.....Nilisikia Nape siyo mtoto wa mzee Nnauye ndo maana hajatajwa hapo juu. Eti wanadai Nape ni mtoto wa nanihii, Mzee Nnauye alisakiziwa tu!!.mbona jina halionekani hapa
![]()
WanaJF na Watanzania Wote,Salaam.
Naandika kujibu hofu,wivu,mashaka na upotoshaji pia wa makusudi unaofanywa baada ya Picha na habari kusambaa zinazoonyesha namna Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe alivyoapisha Vikundi Vya Ulinzi na Usalama "Brigedia Nyekundu(Red Brigade)"vya CHADEMA katika kanda na mikoa mbalimbali
![]()
Vikundi hivi ambavyo vimepewa mafunzo ya hali ya juu sana kuliko wakati mwingine wowote na vyenye uwezo mkubwa na mbinu za kisasa kabisa vinatambulika kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA ibara ya 7.6.4.(h) inayotangaza na kutambua uundwaji wa Kurugenzi ya Ulinzi na Usalama ya Chama ambayo Brigedia Nyekundu inatekeleza majukumu yake yaliyoanishwa ya Kulinda Mali,Viongozi na Maslahi ya Chama popote nchini.Pia katika Fasiri ya " B" ya kanuni za uendeshaji wa Chama
Katiba ya Zamani kabla ya toleo la Mwaka jana na Marekebisho yake ilisomeka katika ibara ya 7.7.5
Katiba hii imekaguliwa na kuthibitishwa na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini kuwa ni katiba halali na ambayo ibara zake zote hazijakiuka sheria wala katiba ya nchi na katiba hii ipo kwa msajili miaka yote
Msajili amethibitisha kuwa matakwa ya katiba ya nchi ibara ya 20.2(C) yamezingatiwa kwamba hakuna chama cha siasa bila kuathiri kifungu cha 1 na 4 kitakachotumia nguvu kama sera yake ya kufikia dhima yake katika lengo la kuchukua madaraka.
Hofu,Wivu na kelele zinatokana na wapinzani wetu kuona kwamba Mwaka huu hawataweza kuufanya uharamia wao waliokuwa wakiufanya miaka yote hasa wizi wa kura,kutisha wanachama na wafuasi wetu na hata wananchi wakati wa kujiandikisha na kupiga kura
Zilishaibuliwa Propaganda humu na Naibu katibu mkuu wa CCM Mhe.Mwigulu na kupotosha kwamba Red Brigade ni Sawa na "Brigate Rosse" ya Italia ambacho ni kikundi cha kiuhalifu.Alifanya kazi yake kwa nafasi yake nasi tulifanya kazi yetu tukampa changamoto atuletee katiba ya "Brigate Rosse" hadi leo hatujui alikotokomea au pengine labda anaisaka
Pia wananchi waliopotoshwa na kuanza kutulaumu na kuonyesha mashaka wana haki ya kufanya hivyo kwa kuwa hawajaambiwa kuwa kikundi hiki kinatambulika kisheria.Kwa kuwa sasa watafahamu kuwa kikundi hiki kinatambulika kikatiba na kisheria hawatakua wanatutendea haki ikiwa wataendelea kutulaumu au kukubali kupotoshwa
Sasa na Mimi Natoa Changamoto kwa Chama tawala CCM kilichounda serikali inayopaswa kusimamia Utawala bora wa Sheria nchini kitueleze Vikosi vyake vya "GREEN GUARD" vinatambulika kwa mujibu wa katiba ipi maana sijaona kipengele chochote kwenye katiba ya CCM kinachokitambua kikundi hicho na hivyo ofisi ya Msajili haikitambui ,hakitambuliki kisheria.Ninayo katiba yao hapa,Sikioni.
Kikosi chao Kina hadhi na sifa zote za kuitwa kikosi cha kihuni,cha kihalifu na kinachotekeleza majukumu yake kwa mrengo wa itikadi za kigaidi maana vikundi vyote vya kigaidi kama Interahamwe,Boko Haramu, Banyamulenge n.k vilianza hivi.Havitambuliki popote kisheria
Jeshi la Polisi nchini limekaa kimya. Hivi tunalipeleka wapi taifa hili?
Kama ambavyo "Brigate Rosse" ilivyojiendesha kihuni ndivyo "Green Guard" wanavyojiendesha na tukio la karibuni ni kumteka Mhe.Rose Kamili Mbunge wa Chadema kule Kalenga kwenye uchaguzi mdogo
Utekaji nyara umeshamiri nchini huku kikundi hiki kisichotambulika kisheria kikiachwa tu
Mauaji ya Albino yameshamiri na inawezekana unyama huu unafanywa na vikosi vya kukodishwa .Ni nani anadhibiti(Regulate) utendaji wa Kikosi hiki cha Green Guard?
Jeshi la Polisi kama halitaki kufanya kazi yake au linapoendelea kufanya kazi kwa upendeleo tutajilinda na pia tutawalinda wananchi wanyonge wanaonyimwa haki zao za kiraia kwa sababu chama tawala na jeshi la polisi kuruhusu uharamia huu
Kwa kuwa CHADEMA tunalenga kuunda Serikali yenye nidhamu,Kikundi chetu cha Ulinzi kipo kisheria na tumeonyesha dhamira ya dhati kabisa katika kufuata sheria tunapojilinda na pia tumelipa kipaumbele suala la usalama wa chama chetu kama tunavyolipa kipaumbele suala la usalama wa nchi yetu kwa serikali ijayo.
Wafuasi wetu wamekua wakiuawa na hata viongozi wetu na wengine kujeruhiwa na hata kukoswa koswa hata mahali ambapo Polisi wanajifanya kuweka ulinzi kumbe ni geresha
Hatima ya usalama wetu ipo mikononi Mwetu.Tutajilinda,tuna haki ya kisheria na kikatiba.Tupo Imara kuliko wakati Mwingine wowote
Wasalaam !
Aluta Continua,Victory Ascerta
Ben Saanane
MEANDU
Nimezoom ili nione jina la Nape bado sijaliona.Yamkini alikuwa anatumia jina lingine katika familia
Akiongea leo mkoani Dodoma katika mkutano wa hadhara,katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,bwana Nape Nnauye , amekielezea kikundi cha Red Brigade kama kikundi cha kigaidi kinachoweza kuvunja amani ya nchi na kuwataka wananchi kuwa macho na vikundi vya aina hiyo.
CHANZO:ITV
My take;
Hivi kati ya Red Brigade na watuhumiwa wa Escrow,nani anahatarisha amani ya nchi hii?!
He is more than kilaza!
Unisamehe tu uvumilivu umenishinda.Mkuu salary slip unaweza kujenga hoja zako bila kunitaja...!!??
Nitashukuru sana
Anapaswa kujibiwa kisawasawa anaonyesha ujinga usio kifani anapoongea ujinga kama huo ili kutisha wananchi
Kumbe FUTUHI huwa wanamuigiza yeye, mzee wa kukurupuka