Wakubwa heshima kwenu!
Nimelazimika kuingia mapema kujaribu kuweka mambo sawa ili mjadala uwe na manufaa.
1.kwa aliyeangalia vizuri taarifa ile wakati mimi nazungumza nilichokisema ni kuwa, MCHANGO WA VIONGOZI WA DINI KATIKA AMANI NA UTULIVU WA NCHI YETU NI MKUBWA MNO NA WANASIASA WAUHESHIMU. LAKINI PIA NIKASISITIZA KIZAZI HICHI CHETU KUKABILIWA NA KANSA MBAYA YA UFISADI NA RUSHWA NA KUWAOMBA VIONGOZI WA DINI WASAIDIE SERIKALI KATIKA VITA YA KUKIOKOA KIZAZI NA KANSA HII.
2. KAMWE KATU HAKUNA BEI YA UTU WANGU,NA KWAKWELI KUSEMA NAPE KANUNULIWA KWANGU NI ÑATUSI MAKUBWA.NACHUKIA UFISADI LEO KULIKO JANA..NA GRAFU ITAENDELEA KUPANDA YA KUCHUKIA UFISADI NA KUUPIGA VITA.
3. NAAMINI KATIKA UZALENDO KWA NCHI KWANZA CHAMA BAADAE,NIMEKUWA NIKIYASEMA HAYA NA KUYAAMINI HADHARANI,HIVYO SI SAHIHI KUSEMA ETI KWA NAPE CCM NDIO BABA NA MAMA YAKE. KUMBUKENI NILIKUWA TAYARI KUFUKUZWA CCM KWA KUSIMAMIA HAKI LEO KUTUMIA MANENO YA KEJELI KAMA HAYA SI SAWASAWA NADHANI.
4. NAAMINI YAPO MAMBO HAYAWEZEKANI KWA NGUVU YA SIASA PEKEYAKE INAHITAJIKA NGUVU YA DINI/MUNGU,NA KWAKWELI KATIKA HILI NIMESOMA WARAKA WA MAASKOFU TOKA MWANZO MPAKA MWISHO SIJAONA KASORO NATAMANI TUUCHUKUE UWE SEHEMU YA ILANI YA CHAMA. NAWAPONGEZA MAASKOFU.
Sasa tujadili.
Nape Nnauye