Nape: CHADEMA wajiandae kuingia msituni

Nape: CHADEMA wajiandae kuingia msituni

Akiongea leo mkoani Dodoma katika mkutano wa hadhara,katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,bwana Nape Nnauye , amekielezea kikundi cha Red Brigade kama kikundi cha kigaidi kinachoweza kuvunja amani ya nchi na kuwataka wananchi kuwa macho na vikundi vya aina hiyo.

CHANZO:ITV

My take;
Hivi kati ya Red Brigade na watuhumiwa wa Escrow,nani anahatarisha amani ya nchi hii?!

He is more than kilaza!

Katibu wa uenezi na propaganda.....ulitaka aseme ukweli?
 
ha ha ha thread zako zinanifurahisha sana, zimejaa kila aina ya unafiki, sijui ulisomea wapi
 
Kwa kiwango cha Division IV ya point 29 katika mtihani wa kidato cha Nne aliyoipata Nape Nnauye hawezi kuwa na uwezo wa kufanya hicho unachotarajia Mzee Tupatupa.

Katika hili wala siwezi kumlaumu kwakuwa hicho ndio kipeo chake cha uelewa na hata ccm wamfanyeje hawezi kufanya zaidi ya hapo kwakuwa akili hiyo hana. Apeche alolo...
 
Last edited by a moderator:
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM-Taifa, Nape Nnauye amechoka. Amechoka kimwili,kiakili,kimaneno na kimatendo. Kila uchao na kila apitapo,Nape anasema yale yale na kwa namna ile ile. Sasa Nape ameambatana na Katibu Mkuu wa CCM,Kanali Mstaafu Abdurahman Kinana huko Dodoma. Nape ana ngekewa ya kupewa jukwaa na kuhutubia. Viongozi wa kitaifa waamuamini na kumpa nafasi.

Nape amechoka.Uchovu wake sasa u wazi kabisa. Anarudiarudia yale yale palepale na kwingineko.Yeye ni CHADEMA tuuuuuuuu...basi.Hana hoja za haja za kuwaambia wananchi na kuiuza vyema Ilani yetu ya CCM ya 2010-2015. Kuonesha Ilani ilivyotekelezwa kwa vitendo na vitengo kumemshinda Nape. Nape anang'ang'ania ugaidi,utapeli wa CHADEMA na mgogoro wa CHADEMA.

Nape habadili santuri. Hana jipya.Hapaswi kuendelea kupewa jukwaa na kuendelea kuwaboa na kuwakera wananchi. Apumzishwe. Kurudiarudia maneno na matendo ni uchovu wa dhahiri kwa Nape Nnauye. Nafasi adhimu anayopewa Nape apewe mwingne chamani. Kama vijana tunao wengi tu!


Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Ukweli yeye kama katibu mwenezi alitakiwa atengeneze mikakati ya ndani ya chama itakayoiwezesha ccm kupata ushindi badala ya kuleta porojo, nikweli anaongea yaleyale kila siku wakati chama kinazidi kuporomoka, katika siasa za ushindani anatakiwa kilasiku aje na mbinu mpya na bora zaidi za kukijenga chama.

Anaposema redbrigadi magaidi anasahau hao redbrigadi wanaishi katika jamii hiyohiyo anayoihutubia na wanawajua zaidi kuliko hata yeye anavyowajua.
 
Last edited by a moderator:
magaidi mnakazi nape kawagusa nape kapiga msumari wa moto.

Kapiga au kajipiga? Hizo ndio akili kama za Ngeleja, kwamba nimepewa hela haramu lakini sio peke yangu ila na wengine akidhani huo ni utetezi wenye msaada. Nape anazungumzia vikundi hivyo wakati msajili wa vyama kaisha sema Red Brigade iko kwenye katiba ya Chadema hivyo iko kisheria lakini katiba ya CCM haisemi chochote kuhusu Green guard hivyo hicho ni kikundi cha kihuni tuu.
 
Wewe kila siku unawadanganya wanaJf kuwa ni kiongozi wa CCM Makao Makuu.

Sasa unawaomba kina nani wampumzishe wakati wewe ndiyo unatakiwa umpumzishe?.

Au umesahau kama wewe ni kiongozi wa CCM makao Makuu.

Vijana wa BAVICHA mnafurahisha sana.

Unakuja kwa unafiki wa kutoa ushauri baada ya kupata kipigo cha hoja.
 
Kwa kiwango cha Division IV ya point 29 katika mtihani wa kidato cha Nne aliyoipata Nape Nnauye hawezi kuwa na uwezo wa kufanya hicho unachotarajia Mzee Tupatupa.

Katika hili wala siwezi kumlaumu kwakuwa hicho ndio kipeo chake cha uelewa na hata ccm wamfanyeje hawezi kufanya zaidi ya hapo kwakuwa akili hiyo hana. Apeche alolo...

Mkuu Mwita Maranya naona umefufuka kuongeza nguvu katika homa ya October.
 
Last edited by a moderator:
hili tunalisema hata hapa jf...hoja za miccm ni zile zile tu..ugaidi, ukabila na udini
 
Wewe kila siku unawadanganya wanaJf kuwa ni kiongozi wa CCM Makao Makuu.

Sasa unawaomba kina nani wampumzishe wakati wewe ndiyo unatakiwa umpumzishe?.

Au umesahau kama wewe ni kiongozi wa CCM makao Makuu.

Vijana wa BAVICHA mnafurahisha sana.

Unakuja kwa unafiki wa kutoa ushauri baada ya kupata kipigo cha hoja.

Naona boss mwenyewe umeamua kuja ili kumhami kijana wenu.

Mbona mbunge wa Kongwa Job Ndugai hatujamuona jana katika mapokezi na ziara ya Kinana Mkoani Dodoma? au hizi taarifa ya kwamba mmemwakyembe ni za kweli?
 
Hawezi kujibu hoja zozote zaidi ya kuumiza masikio ya wananchi kwa kelele kwenye mic tu

Wewe siasa zako ni Jamiiforums.

Hufahamu hata kushika mic kwenye mkutano wa kisiasa wa hadhara achilia mbali kuongea na kueleweka.

Pamoja na kupiga kelele kila sekunde hapa Jamiiforums, Uenyekiti wa Bavicha uliota mbawa.

Tisha toto ya kwenda mahakamani ikaishia kwenye mitandao.

Ujumbe wa Kamati Kuu ukaishia kwenye makaratasi.

Kwa sasa unasubiri hisani ya Katibu Mkuu wa CHADEMA.
 
Nape hana kitu cha maana zaidi ya kukoroma jukwaani kama mamba anaye hami mzoga Ili asinyang'anywe na wenzake.
 
Mimi nikimwonaga jamaa huyu anaanza kuzungumza tu huwa nahama station. Huwa hakuna cha kujifunza au kitu kipya toka kwake. Amekalia uzandiki tu.
 
Naona boss mwenyewe umeamua kuja ili kumhami kijana wenu.

Mbona mbunge wa Kongwa Job Ndugai hatujamuona jana katika mapokezi na ziara ya Kinana Mkoani Dodoma? au hizi taarifa ya kwamba mmemwakyembe ni za kweli?

Ndugu,

Subiri timu ya Katibu Mkuu itakapotua katika Jimbo la Kongwa kama unataka kumuona Job Ndugai.

Kwa sasa timu bado iko Mpwapwa vijijini.

Karibu Mpwapwa vijijini.
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM-Taifa, Nape Nnauye amechoka. Amechoka kimwili,kiakili,kimaneno na kimatendo. Kila uchao na kila apitapo,Nape anasema yale yale na kwa namna ile ile. Sasa Nape ameambatana na Katibu Mkuu wa CCM,Kanali Mstaafu Abdurahman Kinana huko Dodoma. Nape ana ngekewa ya kupewa jukwaa na kuhutubia. Viongozi wa kitaifa waamuamini na kumpa nafasi.

Nape amechoka.Uchovu wake sasa u wazi kabisa. Anarudiarudia yale yale palepale na kwingineko.Yeye ni CHADEMA tuuuuuuuu...basi.Hana hoja za haja za kuwaambia wananchi na kuiuza vyema Ilani yetu ya CCM ya 2010-2015. Kuonesha Ilani ilivyotekelezwa kwa vitendo na vitengo kumemshinda Nape. Nape anang'ang'ania ugaidi,utapeli wa CHADEMA na mgogoro wa CHADEMA.

Nape habadili santuri. Hana jipya.Hapaswi kuendelea kupewa jukwaa na kuendelea kuwaboa na kuwakera wananchi. Apumzishwe. Kurudiarudia maneno na matendo ni uchovu wa dhahiri kwa Nape Nnauye. Nafasi adhimu anayopewa Nape apewe mwingne chamani. Kama vijana tunao wengi tu!


Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Nape akipumzishwa ukatibu enezi anaweza akaingia msituni!
 
Wewe siasa zako ni Jamiiforums.

Hufahamu hata kushika mic kwenye mkutano wa kisiasa wa hadhara achilia mbali kuongea na kueleweka.

Uenyekiti wa Bavicha uliota mbawa.

Tisha toto ya kwenda mahakamani ikaishia kwenye mitandao.

Ujumbe wa Kamati Kuu ukaishia kwenye makaratasi.

Kwa sasa unasubiri hisani ya Katibu Mkuu wa CHADEMA.

Ha ha ha mkuu umenena kweli, sijawahi kumuona ben akihutubia hata dakika moja, labda kwa sababu ana kugugumizi, ndio maana lema anataka kumfukuza kwenye chama
 
Back
Top Bottom