Kwa Tanzania; Kama Mwanamke hajawahi fika Ukanda wa Pwani ni hakika Hajui Kupika chakula kitamu

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,876
Kwema Wakuu!

Kuna watu watabisha Kwa ubishi wao tuu lakini kimsingi na kitaalumuna unapozungumzia mapishi Kwa nchi yetu basi hapo utakuwa unazungumzia ukanda wa Pwani.
Kama unaishi maisha ya kawaida Kurudi ufukara na hujawahi kuishi Maeneo ya Pwani na hapa nazungumzia DAR es salaam, Pwani yenyewe, Tanga, Lindi, Mtwara, na Zanzibar basi kaa ukijua hujawahi Kula chakula kitamu.

Na Kama Mwanamke hajawahi fika na kuishi Pwani basi ni hakika hajui Kupika chakula kitamu.

Wanawake WA Pwani moja ya silaha zao nzito za Masafa mafupi na marefu mbali na kukata mauno pia Upishi WA chakula kitamu wameshindikana.

Kuanzia Chai, Andazi, chapati, wali, pilau, biriani, Makande, Makange, Ndizo, maharage, kunde, mtori, n.k. vyakula hivyo Kama hujawahi kupikiwa na Mwanamke wa Pwani basi jua hujui utamu wake.

Ukiona mtu yeyote anajua Kupika chakula Kwa nchi hii ya TANZANIA, jua Ujuzi huo ameupatia baada ya kuishi aidha ni DAR es salaam, au Pwani, au Tanga.

Kupika Kwa wanawake WA Pwani ni Sanaa, ni ufahari, ni Jadi Yao. Vikorombwezo bila ya bezo, wakiimba Kwa Dezo na michezo ya Ngoma chakula chenyewe kinageuka chocolate.

Mwanamke wa Pwani hahitaji kwenda kujifunza Hotelia ATI ili awe MPISHI mzuri, mapishi matamu kwao ni silaha.

Wengine chakula kitamu ni mpaka siku ya Harusi au sikukuu hasa huko Mikoani.
Ila ukanda wa Pwani kila siku chakula kitamu bila kujali bajeti ni ndogo kiasi gani.

Taikon Leo nipo kwenye Migahawa ya Waswahili huku, kuna watu wanapika bhana, utamu mpaka unafumba macho.

Ooh! Kalogwa! Sijui limbwata! Hivi chakula kitamu unafikiri mchezo!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Kama umeoa inaonekana mke wako hajui kupika chakula kitamu. Umekuja pwani umekula chakula kitamu umeanzisha uzi. Ila all in all msinipopoe wanawake wa wengi wa kichaga na waha hawajui kupika chakula kitamu.

Huwezi elewa vizuri ninachokisema Kama nchi hii haujazunguka
 
Wakati flani nikiwa safarini nairobi niliingia ktk mgahawa unaomilikiwa na mkenya wa bara(mkikuyu).

Chakula chao sikukipenda. nilimlalamikia sana mwenyeji wangu aliyenipeleka kwenye mgahawa ule.

Akaniambia niwe mpole, kesho atanipeleka kwenye mgahawa unaomilikiwa na mkenya wa pwani toka mombasa.

Basi siku ya pili tukaenda kwenye ule mgahawa, aisee nilikula biriani tamu san. jambo zuri zaidi wahudumu waliotuhudumia ni mabinti wazuri wanaozungumza kiswahili kitamu cha pwani.

Kwa siku zote nilizokaa pale, breakfast na lunch nilikuwa nakula kwenye ule mgahawa wa mtu pwani.
 
Hii ni kweli kabisa

Kanda ya ziwa ukiona mwanamke anajua kupika basi utakuta alishafika pwani.
Lakini wale ambao hawajawahi fika huko pwani hawajui kitu
Acha maneno yako wewe, huku kwetu kanda ya ziwa tuna vyakula vyetu vya asili yetu ambavyo wanawake wetu ni mahili sana kuvipika ukilinganisha na hao wa pwani. Mwandishi amebainisha aina ya vyakula ambavyo wapwani ni mahili hapo nimekubali kabisa lakini kwa vile vya asili ya ukanda kila kanda kwa asili yake inafanya vizuri.

Mfano ukipikiwa kande na mtoto wa kanda ya ziwa(hasa hasa usukumani) kiukweli "utajua hujui" kama uliwahi kula chakula hicho bila kusahau ugali, wa kwetu huku ni tofauti sana na wa huko pwani. Vile vile ukienda pande za Kagera ukapikiwa ndizi za asili yao kwa kweli ni tamu sana na mapishi yao ni ya tofauti sana ukilinganisha na mahali kwingine.

Naweza kuhitimisha kwa kusema kuwa uzuri wa mapishi ya vyakula mbalimbali hutegemea na asili ya chakula chenyewe ijapokuwa wenzetu wa pwani wanajua kutumia zaidi viungo katika mapishi yao kuliko mahali kwingine popote Tanzania hii.
 
Kwema Wakuu!

Kuna watu watabisha Kwa ubishi wao tuu lakini kimsingi na kitaalumuna unapozungumzia mapishi Kwa nchi yetu basi hapo utakuwa unazungumzia ukanda wa Pwani.
Kama unaishi maisha ya kawaida Kurudi ufukara na hujawahi kuishi Maeneo ya Pwani na hapa nazungumzia DAR es salaam, Pwani yenyewe, Tanga, Lindi, Mtwara, na Zanzibar basi kaa ukijua hujawahi Kula chakula kitamu.

Na Kama Mwanamke hajawahi fika na kuishi Pwani basi ni hakika hajui Kupika chakula kitamu.

Wanawake WA Pwani moja ya silaha zao nzito za Masafa mafupi na marefu mbali na kukata mauno pia Upishi WA chakula kitamu wameshindikana.

Kuanzia Chai, Andazi, chapati, wali, pilau, biriani, Makande, Makange, Ndizo, maharage, kunde, mtori, n.k. vyakula hivyo Kama hujawahi kupikiwa na Mwanamke wa Pwani basi jua hujui utamu wake.

Ukiona mtu yeyote anajua Kupika chakula Kwa nchi hii ya TANZANIA, jua Ujuzi huo ameupatia baada ya kuishi aidha ni DAR es salaam, au Pwani, au Tanga.

Kupika Kwa wanawake WA Pwani ni Sanaa, ni ufahari, ni Jadi Yao. Vikorombwezo bila ya bezo, wakiimba Kwa Dezo na michezo ya Ngoma chakula chenyewe kinageuka chocolate.

Mwanamke wa Pwani hahitaji kwenda kujifunza Hotelia ATI ili awe MPISHI mzuri, mapishi matamu kwao ni silaha.

Wengine chakula kitamu ni mpaka siku ya Harusi au sikukuu hasa huko Mikoani.
Ila ukanda wa Pwani kila siku chakula kitamu bila kujali bajeti ni ndogo kiasi gani.

Taikon Leo nipo kwenye Migahawa ya Waswahili huku, kuna watu wanapika bhana, utamu mpaka unafumba macho.

Ooh! Kalogwa! Sijui limbwata! Hivi chakula kitamu unafikiri mchezo!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Ufafanuzi zaidi huu hapa.


Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
wakati flani nikiwa safarini nairobi niliingia ktk mgahawa unaomilikiwa na mkenya wa bara(mkikuyu).

chakula chao sikukipenda. nilimlalamikia sana mwenyeji wangu aliyenipeleka kwenye mgahawa ule...

Utaambiwa Chai.

Kuna watu hawapendi ukweli pale wengine wanaposifiwa
 
Back
Top Bottom