Naombeni ushauri: Msichana wangu ana mchepuko

Naombeni ushauri: Msichana wangu ana mchepuko

Jamaaa kazinguaa sanaa... huyoo ni malayaaa na dyudyu yakoo haimtoshii..piga chini mzee kuna Ngomaa siku hizii
 
Kaka unahitaji ushauri gani tena apo....ACHA IYO NYUMBU....narudia tena ACHA IYO NYUMBU
 
Duh maneno makali mkuu
Sijuagi kufumba fumba we huoni hata andiko lake ke anaweza kukufanyia hayo yote na Bado ukaombq ushauri ufanyeje na unajiliza kabisa kwamba Bado unampenda,
Kati yake na huyo ke nani dume sasa
 
Habarini wakuu,

Nina msichana wangu mmoja tulianza nae mahusiano toka 2013, katika maisha ya mapenzi baina yetu kuna kipindi cha kati hapo tukagombana, ikabidi kila mmoja akaendelea na ishu zake.

Sasa yeye mwenzangu katika kipindi hicho tulichoachana akatoka na lijamaa huko akapewa kibendi, Mungu akamjaalia akajifungua mtoto wa kiume. Katika kipindi chote toka alipopata ujauzito jamaa aliyempa kibendi alikataa kuhudumia mpaka mtoto alipozaliwa.

Mara baada ya kujifungua huyu msichana akaanzisha tena mahusiano na jamaa aliyemtoa usichana (huyu siye aliyempa kibendi), katika mahusiano yao sijui kilichoendelea lakini niliskia waliachana.

Katika shida shida za utawala huu wa mjomba magu huyu msichana akanitafuta last year and tuka reconcile so akawamsichana wangu tena. Tatizo lilikuja alipotaka nimuoe, mimi sikuwa na tatizo sema kama mtu ninaejielewa ikabidi nifanye uchunguzi (sikutaka kuingia kichwakichwa kwenye ishu za ndoa) kama hana mchepuko huko alipo na ndio hapo nilipojua anatoka na lijamaa lake la zamani.

Ushahidi nilikuwa nao wa kutosha kuanzia messages hadi baadhi ya siku huwa anaenda kulala kwa mchizi, sasa nilipo mconfront kama najua anamchepuko na najua huwa analala kwa mchizi baadhi ya siku msichana alinijia juu kwa maneno mengi akataka tuachane, tatizo sikuwa na nia ya kumuacha ilikuwa tuongee tuyamalize lakini mwenzangu akawa analazimisha tuachane, sasa katika marumbano mimi nikaona isiwe tabu tukapigana chini.

Sasa cha kushangaza jioni yake baada ya kuachana akanitumia message kuniomba msamaha kwa alivyokuwa ananijibu na hataki tuachane kwa hasira, nikamwambia nimemsamehe.

Sasa hapa nipo dilema maana msichana nampenda na yeye ana feelings nasema hivi kwa sababu tunakaa mikoa jirani na kila nikiwa na shida naye nikimpigia aje kesho jua lazima atatia maguu gheto, sijawahi kumwambia aje akazingua au akagoma au akaleta kisingizio cha kutokuja.

Na hata kesho nikimwambia aje huku nilipo atakuja ingawa tumeachana, tatizo hataki kukiri makosa yake na hataki hata kusikia ushahidi niliokuwa nao.

Naombeni ushauri wakuu nimpotezee kimoja au niwe mvumilivu nishee na mchizi?
share na mchizi mwanangu umoja ni nguvu utengano ni dhaifu!! wahenga waliyaona haya!
 
mtoa mada sijui ni mtu wa aina gani wewe. Kwa kifupi wewe ndio mchepuko wa huyo demu njia kuu ni huyo mwingine. Halafu demu kazaa na mtu ana jamaa mwingine anakutukana bado tu unataka kumuoa hustuki? au ndio mpaka umwagiwe tindikali usoni ndio ujue hutakiwi?
Sidhani kama mm ndo mchepuko maana hadi kwao nafahamika na bi mdashi wake
 
Hivi mwanaume unaanzaje kupenda?
How on earth unapenda
eti mwanaume kamili kabisa unapenda
acha ujinga wewe jamaa..Grow up..ndio maana unatombewa
 
Back
Top Bottom