumbiwa macho, ni vizuri tujifunze kukubali kujikosoa na kukosolewa.

Sina tabu na umiliki wa babu wa kadi ya CCM kama tu angewahamasisha na wengine wafanye kama anavyofanya yeye, kuongoza ni kuonyesha njia. Si uongozi bora kusema fuateni maneno yangu na si matendo yangu, kiongozi wa namna hiyo hatumhitaji kwasasa.

Ndio maana tunashuhudia Chadema chini ya babu huyu kama katibu mkuu wa chama, wameshindwa mpaka leo kuweka bayana msimamo wao juu ya sera za ushoga huku wakiwa marafiki na wapokeaji wakubwa wa misaada kutoka kwa waumini wakubwa wa ushoga duniani. Wanasiasa wanaosema wasichoamini na hawatendi isipokuwa wanataka watu watende. Onyesheni upendo wa kweli kwa babu yangu huyu kwa kumwambia ukweli badala ya kumdanganya na kumfanya apumbazike. KUONGOZA NI KUONYESHA NJIA.

Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki CCM.

Imetolewa na;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa

nisingependa lakini nalazimika kukuita mjinga kwa sababu chache!
1.Wewe unawezaje kufananisha kadi ya chama na funguo za nyumba ya mapadre? ni wazi ujue kuwa nyumba ya mapadre ni mali ya kanisa na hata baadhi ya vifaa vya kuendeshea ibada ni mali ya kanisa sasa wewe ulitaka aondoke navyo kivipi? kumbukumbu za upadre wake anaweza kuwa nazo kama biblia,,vitabu mbalimbali na hata baadhi ya mavazi kama kanzua ambayo sio mali ya kanisa

2.Unasema kuwa Dr, amezoea uwongo na uzushi mwingi, fine hebu tuorodheshee uwongo wake? unakumbuka list of shame ya mwembe yanga? unakumbuka kashfa ya EPA unakumbuka meremeta na Deep green? wote huo uwongo na uzushi wa doctor??

3.Umefikia hata hatua ya kuingilia privacy na maisha ya mtu kibinafsi? unajua ni sababu zipi za msingi zilizoshabaisha doctor akaacha upadre? na kitu cha ajabu unasema kuwa kamuasi mungu? kuasi maana yake asingeendelea kuwa muumini badala yake angeanza kuwa mfuasi wa shetani na kufanya maovu, kuhusu familia sio jambo la ajabu watu kutengana! Nelson Mandela baba wa Africa alitengena na Winnie and still amekuwa ni rasi bora mno Africa,ungefuatilia ujue chanzo na slaa na rose kutengena sio unarusha lawama za jumla

3.Unamnukuu Mwadhama akisema wapinga ufisadi nao ni mafisadi hapa sijakuelewa kwamba basi wewe unatetea mafisadi Pengo nae aliwatetea? Siamini Pengo nayemfahamu kama kiongozi wangu wa kanisa angeweza kuongea utumbo huu wewe ndio umemlisha maneno!

4.Viongozi wengi wa CCM ambao wana kadi moja tu ya ccm mbona ndio hao sasa wanaongoza kwa kuuza nchi, rasilimali na kuhamisha mabilioni na kuyaficha nje!

Mwisho*CCM ni janga la kimataifa ni kansa inatafuna watanzania ni kirusi kinachosababisha ugonjwa wa umaskini na kunenepesha wagonjwa wa ufisadi, lazima tuiong'oe sasa na haraka
 
Nape hebu mwige Mnyika anavyotenga hoja za kulisaidia taifa sasa unahama kwenye uenezi wa chama unaanza umbea na unafiki ndivyo unataka ziwe siasa za chama unatuabisha vijana kama vijana ukiheshimiwa na chama na rais ukapewa nafasi ndivyo haya heri wazee waendelee.
We unadhani jk alivyosema muwe mnajibu na akakusifu unasema amekupa nafasi ya kuandika upuzi na vioja unajidhalilisha.
heri uombe likizo isiyokuwa hata na malipo ukapumzike upate muda wa kutafakari changamoto za taifa nawe kama kijana unaonyesha njia gani kuzitatua pia ukasoma jinsi vijana wenzako mnyike, lema, lissu na zitto na wakina mde wanavyojibu hoja

Jamani acheni kudanganya hivi mfano lema kuna hoja ambazo huwa anajibu zaidi ya kila kukicha kuhamasisha watu kuandamana na kuingia mstuni ? Ebu twende kwa lissu yeye kila kukicha kushambulia watu binafsi hivi sasa hana hoja nyingine zaidi ya majaji sana sana nawafagilia mnyika na zitto,lakini hanachofanya napa hakitpfautiani na viongozi wote wa siasa kuanzia dr slaa mpaka kina mbatia na mrema
 
hiv prezdaa wetu mbona ana watoto wengi kila mtoto ana mamake. mi nilfikiri riz1 mamake ni salma kumbe sio.
 
Nape asipotoshe. Rushwa ilitawala Uahaguzi ndani ya CCM na hao ndio wanaongoza nchi. Tutarajie nini? Tunatakiwa kujadili masuala ya kitaifa kama vile ajira, rushwa iliyotamalaki, wanafunzi kufaulu mitihani wakati hawajui kusoma na kuandika, fedha zilizopo Uswiss, wizi wa EPA, Meremeta...nk.
Nape kuleta mjadala wa Dr. Slaa inaonyesha akili yake ilivyo ndogo. Small minds discuuss people. This is typical of huyu Mnyakyusa Nape.
 
Nape,
Ni ngumu sana kwa mtu kujadili hiki unachokiita mada. Kwa uhalisia hii siyo mada ni siasa majitaka.
Pamoja na kuwa katika kundi la watazamaji nashindwa kujiuzuia kujibu hoja zako kwasababu zifuatazo;

1. Unachotaka ni mjadala uendelee kwasababu tayari umeshaona matunda yake(Mjadala usio na tija na taifa)
2. Watanzani wafahamu kwanini sisi tumebaki kuwa nchi masikini duniani
3. Hatari inayolikabili taifa huko mbeleni kama hatutachukua hatua madhubuti.

Sikutegemea kijana wa umri na wadhifa kama wako ndani ya chama tawala ungeweza kujinasibu kuanzisha mjadala(ambao si mjadala) kwa hoja dhaifu hafifu na inayodhalilisha kama hii.

Kwasisi wengine unatuacha na maswali, je wale vijana walioshauriwa wachukue uongozi kwa kuwa ni wakati wao ndio hawa kweli? Hivi kuna watu tunaowategemea kutoa dira na mwelekeo wa taifa kweli!!

Nilitegemea ungekuwa umeanzisha mada zinazogonganisha vichwa juu ya hali ya nchi yetu na mustakabali wake leo na kwa vizazi vijavyo. Kwa bahati nzuri sana kwa wapotofu na ambayo ni mbaya sana kwa dunia hii hukufanya hivyo.

Ukisoma maandishi yako huwezi kumdanganya mtu kuwa unamheshimu Dr Slaa. Hakika umemvunjia heshima ikamilifu.
Dr Slaa kama mwanadamu mwingine ana maisha yake binafsi kama alivyokuwa mzee Nanuye.
Sijui utajisikia vipi leo watu wakijadili undani wa maisha ya Nnauye hadi mauti yanamfika! Fikiri hilo kwa makini.

Mifano unayotoa hailingani na elimu au hadhi yako.
Kama mtazamaji nimeshindwa kuelewa uhusiano wa funguo za Nyumba ya upadre na kadi.

Kama utakuwa na ufahamu kuna mzozo uliokuwepo kuhusu Mwalimu Nyerere na zawadi alizopewa zile za kitaifa na binafsi. Hakuna mzozo kuhusu umiliki wa funguo za Ikulu, lile gari la kwanza la TANU n.k.
Mfano wako ni hafifu sana na ninawasi wasi na ujana kama si uwezo wako kifikra.

Umebadili hoja na kukudai Dr Slaa si Mwanachama. Umesahau ulisema analipia kadi.
Baada ya wananchi kukuonyesha jinsi usivyoijua katiba ya chama unachoongoza, utaratibu wa nchi kuhusu uongozi na vyama vya siasa sasa unakuja na habari ya kukanusha. Tunazo kumbu kumbu na zikitolewa ni aibu kwa taifa si wewe.

Umezungumzia kuhusu uongo wa kisiasa wa Dr Slaa. Ingefaa uweke wazi madai hayo kwasababu yale tunayoyasikia hakunahata moja lililokanushwa na serikali inafanyia kazi. Mathalani orodha ya mafisadi 11, serikali ya chama chako imefikisha watu mahakamani. Hebu tueleze mengine ya uongo na uzushi hasa sisi watazamaji.

Umesema kuongoza ni kuonyesha njia na kiongozi asemaye fuateni maneno yangu na si matendo huyo hatufai kwa sasa.
Nakaubaliana na maneno yako matamu sana. Lakini Nape wewe umesimama katika kutenda unayoyasema?
Mbona hujatuonyesha njia ya kukabiliana na dhambi zilizotitia ndani ya chama na serikali ya chama chako?

Mbona hatujaona matendo ya maneno uliotuahidi kuhusu vita dhaidi ya ufisadi na kuvua watu magamba?
Je, siku tisini zinaisha lini ili tujue kuwa sasa upo katika matendo zaidi ya kauli?
Je, kuhamishia kodi za taifa Uswiss ndiko kuonyesha njia?
Je, kutoa na kupokea rushwa(Kikwete kasema) kulikokithiri ndani ya chama chako tawala(Sumaye)ndiko kuonyesha njia?

Endapo Dr Slaa ni mfano wa viongozi wanaohimiza watu ''wakatibiwe katika hospitali wasizo na imani nazo'' Nape umesahau kuwa Mwenyekiti wako wa chama anachekiwa(si kutibiwa) afya Ulaya? Umesahau kuwa Marais wote na mawaziri wakuu wastaafu na waliojiuzulu kutoka chama chako wanatibiwa Ulaya kwa pesa za walipa kodi?
Je, nao wana walk the talk! Je, wanasimamia kauli kuwa Muhimbili ni pazuri sana na twende huko si ulaya, India n.k!

Spika wa bunge linaloongozwa na chama chako amefikia mahali pa kuita wahindi waje kucheki afya za wabunge, je, naye anahimiza matibabu kule asikotibiwa au ana walk the talk kwa maana yako? Anatenda anachohubiri au naye ni kama Slaa asiye walk the talk kwa maana yako

Sijui kingetokea nini kama Zitto ndiye angesema ana kadi hiyo. Ninashindwa kutabiri kwasababu sijui kingetokea nini kama Selelii, Shelukindo wangekutwa na ufisadi wa kuhujumu nchini kama ilivyo kwa Lowassa na Chenge!
Hilo sitakubaliana nawe unless unishawishi kuwa mfano huo hauna uwiano.

Mwisho kabisa, Nape nakushauri ujikite na kujifunza siasa za kileo kulingana na elimu yako, exposure na nafasi yako.
Mijadala kama hii unaoyiita mijadala inadhalilisha sana nafasi ya uongozi katika nchi yetu.

Katibu mwenezi wa chama tawala, mjumbe wa halamashauri kuu, mkutano mkuu na kamati kuu unapolete hoja za kiwango duni katika mizania hii, masikini wa TZ hana sababu ya kuwa na tumaini tena bali kilio na msiba tu.

Nape, unazidi kuipa nguvu hoja ninayoitetea kila siku kuwa uongozi ni hekima, maono na busara wala si umri , jinsia, kabila au dini. Uongozi ni kitu anachotunukiwa mtu na mola wake wala si unasaba au kurithishana kwa majina.

Ungekaa kimya ingekusaidia sana maana kila unapoandika unatutoa mashaka tuliyokuwa nayo juu yako.

Wako Raia mtiifu

Nguruvi3
 
Huyo ndio mtoto wa Marck Mwandosya bwana utamtambuaje weweeeeeeeeeeee mzee alichakachua na Mnyira eti nasikia...............
 
DR. SLAA NA KADI YA CCM, NA UNAFIKI WA WATETEZI *WAKE

Kwa muda sasa wa karibu wiki tatu au nne pamekuwa na mjadala mkubwa juu ya kumiliki kadi ya CCM kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA na padri aliye asi Dr. Wilbroad Slaa.Mjadala huu umeingiza watu wengi sana kwenye maeneo mbalimbali lakini ukigawa wajadiliji kwenye makundi matatu makubwa, kundi la kwanza la wanaoona Dr. Slaa kateleza hasa majibu yake juu ya kwanini anayo kadi ya CCM, kundi la pili la watetezi wake na kundi la tatu la watazamaji wasiokuwa na upande maalum.


Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki CCM.

Imetolewa na;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa...........

Bora uwe masikini wa kipato lkn siyo wa fikira. Hapa nape uliipoteza muda mwingi kuandika *****. Inaonesha dhahili kuwa ili suala la Mkuu wetu Dr. wa ukweli, CCM mnataka kulitumia kukwepa kujibu hoja za wananchi za ugumu wa maisha.

Fanya kazi na mtatue matatizo ya wa tz na siyo slaaa slaaa slaaa kila kukicha.
 
Nape,
Ni ngumu sana kwa mtu kujadili hiki unachokiita mada. Kwa uhalisia hii siyo mada ni siasa majitaka.
Pamoja na kuwa katika kundi la watazamaji nashindwa kujiuzuia kujibu hoja zako kwasababu zifuatazo;

1. Unachotaka ni mjadala uendelee kwasababu tayari umeshaona matunda yake(Mjadala usio na tija na taifa)
2. Watanzani wafahamu kwanini sisi tumebaki kuwa nchi masikini duniani
3. Hatari inayolikabili taifa huko mbeleni kama hatutachukua hatua madhubuti.

Sikutegemea kijana wa umri na wadhifa kama wako ndani ya chama tawala ungeweza kujinasibu kuanzisha mjadala(ambao si mjadala) kwa hoja dhaifu hafifu na inayodhalilisha kama hii.

Kwasisi wengine unatuacha na maswali, je wale vijana walioshauriwa wachukue uongozi kwa kuwa ni wakati wao ndio hawa kweli? Hivi kuna watu tunaowategemea kutoa dira na mwelekeo wa taifa kweli!!

Nilitegemea ungekuwa umeanzisha mada zinazogonganisha vichwa juu ya hali ya nchi yetu na mustakabali wake leo na kwa vizazi vijavyo. Kwa bahati nzuri sana kwa wapotofu na ambayo ni mbaya sana kwa dunia hii hukufanya hivyo.

Ukisoma maandishi yako huwezi kumdanganya mtu kuwa unamheshimu Dr Slaa. Hakika umemvunjia heshima ikamilifu.
Dr Slaa kama mwanadamu mwingine ana maisha yake binafsi kama alivyokuwa mzee Nanuye.
Sijui utajisikia vipi leo watu wakijadili undani wa maisha ya Nnauye hadi mauti yanamfika! Fikiri hilo kwa makini.

Mifano unayotoa hailingani na elimu au hadhi yako.
Kama mtazamaji nimeshindwa kuelewa uhusiano wa funguo za Nyumba ya upadre na kadi.

Kama utakuwa na ufahamu kuna mzozo uliokuwepo kuhusu Mwalimu Nyerere na zawadi alizopewa zile za kitaifa na binafsi. Hakuna mzozo kuhusu umiliki wa funguo za Ikulu, lile gari la kwanza la TANU n.k.
Mfano wako ni hafifu sana na ninawasi wasi na ujana kama si uwezo wako kifikra.

Umebadili hoja na kukudai Dr Slaa si Mwanachama. Umesahau ulisema analipia kadi.
Baada ya wananchi kukuonyesha jinsi usivyoijua katiba ya chama unachoongoza, utaratibu wa nchi kuhusu uongozi na vyama vya siasa sasa unakuja na habari ya kukanusha. Tunazo kumbu kumbu na zikitolewa ni aibu kwa taifa si wewe.

Umezungumzia kuhusu uongo wa kisiasa wa Dr Slaa. Ingefaa uweke wazi madai hayo kwasababu yale tunayoyasikia hakunahata moja lililokanushwa na serikali inafanyia kazi. Mathalani orodha ya mafisadi 11, serikali ya chama chako imefikisha watu mahakamani. Hebu tueleze mengine ya uongo na uzushi hasa sisi watazamaji.

Umesema kuongoza ni kuonyesha njia na kiongozi asemaye fuateni maneno yangu na si matendo huyo hatufai kwa sasa.
Nakaubaliana na maneno yako matamu sana. Lakini Nape wewe umesimama katika kutenda unayoyasema?
Mbona hujatuonyesha njia ya kukabiliana na dhambi zilizotitia ndani ya chama na serikali ya chama chako?

Mbona hatujaona matendo ya maneno uliotuahidi kuhusu vita dhaidi ya ufisadi na kuvua watu magamba?
Je, siku tisini zinaisha lini ili tujue kuwa sasa upo katika matendo zaidi ya kauli?
Je, kuhamishia kodi za taifa Uswiss ndiko kuonyesha njia?
Je, kutoa na kupokea rushwa(Kikwete kasema) kulikokithiri ndani ya chama chako tawala(Sumaye)ndiko kuonyesha njia?

Endapo Dr Slaa ni mfano wa viongozi wanaohimiza watu ''wakatibiwe katika hospitali wasizo na imani nazo'' Nape umesahau kuwa Mwenyekiti wako wa chama anachekiwa(si kutibiwa) afya Ulaya? Umesahau kuwa Marais wote na mawaziri wakuu wastaafu na waliojiuzulu kutoka chama chako wanatibiwa Ulaya kwa pesa za walipa kodi?
Je, nao wana walk the talk! Je, wanasimamia kauli kuwa Muhimbili ni pazuri sana na twende huko si ulaya, India n.k!

Spika wa bunge linaloongozwa na chama chako amefikia mahali pa kuita wahindi waje kucheki afya za wabunge, je, naye anahimiza matibabu kule asikotibiwa au ana walk the talk kwa maana yako? Anatenda anachohubiri au naye ni kama Slaa asiye walk the talk kwa maana yako

Sijui kingetokea nini kama Zitto ndiye angesema ana kadi hiyo. Ninashindwa kutabiri kwasababu sijui kingetokea nini kama Selelii, Shelukindo wangekutwa na ufisadi wa kuhujumu nchini kama ilivyo kwa Lowassa na Chenge!
Hilo sitakubaliana nawe unless unishawishi kuwa mfano huo hauna uwiano.

Mwisho kabisa, Nape nakushauri ujikite na kujifunza siasa za kileo kulingana na elimu yako, exposure na nafasi yako.
Mijadala kama hii unaoyiita mijadala inadhalilisha sana nafasi ya uongozi katika nchi yetu.

Katibu mwenezi wa chama tawala, mjumbe wa halamashauri kuu, mkutano mkuu na kamati kuu unapolete hoja za kiwango duni katika mizania hii, masikini wa TZ hana sababu ya kuwa na tumaini tena bali kilio na msiba tu.

Nape, unazidi kuipa nguvu hoja ninayoitetea kila siku kuwa uongozi ni hekima, maono na busara wala si umri , jinsia, kabila au dini. Uongozi ni kitu anachotunukiwa mtu na mola wake wala si unasaba au kurithishana kwa majina.

Ungekaa kimya ingekusaidia sana maana kila unapoandika unatutoa mashaka tuliyokuwa nayo juu yako.

Wako Raia mtiifu

Nguruvi3

Sijui kama atayaelewa haya!!
 
nape,

katiba ya ccm inasema kadi ni mali ya ccm ama ya mwanachama?

Huna mkakati mwingine wa kumarisha chama chako cha ccm zaidi ya kujidharirisha na mbinu hafifu za kuua mshikamano wa chadema?

Huna sifa, uwezo wala vigezo vya kupambana na dr slaa wewe. Waliokushauri wana kudanganya.


Ushauri wangu, kama huna job description ama huna kazi za kufanya katika kufufua chama chako ccm, omba likizo isiyo na malipo ukapumzike. Unachokifanya sasa kinazidi kuharibu image ya ccm na kinaweka peupe namna gani mmebaki watupu........

Kumbe slaa yuko kwa ajili ya mapambano ee! Ccm ipo kwa ajili ya kushughulikia mambo ya msingi na sio kupambana na watu. Sasa kama chadema mmeji tune kwa mapambano mtapambana na wengine lakini si CCM.
 
Mimi nilipona huu uzi nikajua kwamba leo Nape amelete uthibitisho kama alivyoahiadi kwamba Dr. Slaa anamiliki kadi ya CCM na amekuwa akiilipipia kila mwaka.

Tena Nape akaenda mbali zaidi kwamba kama Dr. Slaa atabisha kwamba sio mwanachama hai wa CCM, basi ataweka vielelezo vyake jinsi anavyolipia kadi hiyo ya CCM (Please mwenye ujumbe huo wa Nape auweke tena for the sake of the record).

Mimi nikaahidi kama kweli Dr. Slaa analipia kadi ya CCM basi nitakuwa mtu wa kwanza kurudisha kadi ya CDM. To my surprise leo Nape anakuja na hadithi nyingine za Alfu Lela Ulela. Hivi Nape anafahamu ni watu awa aina gani tunaosoma mtandao wa JF.

Nape hizo siasa za stone age hapa JF hazikujengi wewe na Chama chako bali zinawabomoa. It is my two cents advise to you and your party.
 
Ccm nambari wani kwa mafisadi, wezi, wauaji, wazinzi n.k n.k
 
Nape anajua anafanya nini, Mwache atape tape, maana kama wakitoka madarakani wana jua moto unaokuja, wengi watakimbia nchi. watu wana tuibia alafu wana kuja kutukana hapa...Nape omba hiyo siku isifike, tutaanza na wewe!
 
Nape umezidi kudhihilisha upunguani wako,mimi huwa napenda kukuita PUNGUANI,maaana mambo yote unayoyafanya
hufanywa na PUNGUANI tu,kote Duniani.maana wanaoongoza kwa kutenda,na kusema wasiyoyaamini ni wewe na chama
chako na sio Dr.SLAA.

Mfano,ni wahubili wazuri wa kutunza amani na utulivu huku ni wa kwanza kuvuruga amani,wahubili wazuri wa kupinga rushwa,Udini huku ndio wala rushwa wakubwa mpaka kwenye chaguzi zeni na wadini wakubwa,hii ni mifano michache kwa kutaja.
 
Kageuka kiukwel cjaona pointi kabisa uliyozungumza ila ni propaganda tuu, hata huwo mfano uliotoa kwamba padri akiasi mbona haondoki na ufunguo..?

Hii ni sawa nakusema kwamba kwa nini dereva anapo acha kazi haondoki na funguo za gari..? Kageuka kwanza naomba utofautishe mali ya taasisi flani na mali ya mtu mmoja mmoja aidha kutoka kwenye taasisi flan, kama ilivyo kwa Dr. Slaa alivyokuwa CCM ile kadi ya CCM ilikuwa ni kadi yake mwenyewe ila kutoka kwa CCM na cha ziada ni kwamba hamna mahali popote kwenye ile kadi polipo andikwa kwamba ukihama chama ni lazima huirudishe kadi ya chama kwenye tawi lolote la chama. so mbona hatusemi kwa Wassira kumiliki kadi ya NCCR-Mageuzi na bado ni waziri wa serikali ya CCM, na tena alikili kumiliki kadi hiyo kama kukumbu yake mbona hilo hamsemi...?

Dr. Slaa is not a traitor as u think but is a fore fighter of democracy!!! He is and we believe in him not only because of his name but coz of his patriotism... Vivas forever CHADEMA....
 
Back
Top Bottom