Mimi ni binti wa miaka 23 sasa. Nimekuwa kwenye mahusiano na kijana wa miaka 32. Mahusiano yetu ni ya mbali.
Yeye yupo Dar ila mimi nipo mkoa wa mbali sana ambapo kukutatana kwetu ni pale tu inapotokea likizo toka chuo kurudi nyumbani. Hapo tunaweza kuonana.
Tumeanza mahusiano huu ni mwaka wa tatu. Mahusiano yetu yalikuwa kwenye simu, kupigiana na kutext. Kiukweli mwenzangu ana tabia nyingi mbaya ambazo nimezigundua ingawa simjui vema. Nakumbuka nikiwa mwaka wa kwanza kipindi cha likizo fupi, niliwahi safiri na kwenda kwa mwenzangu. Amepanga gheto, na anafanya kazi.
Hofu yangu ni hii. Mwanzo nilimpenda na kumuamini sana. Ingawa mwenzangu anapenda sana starehe na anafanya akidai kuwa sababu mimi nipo mbali naye. Jambo ambalo kidogo sasa linanipa mashaka kama ni kweli ataweza badilika ama hapa najifanganya. Maana kiukweli mimi sipendi kabisa lifestyle yake. Hawezi hata kunitumia pesa ya matumizi hadi tugombane. Na pesa kubwa anayotuma ni 15000 hiyo ni kubwa sana.
Jambo la pili na kubwa linalonitia mashaka ni kwamba nimegundua kuwa mara kadhaa amekuwa na mahusiano na mwanamke kwa muda mrefu sana. Miaka 9. Wanaachana na kurudiana. Na kuachana kwao hakufiki mwezi. Wapo mkoa mmoja. Na huyo mwanamke wana umri sawa ingawa mwenzangu amemzidi kidogo.
Mwanzo mwenzangu alikataa. Lakini baada ya kupata ushahidi, aliweka wazi na kuomba msamaha. Lakini amekuwa mara kwa mara akirudia kosa hilo. Kila mara nagundua kwa ushahidi kuwa wamerudiana. Jambo ambalo mimi linanikwaza sana.
Hiki kitu kimenifanya niwe addicted kumfuatilia yule mwanamke anafanya nini, yuko wapi na nani. Yaan sina raha hata kidogo. Najikuta badala ya kuongelea future mara nyingi namuongelea huyu mwanamke.
Kijana huyu ameapa kuwa ananipenda na amenichagua mimi ila yule mwanamke anamnganda. Lakini najiuliza kama kweli angekuwa anagandwa, ina maana yeye hana uwezo wa kujicontrol juu ya mwanamke huyo? Tena mbaya zaidi ni mwanamke ambaye wamesaidiana sana kabla ya mwenzangu kupata kazi. Hadi sasa hata ikitokea shida yoyote wataongea na kusolve.
Kwenye starehe mara kwa mara nashuhudia picha wakiwa wamepiga wanafurahi pamoja. Mwenzangu nikimuuliza ananiambia anajilazimisha tu hapo. Na amenitamkia ndoa.
Sielewi jamani. Ni kweli hapa ni pa kukaa? Na kama kuna ndoa inawezekana huyu mwanaume anafanya haya kwa kuwa mimi nipo mbali au ni tamaa zake tu? Mwaka huu namaliza elimu yangu na ninategemea kuwa karibu na kijana huyu kuanza mahusiano ya karibu. Naombeni mnisaidie kwa ushauri ndugu yenu. Kama ninaangamia ama la.
Shukrani.
Yeye yupo Dar ila mimi nipo mkoa wa mbali sana ambapo kukutatana kwetu ni pale tu inapotokea likizo toka chuo kurudi nyumbani. Hapo tunaweza kuonana.
Tumeanza mahusiano huu ni mwaka wa tatu. Mahusiano yetu yalikuwa kwenye simu, kupigiana na kutext. Kiukweli mwenzangu ana tabia nyingi mbaya ambazo nimezigundua ingawa simjui vema. Nakumbuka nikiwa mwaka wa kwanza kipindi cha likizo fupi, niliwahi safiri na kwenda kwa mwenzangu. Amepanga gheto, na anafanya kazi.
Hofu yangu ni hii. Mwanzo nilimpenda na kumuamini sana. Ingawa mwenzangu anapenda sana starehe na anafanya akidai kuwa sababu mimi nipo mbali naye. Jambo ambalo kidogo sasa linanipa mashaka kama ni kweli ataweza badilika ama hapa najifanganya. Maana kiukweli mimi sipendi kabisa lifestyle yake. Hawezi hata kunitumia pesa ya matumizi hadi tugombane. Na pesa kubwa anayotuma ni 15000 hiyo ni kubwa sana.
Jambo la pili na kubwa linalonitia mashaka ni kwamba nimegundua kuwa mara kadhaa amekuwa na mahusiano na mwanamke kwa muda mrefu sana. Miaka 9. Wanaachana na kurudiana. Na kuachana kwao hakufiki mwezi. Wapo mkoa mmoja. Na huyo mwanamke wana umri sawa ingawa mwenzangu amemzidi kidogo.
Mwanzo mwenzangu alikataa. Lakini baada ya kupata ushahidi, aliweka wazi na kuomba msamaha. Lakini amekuwa mara kwa mara akirudia kosa hilo. Kila mara nagundua kwa ushahidi kuwa wamerudiana. Jambo ambalo mimi linanikwaza sana.
Hiki kitu kimenifanya niwe addicted kumfuatilia yule mwanamke anafanya nini, yuko wapi na nani. Yaan sina raha hata kidogo. Najikuta badala ya kuongelea future mara nyingi namuongelea huyu mwanamke.
Kijana huyu ameapa kuwa ananipenda na amenichagua mimi ila yule mwanamke anamnganda. Lakini najiuliza kama kweli angekuwa anagandwa, ina maana yeye hana uwezo wa kujicontrol juu ya mwanamke huyo? Tena mbaya zaidi ni mwanamke ambaye wamesaidiana sana kabla ya mwenzangu kupata kazi. Hadi sasa hata ikitokea shida yoyote wataongea na kusolve.
Kwenye starehe mara kwa mara nashuhudia picha wakiwa wamepiga wanafurahi pamoja. Mwenzangu nikimuuliza ananiambia anajilazimisha tu hapo. Na amenitamkia ndoa.
Sielewi jamani. Ni kweli hapa ni pa kukaa? Na kama kuna ndoa inawezekana huyu mwanaume anafanya haya kwa kuwa mimi nipo mbali au ni tamaa zake tu? Mwaka huu namaliza elimu yangu na ninategemea kuwa karibu na kijana huyu kuanza mahusiano ya karibu. Naombeni mnisaidie kwa ushauri ndugu yenu. Kama ninaangamia ama la.
Shukrani.