Nape: CHADEMA wajiandae kuingia msituni

Nape: CHADEMA wajiandae kuingia msituni

nadhani watanzania tunahitaji kuwa makini, vikundi hivi inabidi kuvipiga vita kwa nguvu zetu zote. usisapoti kikundi kinachoweza kuhatarisha amani yako, ya familia yako, ya mtaa wako ya nchi yako eti kisa chama unachokichukia nacho kina kikundi.

cha msingi tuvikatae vikundi vyote vya kijeshi katika vyama vya siasa.

vikundi hivi inabidi tuvizuie kwa nguvu zetu zote bila kujali wakekereketwa wasiojua wanachokifanya kushabikia vikundi hivi wanafanya nini.

kama kweli tunaipenda amani ya nchi yetu tutafanya jitihada za kuzuia vikundi hivi bado vikiwa vichanga na tubadili sheria zetu ili chama chochote kisiruhusiwe kuunda kikundi cha jeshi.

nadhani watumishi wa majeshi yetu hawaruhusiwi kujiunga katika vyama inabidi tujiulize tulikuwa na lengo gani kwa kuweka jambo kama hilo sasa vyama vinaunda majeshi tumenyamaza na tunawasikiliza wendawazimu wanaoshabikia.

lakini jambo pia kwa vyama vya siasa pengine visitumie chokochoko zinazohatarisha uasalama wa nchi kama mtaji wa kisiasa. hapa ni kutafuta kubishana tu ambako katika kubishana hakuna anayekubali kushindwa ili apoteze kisiasa na hilo linakuwa linatupeleka pabaya. kila chama kijitafakari kifanye maamuzi ya busara kuondokana na mchezo huu mchafu.

kimsingi mimi ningekuwa ni kiongozi wa nchi kama vyama vya siasa visingeona busara kuondoka katika mwelekeo huu kwanza ningetumia mamlaka niliyopewa kuviua vyombo hivyo na kuweka sheria za kuzuia visije kuibuka tena.

lakini katika kuviua vyombo hivyo haitakiwi kutumia njia mbazo zitawafanya wahusika kukimbilia msituni moja kwa moja na hivyo badala ya kutibu tukajikuta tunaongeza kasi ya ugonjwa.

jambo hili likielezwa kwa watanzania najua walio wengi wataelewa ingawa wendawazimu ambao upeo wao wa kuona mbele unaishia kwenye kiganja cha mikono yao hawawezi kukosekana ambao watalaumu na kwao kuona hasara mpaka zimewafikia. hatuwezi kutumia busara hiyo mpaka hatari zimefika kwenye viganja vyetu ndio tuzibaini kwa maana kutakuwa hakuna la kufanya kuziepuka balli kukabiliana nazo kwa njia mbayo zitatuathiri.

VYAMA VYA SIASA KUUNDA MAKUNDI YA KIJESHI NI HATARI KWA USALAMA WA NCHI YETU
 
Wewe siasa zako ni Jamiiforums.

Hufahamu hata kushika mic kwenye mkutano wa kisiasa wa hadhara achilia mbali kuongea na kueleweka.

Pamoja na kupiga kelele kila sekunde hapa Jamiiforums, Uenyekiti wa Bavicha uliota mbawa.

Tisha toto ya kwenda mahakamani ikaishia kwenye mitandao.

Ujumbe wa Kamati Kuu ukaishia kwenye makaratasi.

Kwa sasa unasubiri hisani ya Katibu Mkuu wa CHADEMA.

Mkuu, kumkosoa Nape haimaanishi hatumtakii mema, kwanza walioko hapa wanavipato vyao na hawana sababu ya kulilia fadhila, tunataka ccm wenye uwezo wa kutawala na kama itashindwa basi kiwe chama cha upinzani chenye nguvu vilevile ili chama tawala kisejefanya madudu yaleyale ya ccm.
 
Wewe kila siku unawadanganya wanaJf kuwa ni kiongozi wa CCM Makao Makuu.

Sasa unawaomba kina nani wampumzishe wakati wewe ndiyo unatakiwa umpumzishe?.

Au umesahau kama wewe ni kiongozi wa CCM makao Makuu.

Vijana wa BAVICHA mnafurahisha sana.

Unakuja kwa unafiki wa kutoa ushauri baada ya kupata kipigo cha hoja.
MwanaDiwani,unajidhalilisha. Acha kunifuatilia mimi kijana.Ninakuheshimu lakini huniwezi. Endeleeni na ziara na Katibu Mkuu Kinana. Kazi yako ni hiyo ya kuripoti kinachotokea.Haumo kwenye wajenzi wa hoja.Kila la heri huko ndugu yangu MwanaDiwani

Mzee Tupatupa
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, kumkosoa Nape haimaanishi hatumtakii mema, kwanza walioko hapa wanavipato vyao na hawana sababu ya kulilia fadhila, tunataka ccm wenye uwezo wa kutawala na kama itashindwa basi kiwe chama cha upinzani chenye nguvu vilevile ili chama tawala kisejefanya madudu yaleyale ya ccm.

Ndugu,

Nani amesema kumkosoa kiongozi wa CCM ni kosa?.

Kosa ni kumkosoa kiongozi yoyote wa CCM bila hoja mbadala huku anayekosoa amejivika uanaCCM wakati anaeleweka ni BAVICHA.
 
Kama Red Brigade ni vikundi vya kigaidi na serikali haichukui hatua basi serikali Hii ni dhaifu sana ijiuzulu tu!
 
Ni kweli naunga mkono hoja hii na nitatoa sababu kama ifuatavyo
 
Siasa za ndugu yetu Nape siku hizi hazina mashiko kwa waliomfaham kijana huyu hapana shaka sasa ameishiwa hoja na ameshindwa kufahamu kua CCM ndo inatakiwa ieleze sera na utekelezaji wa Ilani yake lakini anageuka kua msemaji na Mwenezi wa Chadema kwani katika saikolojia inaaminiwa kua unapomsema vibaya mtu fulani kwa muda mwingi basi ndipo unawafanya watu wamfaham na kumfuatilia na siku akikutana nao yeye atatumia lugha rahisi kujitetea kwamba naonewa , na watu wale watamwelewa sana Nape kuisema chadema vibaya ni kuieneza bila yeye kujua kwa kua na uelewa usiokua mkubwa juu ya saikolojia hii ambayo ndio hii hii imewafanya wampe nguvu Lowassa na watu wengi sasa kumfaham na kua na nguvu kubwa bila wao kujua.
 
Kwenye msiba wa RIP Komba nilimsikia Nape akimtaja Marehemu Baba yake kama Mzee Moses jina ki kikristo.Nakumbuka kuhudhuria mazishi ya Mzee Mnauye yaliyosimamiwa na Mzee Makamba na yalifanyika kiislam.Mimi nina maswali mengi sana mojawapo ni kwa nini Nape halipi Fadhila kwa January kwa vile familia yao ilimzika baba yake??Maswali mengine kwa vile mnayajuwa yatoleeni majibu.
 
Nape yuko sahihi kabisa.

Naifananisha RB na Mungiki.

Watu wenye usaha kichwani badala ya ubongo hamna nafasi tena ktk dunia hii... Leo unaunga mkono Nape lile gwaride la kijeshi maji maji mbele ya amiri jeshi mkuu lilikuwa lanani? Hakuna mwenye hati miliki ya nchi hii kima wewe unatia kinyaa kwa uwezo wako finyu wakufikiri...
 

Attachments

  • 1425626799750.jpg
    1425626799750.jpg
    85.6 KB · Views: 118
Kwa mfano leo hii Nape akiongea na intellectuals atawaeleza nini juu ya Kagoda, Mereremeta, NBC, EPA, RICHMOND, ESCROW ambapo katika mambo hayo yote wao kama CCM walikua wa kwanza kupinga lakini kwa juhudi za wanausalama ambao hua ni wazalendo na walioupande wa wananchi nao husaidia kudakwa kwa shahidi mbalimbali na hivo baadae wateule wao kua hatiani hapo utasema wako upande wa wananchi au upande gani?
 
Nape tangu apewe hiyo nafasi amekuwa katibu mwenezi kivuli wa chadema
 
Salaryslip,
Kama unavyojiita,unaandika hoja kuwa Redbrigarde ni kikundi cha ugaidi nataka utuambie bila kupepesa macho,
* kwa nini ccm,unapofika uchaguzi huwa inachukua vijana kila mtaa/ kijiji/ kitongoji kuwapeleka mafunzo ya siri kwenye kambi za siri?
* hivi kwa kuwa ccm inaserikali inaweza zima maisha na mfumo uliouasisi mwenyewe?
* green guarde ilianzishwa kwa malengo gani?
* chipukizi inayofunzwa ukakamavu,mazoezi ya kujilinda,huwa wanatumia yafanye nni
Ccm imepoteza Dira √\ by DR.HORACE KOLIMBA ( late)
 
Wewe kila siku unawadanganya wanaJf kuwa ni kiongozi wa CCM Makao Makuu.

Sasa unawaomba kina nani wampumzishe wakati wewe ndiyo unatakiwa umpumzishe?.

Au umesahau kama wewe ni kiongozi wa CCM makao Makuu.

Vijana wa BAVICHA mnafurahisha sana.

Unakuja kwa unafiki wa kutoa ushauri baada ya kupata kipigo cha hoja.

kama kachoka tusiseme nape ndiye ameiua ccm kwa kas ya ajabu mku mwanadiwani
 
Niombe samahani Salaryslip

Hoja hiyo ni ya Nape Nnauye mtoto wa jrMoses Nnauye ambao wameamua kupeana vyeo,atujibu hoja hiyo
 
Kauli za hovyo kama hizi za Nape kiongozi wa juu CCM ndiyo zinaipunguzia kura chama chake kila uchaguzi

Red Brigade ni magaidi lkn Green Guard yao ni watakatifu?Nape una akili mbovu mno
 
Nape wa kutaka kuhamia Chadema na Nape wa CCJ ni tofauti na Nape waleo ambae hutukana hovyo vyama pinzani kwa kutaka kuvuruga amani ya nchi akisahau chama chake ndicho chenye Dola na polisi wanaua Raia bila sababu, Rushwa kila idara, mahusiano na majirani wa Tanzania hayaeleweki vizuri hadi leo, mfumuko wa bei za bidhaa, kushuka kwa thamani ya shilingi, sera za kiuchumi zisizo na tija kwa taifa, kupanda kwa deni la taifa, kushindwa kudhibiti madawa ya kulevya na kufanya taifa kua la mateja kila kukicha wanaongezeka na matatizo mengine mengi hawezi kuyajibu wala serikali yake haina ufumbuzi na matatizo hayo angejikita kuangalia hayo angeeneza chama chake vizuri
 
Back
Top Bottom