Nape nnauye kanunuliwa na mafisadi??

Afadhali umeliweka hili sawa. Nilianza ku-doubt niliposoma thread hii nikadhani sikukusikiliza vizuri kwenye ITV usiku wa Jumamosi. Wewe ni mpiganaji, keep it up, boy! Naunga mkono pia wazo lako la kujadili vipengele muhimu kwenye waraka wa Wakatoliki.
 
Nape we ni ndugu yangu na rafiki yangu....kukuleta jamvini sikupenda lakini kutokana na ukaribu nikaona utaona nakuasi.....tunachotaka bw nnauye usibadilishe misismamo yako....na kitendo cha kuja huku ni ile heshima yako iendelee kwa jamiii
Nadhani simtoto wala mkubwa aliesikiliza taarifa ile unless ulisema mengine na kwenye TV wakatuonyesha mengine...naona hoja yako mjadala ufungwe ila ningependa umalizike kwa manufaa yako ...kwa kukuona ukiwa serious na hawa mafisadi na si kwamba wakiwachunia labda kwenye migao mnaanza kukurupuka na vibomu......binafsi nakutakia kila la kheri ila ningependa uombe mkanda mzima wa ile shuguli uone ulichongea....wazo muhimu napenda kukwambia hivi sasa makanisa yameamka.....kama wengine wamelala nakuhakikishia MAKANISA YOTE YATAHAKIKISHA HAKI YA MTU AIPOTEI NAHAO WANAOIJIITA MAFISADI AIBU LAZIMA IWAKUMBE HATA MKIWATETEA....NAKUTAKIA UDC MWEMA...MUNGU AKIPENDA
 
Wakubwa heshima kwenu!
Nimelazimika kuingia mapema kujaribu kuweka mambo sawa ili mjadala uwe na manufaa.
1.kwa aliyeangalia vizuri taarifa ile wakati mimi nazungumza nilichokisema ni kuwa, MCHANGO WA VIONGOZI WA DINI KATIKA AMANI NA UTULIVU WA NCHI YETU NI MKUBWA MNO NA WANASIASA WAUHESHIMU. LAKINI PIA NIKASISITIZA KIZAZI HICHI CHETU KUKABILIWA NA KANSA MBAYA YA UFISADI NA RUSHWA NA KUWAOMBA VIONGOZI WA DINI WASAIDIE SERIKALI KATIKA VITA YA KUKIOKOA KIZAZI NA KANSA HII.
2. KAMWE KATU HAKUNA BEI YA UTU WANGU,NA KWAKWELI KUSEMA NAPE KANUNULIWA KWANGU NI ÑATUSI MAKUBWA.NACHUKIA UFISADI LEO KULIKO JANA..NA GRAFU ITAENDELEA KUPANDA YA KUCHUKIA UFISADI NA KUUPIGA VITA.

3. NAAMINI KATIKA UZALENDO KWA NCHI KWANZA CHAMA BAADAE,NIMEKUWA NIKIYASEMA HAYA NA KUYAAMINI HADHARANI,HIVYO SI SAHIHI KUSEMA ETI KWA NAPE CCM NDIO BABA NA MAMA YAKE. KUMBUKENI NILIKUWA TAYARI KUFUKUZWA CCM KWA KUSIMAMIA HAKI LEO KUTUMIA MANENO YA KEJELI KAMA HAYA SI SAWASAWA NADHANI.

4. NAAMINI YAPO MAMBO HAYAWEZEKANI KWA NGUVU YA SIASA PEKEYAKE INAHITAJIKA NGUVU YA DINI/MUNGU,NA KWAKWELI KATIKA HILI NIMESOMA WARAKA WA MAASKOFU TOKA MWANZO MPAKA MWISHO SIJAONA KASORO NATAMANI TUUCHUKUE UWE SEHEMU YA ILANI YA CHAMA. NAWAPONGEZA MAASKOFU.

Sasa tujadili.
Nape Nnauye

Kama huyu kweli Nnape kuna shughuli ya kurekebisha kiswahili kidogo hapo.
Anyway, mie nilikuwa nashangaa mbona mara hii ule moto uliouwasha umetulia au mafisadi nao wako likizo?! Ningekushauri uunganishe nguvu zako na wapambanaji wengine hata kama mnatofautiana itikadi. Huu si wakati ya kunyamaza.
 
Back
Top Bottom