Naona Kula Mgahawani ni nafuu kuliko kupika kwa mtu mmoja

Kupika simple sana na napenda sana sana Ila baada ya kupika na kula vyombo naosha baada ya wiki 3 mpaka mwez na mpaka nione kutu Labda ndo nashtuka au mpaka nzi wasuse na hujikuta nambulia kuvitupa nankununua tena

Karibu buan ndo maisha yetu
 
Wakuu,
Moja ya changamoto kubwa ninayokumbana nayo ni suala la kupika.

Baada ya Kula Mgahawani kwa muda mrefu, nikaona nianze mchakato wa kupika. Lakini nimegundua kuwa, Kupika chakula cha mtu mmoja ni Gharama kubwa kuliko kula mghahawani.

Mimi bajeti ya chakula cha mchana ni 3000 na jion hivyohivyo, hivyo jumla kuwa 6000 kwa siku.

Lkn nilipo anza kupika nikaona gharama ni zilezile mchanganuo ni kama ifuatavyo,

1. Mchele nusu 1000
2. Mboga za majani 500
3. Mafuta 500
4. Nyanya na vitunguu, hoho 1000
5. Nyama robo 1500
6. Nishati 500

Jumla inakua 5000

Najua wengine watasema vitu unanunua kwa jumla, lkn nimefanya hivyo na ukichukua hesabu zake ni kama hivyo tu.

Sasa hapo hujaweka usumbufu wa kupika, kuosha viombo, kumwagamwaga maji, na muda pia.
Pili kupika kunahitaji ufuatiliaji, mana nishaunguza sana tu.

Je nyie ambao ni mabachela mnaweza save vipi gharama kwa kupika na kuepuka kula mghahawani?

Labda mnaweza nishawishi tena nirudi jikoni mana nilipika wiki mbili nikaacha mpk vitu vikakaribia kuharibika ikabidi nivigawe tu.
Sure mkuu ila migahawani wanatulisha sana mauchafu, mara maji ya mchele waoshee qu.mer na maujinga ujinga kibao tu ila kwa issue ya gharama ni nafuu sana kwa walio single kuliko kupika mwenyewe.
 
Asee kupika chakula cha mtuu mmoja inahitaji moyo. Though kuna changamoto lakini ni bora kujipikia mwenyewe kuliko kula kwenye mgahawa. Vyakula vya mgahawa havishibishi na havna flavor..kama umezoea kula nyumbani utapata tabu na vyakula vya mgahawa.
 
Kula mgahawani ni nafuu mno kwa bachelor kama mimi..unaokoa muda pamoja na gharama pamoja na mausumbufu mengine ya ajabu ajabu yanayo husiana na kupika
 
Wakuu,
Moja ya changamoto kubwa ninayokumbana nayo ni suala la kupika.

Baada ya Kula Mgahawani kwa muda mrefu, nikaona nianze mchakato wa kupika. Lakini nimegundua kuwa, Kupika chakula cha mtu mmoja ni Gharama kubwa kuliko kula mghahawani.

Mimi bajeti ya chakula cha mchana ni 3000 na jion hivyohivyo, hivyo jumla kuwa 6000 kwa siku.

Lkn nilipo anza kupika nikaona gharama ni zilezile mchanganuo ni kama ifuatavyo,

1. Mchele nusu 1000
2. Mboga za majani 500
3. Mafuta 500
4. Nyanya na vitunguu, hoho 1000
5. Nyama robo 1500
6. Nishati 500

Jumla inakua 5000

Najua wengine watasema vitu unanunua kwa jumla, lkn nimefanya hivyo na ukichukua hesabu zake ni kama hivyo tu.

Sasa hapo hujaweka usumbufu wa kupika, kuosha viombo, kumwagamwaga maji, na muda pia.
Pili kupika kunahitaji ufuatiliaji, mana nishaunguza sana tu.

Je nyie ambao ni mabachela mnaweza save vipi gharama kwa kupika na kuepuka kula mghahawani?

Labda mnaweza nishawishi tena nirudi jikoni mana nilipika wiki mbili nikaacha mpk vitu vikakaribia kuharibika ikabidi nivigawe tu.
Kusevu gharama ni pamoja na kula vitu usivyopenda kama ugali na misumari (dagaa). Ila kama utataka kula pilau ni aheri ule kibandani tu.
 
Kwenye maisha ya ubachela wanasema kupika sio kazi kuosha vyombo. Endelea kula magengeni au vuta jiko mkuu
Hio ndio biashara ambayo inanifanya nishindwe kupika yani. Kupika ni raha sana ila ingekuwa kuna namna ukishashiba vyombo vinajiosha ingekuwa raha sana. Mchina atufyatulie mashine hio tafadhali. Kupika sio kazi, ishu kuosha vyombo yani ndio balaa!!!
 
Back
Top Bottom