KATIBU wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, ametangaza kiama cha walanguzi wa ufuta kwa kuitaka Serikali ya Wilaya ya Kilwa na Mkoa wa Lindi kuhakikisha inakomesha ulanguzi huo mara moja. Aidha, amemtuhumu waziwazi mmoja wa wabunge, Mbunge wa Kilwa Kusini, Selemani Bungala `*****' (B.we.g.e ili ni tusi) kuwa ni mmoja wa walanguzi, huku akimtaka arejee bungeni kuwawakilisha wananchi wake, badala ya kuwakandamiza kiuchumi. Nape aliyasema hayo kwa nyakati tofauti katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika mji mdogo wa Kilwa Kivinje na Kilwa Masoko katika ziara ya siku mbili ya baadhi ya wajumbe wa Sekretarieti ya CCM mkoani Lindi katika kufikisha ujumbe wa maamuzi ya NEC yaliyofanyika mjini Dodoma Aprili mwaka huu. Kwa mujibu wa Nape wapo viongozi wa kisiasa wanaongoza dhuluma hiyo kwa kisingizio cha kuwasaidia wakulima wakati ukweli wanawadhulumu na kumshushia tuhuma hizo Mbunge wa jimbo hilo, '*****'(Bweg.e) kuwa ni kinara wa dhuluma hiyo. "Naambiwa Mbunge wenu bwana '*****' (Bweg.e)kaacha Bunge la Bajeti na kuja kusimamia dhuluma yake dhidi ya wakulima masikini wa ufuta. *****(Bweg.e) rudi bungeni kama hujui kazi yako ni kuwatetea wananchi, basi bora ujiuzulu wananchi wapate mwakilishi na si mlanguzi" alisema Nape. Alisema wakati bei ya dira mwaka huu ni Sh 1,000 ambayo Serikali iliagiza mkulima alipwe yote ndio asubiri malipo ya pili ambayo nayo yatakuwa mazuri kwani bei ya ufuta safari hii ni nzuri, walanguzi wananunua ufuta kwa kati ya Sh 1,150 na Sh 1,200 ambayo ni wizi kwa wakulima. Akifafanua wizi huo Nape alisema, ushahidi wa wazi uliopo walanguzi wamechezea mizani yao na kwa kila kilo moja wanaiba kati ya robo na nusu kilo na hivyo bei ya Sh 1,200 wanayonunua walanguzi ni danganya toto kwani tayari wameshafidia kwenye mizani za wizi. "Mizani za vyama vyetu vya ushirika imepimwa na wakala wa vipimo hivyo ni sahihi na tayariS yenu imeshasimamia upatikanaji wa bilioni kumi na moja kutoka benki za NMB na CRDB kwa ya ununuzi wa ufuta msimu huu, hivyo hakuna sababu ya wakulima wa ufuta kuendelea kudhulumiwa na hawa matapeli," Alisisitiza Nape. Alisema kuendelea kukwepa mfumo wa stakabadhi ghalani ni kwenda kinyume na maamuzi ya RCC, ambacho ni kikao halali na hata Baraza la Madiwani ambao ni wawakilishi halali wa wananchi. "Naambiwa wako na baadhi ya madiwani wa CCM wanaojihusisha na dhuluma hii, naagiza ushahidi ukipatikana vikao vya chama mchukue hatua kali dhidi yao, tuko tayari kufanya uchaguzi mdogo kuliko kuvumilia dhuluma hii," alisema Nape. Mapema, Nape akizungumza na viongozi hao alieleza kwa kina lengo la hatma ya CCM kufanya mabadiliko ‘kujivua gamba' mjini Dodoma na kwamba moja ya malengo ni kukirejesha chama kwenye misingi yake ili kiweze kukidhi kwa dhati matarajio ya wananchi hasa wanyonge.