Naombeni ushauri nimemfumania shemeji yangu

Habari Wana jamvi,

Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu.

Nina rafiki yangu ambaye ni Kama ndugu yangu kwa jinsi tunavyoishi na kusaidiana once changamoto za kimaisha zinapo arise.

Nimeishi vizuri Sana na huyu rafiki yangu tena kwa ukaribu Sana tukiwa mtaa mmoja. lakini kwa Sasa tupo mbali kwa maana ya distance lakini urafiki wetu bado upo na unakua siku Hadi siku.

Huyo rafiki yangu ni mtumishi wa taasisi Y wakati mke wake naye ni mtumishi wa taasisi W (mwanamke ni mtu wa kusafiri Mara kwa Mara kwa nature ya kazi yao).

Sasa week chache zilizopita nikiwa kwenye Moja ya group la WhatsApp linalodeal na ndoa.

Ghafla nikaona picha ya Shemeji yangu akiwa huged na jamaa Fulani imetumwa kwenye group na jamaa.

Kwa Sababu namfaham nilishtuka Sana nikafuatilia vizuri nani ametuma Ile picha, nikapata kumfaham. nikiwa najiuliza maswali na kutafakari.

Moja ya member katika hilo group aliuliza kwa kumtag mtu aliyetuma Ile picha,,, Boss huyo mwanamke ni mkali Sana ni wa wawapi...?

Jamaa akajibu ni wa mkoa X, alipo taja mkoa kwangu maumivu makali Sana yalikuwa upande wangu as if Mimi ndiye nasaritiwa.

Why niliumia Sasa Mimi wakati sio mke wangu amefanya hivyo?

Kama nilivyosema awali mume wa huyo mwanamke ni rafiki yangu Sana na tumepitia mengi Sana pamoja so ni Kama ndugu yangu tu kwa Sasa.

Huyo Shemeji kabla ya kuwa na rafiki yangu alikuwa na mahusiano na jamaa mmoja ambaye alikuwa na kesi. Yule jamaa akamkopa mwanamke pesa akimuahidi atamrudishia kumbe dhamira yake ni kumtapeli mwanamke na kweli mwanamke alikopa pesa kwenye Vikoba na akachukua mkopo benk then akampa jamaa apeleke kwenye kesi aliyokuwa anakabiliwa nayo.

Kumbe jamaa alifake na kutengeneza matukio ili apate pesa Wala hakukuwepo na kesi halisia Bali ilikuwa ni mipango iliyofanywa na Wakili asiyekuwa mwaminifu.

Basi mgogoro mkubwa ukaibuka mpaka mahusiano yakavunjika.

Ndipo huyo mwanamke akaanza mahusiano na rafiki yangu, kwa Sababu rafiki yangu ni ndugu yangu the way tulivyishi akamtambulisha kwangu yule mwanamke then maisha yakaendelee.

Ila kabla hatujua kuwa mwanamke alikotoka alikuwa na mzigo wa mikopo.

Kuna siku nilimuuliza rafiki yangu unaijua background ya huyo mwanamke ? Akasema hapana hakujua nilimshauri afuatilie kweli anagundua kuwa mwanamke yupo single kwa siku 25.

Hiyo taarifa ilinishtua kidogo na kunipa maswali inawezekanaje mwanamke aliyeumizwa Sana hajapata muda wa kutafakari anaanzisha mahusiano mapya ndani ya muda mfupi hivyo?

Seriously nilihisi hapo Kuna kitu zaidi kinatafutwa sio upendo, nikutaka kumhoji Sana rafiki yangu nilimwambia tu awe makini sana, Basi maisha yakaendelea Kama kawaida.

Miezi kadhaa badaye nikaona rafiki yangu anahangaika Sana kutafuta pesa ikionyesha ana uhitaji mkubwa Sana wa pesa isivyo kawaida yake.

Kama tujuavyo ukitaka kumjua mtu kaa karibu naye so kwa ukaribu niliokuwa nao kwa rafiki yangu niligundua jamaa ana matatizo.

Nikaomba kuongea naye bila hiana akafunguka yote A to Z kuhusu Shemeji na mikopo aliyochukua benk na kwenye vikobo ilikuwa mikopo iliyokuwa kiasi kwamba mshahara wote ulikuwa unakatwa huko huko, huku wa Vikoba nao wakiwa wanamsumbua sana.

Basi nikaingiwa na hurumu Sana kumuona rafiki yangu anateseka vile Kuna kiendo tulinunua eneo la pamoja kwa lengo la kujenga fremu za biashara Kisha tugawane fremu.

Rafiki yangu akaniomba kuuze ili ipatikane pesa ya haraka kuclear mikopo ya Shemeji.
nampenda Sana rafiki yangu, nilikubali kufanya hivyo.

Tukauza tukaclear mikopo yote ya Shemeji maisha yakaendelee.

Mimi nikapata Safari ya kikazi kwenda nje ya Tz. Wakati nasafiri rafiki yangu alikuwa kwenye process za mwisho kabsa za kumuoa huyo Shemeji yangu.

MUNGU saidia kweli alifanikisha na Mambo yalienda vizuri kabisa thou niliumia kutohudhuria harusi ya rafiki yangu lakini sikuwa na namna majukumu ya kazi yalinibana Sana.

Yapata miaka miwili Sasa sijaonana live na rafiki yangu japo tunawasiliana vizuri na Kama Kuna changamoto tunashirikishana ingawa Kuna mazingira nakuwa nipo mawasiliano yanakuwa hamna kabisa mwezi mzima au zaidi.

Mpaka hapa mtakuwa mmeelewa kwanini naumia Sana kuona huo usariti.

Sasa turudi kwenye group la WhatsApp,

Baada ya kuona Ile picha ya mke wa rafiki yangu nikataka evidence juu ya lile Jambo, kweli nilipata evidence zote zikiwemo videos.

Kumbe Mwanamke anamuaga Mwanume kuwa waenda kikazi kwenye mkoa huo lakini kumbe anaenda kwa mwanaume mwingine(mchepuko).

Kusema kweli tangu nione usariti ule nimejikuta sipo sawa kabisa naumia Sana maana rafiki yangu amehangaika Sana na kuhairisha Mambo yake mengi ili tu kuweza kumsaidia mwanamke pamoja na familia ya mwanamke.

Hapa napambana na nafsi mbili

Moja inaniambia nimwambie rafiki yangu ....na nafsi nyingine inasema nisimwambie ...

Tafadhali naombeni ushauri wenu wana jamvi nifanye nini nampenda Sana rafiki yangu

Nakuja kwenu kupata ushauri mpana zaidi.
Nimeaoma huu uzi ila nimeshindwa tambua wewe ni mwanaume au mwanamke
 
Naona utumie busara kumwambia amchunguze mkewe na safari zake ila usimwambie direct. Kama anampenda sana mke wake anaeza akaona unamsingizia na hata ukionyesha ushahidi mwanamke anaweza jitetea ukaonekana mbaya…mapenzi yana ufala mwingi, maandiko matakatifu ya biblia yanasema Ndoa na iheshimiwe na watu wote…usiwe chanzo cha kuvunjika kwa ndoa ya watu.
nakazia tu fuata hii maneno
 
Tafuta admin au mtu yoyote amuunganishe katika Hilo kundi la whatsaap then wewe nitoe kwa siku chache kama mbili Tatu hivi halafu hizo picha azione basi hapo jamaa atajua kila kitu na baadae atolewe na wewe urudi. Hatajua kama wewe ni mhusika ila atajua yote na ushahidi. Mke hapo atajua afanye nini
good idear fanya hivyo boss
 
Achana na wazo la kumuambia maana utasababisha ndoa kuvunjika kitu ambacho si kizuri. Kama hizo picha kwenye group unazo unaweza kutafuta njia jamaa azione hata kwa kumtumia kwa namba ambayo si yako ili ajue bila wewe kujulikana

Ogopa sana kuwa chanzo cha migigoro katika ndoa za watu maana wakisameheana utashindwa kuwaangalia usoni na wakiachana pia utashindwa kuwaangalia usoni
 
Mpe Mkanda Mzima, A to Z.

Kama unaona inaweza kuvunja urafiki wenu, basi tafuta namna ya kumfikishia ujumbe pasipo yeye kujua kuwa umetoka kwako.

Otherwise unamwita unamwambia kile unachofahamu, na inawezekana ukamwambia na asimwache mkewe, akamkanya tu kisha wakaendelea na ndoa yao, sio uwe teyare kupokea hilo.
 
J

Je, ingekuwa wewe mwanaume unayafanya hayo, mkeo aelezwe ili ukamatwe?
Aelezwe tu mkuu. Mkuki kwa nguruwe ila kwa binadamu mchungu. Sisi tumeshawahi kumshusha mchepuko wa mjomba tukiwa safarini. Tulikuwa tunaenda kwenye msiba, uncle alipewa gari na ofisi kwa ajili ya kubeba ndugu na jamaa njiani tukagundua mmoja kati ya marafiki zake waliopanda ni mchepuko wake. Aisee, hawatasahau ile siku. Walisemwa mno na binti akashushwa kwenye moja ya miji tuliyopita njiani.

Kuna familia zinathamini na kuheshimu sana ndoa, ikisikika unafanya upuuzi utatamani uhame ukoo. Haijajilishi una status gani hiyo ndo nidhamu tuliyojiwekea
 
uphaller mwingine,

kosa la kwanza mwanamke kaisaliti ndoa yake, kosa lingine kubwa zaidi ni kwenda kumsaliti mumewe kwa takataka moja isiyojielewa inayopost picha za ushahidi pamoja na video kwenye group, huku ikijua kabisa huyo ni mke wa mtu (hata ingekuwa hajaolewa bado siyo busara)..!

Watakushauri wenye busara zao mingi, me nimemaindi tu vile hao wachepukaji wote ile namna hawajielewi, mtseeeuuw' zao...!

Hata mie hapo sitii neno, mambo ya watu wanaojifunika shuka moja mazito sana, sio ya kuyaendea pupa.

Unaweza kutema nyongo, kesho unawakuta wako wote wanaendelea na maisha yao, unajificha wapi hapo?

Wayamalize wenyewe tu! Kwanza siku hizi watu wanauana na matukio kibao.
 
Hamna ugumu wowote tena hayakuhusu tena usitake kuharibu urafiki wenu, kama mwanaume anaakili timamu basi angeshastuka yaani mtu alouza kiwanja kuclear mkopo wa mpenzi,?,,,unahangaika naye wa nini
Narudia hayakuhusu,utakuja kunishukuru badae
 
Mkuu si usajili line kwa jina tofauti umwambie Huo jamaa yako hatajua
kama ni wewe utajifanya ni msamaria mwema then unamtumia na hiyo evidence ya picha,maana Huyo jamaa yako soon atalea ukimwi ama watoto Wa jamaa mwingine atalea.

Roho itakusuta maana ukweli unaujua na humwambii,Malaya sio Wa kulea.
 
Back
Top Bottom