Nape: CHADEMA iwajibike matukio ya mauaji

Kuna taarifa kuwa askari alie muuwa mwandishi wa habari amekamatwa.sasa km anajuwa kuwa cdm ndio wanaowaua wananchi kwa risasi na mabomu huyu askari wamemkamata kwa kosa gani?.
 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) imekitaka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwajibika kutokana na kuwepo kwa matukio ya watu kupoteza maisha yanayosababishwa na maandamano ambayo yamekuwa yakifanywa na wafuasi wake. Kauli hiyo imetolewa jana mjini hapa na Katibu wa Halmashauri
Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, wakati akizungumza na waandishi wa habari.
“Chadema wana kila sababu ya kuwajibika, kwa sababu matukio haya ya mauaji yamekuwa yakitokea kwenye operesheni za mikutano yao na matukio ya aina hii kutokea katika kazi za chama cha siasa ni aibu, hivyo viongozi wa kisiasa wanaokutwa na matukio hayo ni lazima wawajibike kwa umma, lakini matukio haya yamekuwa yakitokea bila wao kuwajibika,” alisema Nape na kuongeza:
“Inapotokea shughuli za chama chako zinasababisha kupotea kwa maisha ya watu kila unapozifanya na bado usitake kuwajibika, inahitaji roho ngumu na ujasiri wa aina yake.”
Alisema CCM inaungana na wanaCCM na wananchi wote kulaani mauaji ya aliyekuwa Mwandishi wa Channel Ten mkoani Iringa, Daudi Mwangosi aliyeuawa Septemba 2, mwaka huu.
“Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa za kifo hicho na kujeruhiwa kwa askari hao. CCM inachukua nafasi hii kutoa pole kwa wafiwa, wanahabari nchini na wote walioguswa na msiba huu kwa namna moja au nyingine,” alisema Nape.
Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi alisema CCM imetoa mwito kwa vyombo na tume mbalimbali zilizoundwa
kuchunguza kwa umakini na weledi mauaji ya Mwangosi ili kubaini chanzo cha mauaji hayo pamoja na chanzo cha vurugu zilizotokea na mazingira ya kifo cha mwandishi huyo wa habari.
“Pamoja na mwito wetu wa kuchunguzwa suala hili kwa umakini na weledi mkubwa, pia tunatoa rai kwamba
uchunguzi huu ufanyike kwa kutumia muda mfupi ili ukweli uweze kubainika mapema na hatua zinazostahili ziweze kuchukuliwa haraka iwezekanavyo,” alisema Nape na kuongeza:
“Vilevile CCM inasikitishwa sana na mfululizo wa matukio ya watu kupoteza maisha au kujeruhiwa katika mikutano na operesheni mbalimbali zinazoendeshwa na Chadema nchini hasa zile zilizofanyika kwa kukaidi amri halali za vyombovya ulinzi na usalama.”
Aliyataja baadhi ya matukio hayo kuwa ni la kuuawa kwa kada wa CCM mkoani Singida, kuuawa kwa Ali Hassan mjini Morogoro, kuuawa kwa Mwangosi, kujeruhiwa kwa askari polisi Iringa na matukio mengine yalitokea wakati viongozi wa Chadema wakiendesha operesheni zao mbalimbali nchini.
Nape alisema matukio hayo si mazuri kutokea kwenye shughuli za chama cha siasa kwa madai ni aibu kwa
wanachama wake na wananchi kwa ujumla na hivyo kupoteza sifa ya kuitwa chama chema cha siasa.(Source: Habari Leo 6th september 2012)

Kweli nyani haoni kundule. Yahani CCM wameshindwa kuwajibika kwanza wenyewe kwenye ufisadi uliotupeleka masikini mpaka leo halafu anasema CDM iwajibike? Ni wangapi wamekufa kukosa huduma hospitali, njaa? Ni wangapi wameachwa na umasikini wa kupingukia ndani ya aridhi yao? Nani anawajibika hapo? Ndugu nape akatujibu kwanza maswali haya. Kama akina Nape wataendelea kuwa Viongozi wa CCM basi kuna hatari kubwa sana. Hii inafanya niwakumbuke sana kina Mangula. Yahani huyu nape ni hovyo kweli ndani ya CCM na ndo anatuharibia chama chetu lol
 
Hivi hiki kiumbe nape ni aina gani? Kwasababu namuona hayupo kwenye kundi la mamalia labda yeye na reptilia? Nimesema hv coz jamaa anaonyesha kama hayuko tz na hajui wa tz kiuelewa wamefikia wapi. Shame on u.
 
Kuna taarifa kuwa askari alie muuwa mwandishi wa habari amekamatwa.sasa km anajuwa kuwa cdm ndio wanaowaua wananchi kwa risasi na mabomu huyu askari wamemkamata kwa kosa gani?.
 
Imefika wakati viongozi wa Chadema wawajibike kwa vifo vinavyotokea katika maandamano yao kwa sababu wao ndio wanasababisha na wanakuwa wanafahamu kuwa mtu atafariki, Kifo cha Mwangosi Iringa kabla tukio halijatokea Mwandishi Francis Godwin alimuuliza Dr Slaa kwamba kwa nini wanaenda kufanya Mkutano wakati wamezuiliwa kufanya Mkutano Dr slaa alieleza Liwalo na Liwale na yuko tayari kupoteza Maisha ya Mtanzania yeyote ili kuimarisha Chama.
Hivi kwa nn Dr Slaa asiuzulu pamoja na Mwenyeki kama kweli wana nia ya dhati na Watanzania?
Kwa maneno aliyoyatoa ilikuwa ni lazima nguvu itumike kwa Sababu CDM Wakivunja Sheria wasiposhughulikiwa wanasema Serikali ya CCM dhaifu Sasa ili isiwe dhaifu lazima kila mmoja aheshimu sheria na anayevunja achukuliwe Hatua na ninamweleza IGP Na RPC Lazima muuendelee kulinda sheria kila mmoja aheshimu anayebisha ashughulikiwe...

Halafu Dr Alikuwepo Nyololo mbona alipoanzisha fujo tu hatukujua kaelekea wapi au ni Mkakati wa Chadema kuua watanzania wameagizwa na Wafadhili wao?

Kweli nimeamin kikao cha Chadema hakina Tofauti na kikao cha ukoo...Kikao cha Ukoo kinaweza kubadilika kuwa Kikao cha Chama
 
TAIFA LETU TULIPENDALO SAAANA LA TANZANIA HIVI SASA LIKO NJIANI KUANGAMIA SHAURI YA KUKOSA UONGOZI SIKIVU, ADILIFU NA WENYE HEKIMA

"Taifaa la Tanzania linaumwa tena linaugua ugonjwa wa hatari sana tangu uchaguzi wa Oktoba 2010, kufanyike juhudi za haraka kulitibu taifaa," alisikika miezi michahe akitoa hii kauli yenye hekima tele yule Mhe Mbuye wa Arusha alie likizoni Godless Lema.

Hata hivyo, ni wangapi ndani ya nchi hii walau waliweza kumuazima sikio na kutafakari ki-undani zaidi hii kauli???????????

Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete na maswahiba wake wanaoendelea kufilisi nchi hii kupitia Dowans, EPA na rundo la fedha za ki-shetani kwenye Benki Uswisi, wataendeleaa kuishi kwa matumaini ya ulinzi wa FFU mpaka lini?????????

Ama kweli Tanzania taifa langu linaangamia kwa kukosa uongozi wenye hekima na uadilifu.

Kaskazini, mashariki na kusini kuzunguka nje ya uzio wa Ikulu kuna idadi kubwa ya Askari FFU na vifaa vya kazi. Ni idadi kubwa kuliko siku zingine.

Upande wa baharini mahali ambapo ni eneo la kuegesha magari kukiwa na sherehe kubwa ikulu, kuna gari ya maji ya washawasha, defender nne na FFU wamebeba bunduki na mabomu ya machozi.
 
Nape unashindwa hata kuwasiliana na wenzako? Wenzako ndani ya CCM wameshaona kwamba huo mpango wa kuua watu katika kila mkutano wa CDM lil muupake CDM matope umeshindwa. Umeshindwa kwa sababu mauaji yaliyokwishafanyika yameshindwa kuhusishwa na CDM moja kwa moja kwa moja. Mfano wa yule mwandishi wa habari aitwaye Mwangosi aliuawa wakati hapakuwa hata na mkutano wa hadhara na aliuawa wakati hakuwa katika maandamano.

Tatizo lenu CCM hakuna hata mwenye kufikiri ndiyo maana hata maneno yenu mnayozungumza hata mtoto mdogo anaweza kuwashangaa. Hata kupanga mikakati ya kipropaganda yanahitaji kutumia akili siyo kutunga tu sentensi kama hizo za hapa juu.
 
Kwa kauli hii ya Nape naanza kuamini kauli za kuwa haya mauaji kwenye mikutano ya chadema yanapangwa na CCM, ili tu watupe lawama kwa chadema. Lakini wamechelewa sana mpango wao umestukiwa.

ushaona eeh!
 
View attachment 64236 images.jpg
 
Tatizo la watu wa CDM ni uhodari wa kutusi wengine wanapokuja na hoja wasizozipenda. Shame on u

mkuu nadhani hujui definition ya 'tusi'. Kikwete aliposema, 'wanaopata virusi vya UKIMWI ni viherehere vyao' hakutukana? Mwinyi aliposema huku akicheka, 'ukipenda kula vya wengine sharti na wewe uliwe' hakutukana?
 
Back
Top Bottom