Naombeni mwongozo

Usijali rafiki.....
Pamoja sana

 

Weka bando ya wiki, tena kama ni airtel sh elfu ngapi hyo tosha kabisa, halafu vocha uwe unaweka mwenyewe kwenye hiyo simu, kama ni simu yake aweke kwa pesa yake mwenyewe, wewe weka hiyo yako ya nyumbni hiyo vocha.
 
Watu wanadhani ma hausgel hawatakiwi kuwa na social life kama watu wengine
Uuwwwiiiiii, wewe ndo umekuja na mjadala mwingine kabisaaaaaaa, nje ya nilichoombea mwongozo.....
kama wewe ndo Spika, tunapiga kura ya kutokuwa na imani nawe
 
Weka bando ya wiki, tena kama ni airtel sh elfu ngapi hyo tosha kabisa, halafu vocha uwe unaweka mwenyewe kwenye hiyo simu, kama ni simu yake aweke kwa pesa yake mwenyewe, wewe weka hiyo yako ya nyumbni hiyo vocha.
Asante kwa mwongozo.....
Pamoja sana
 
Me nadhan hili tatizo ni gum kulizuia...just imagine hata wewe ukiwa ofisini ukitaka labda kuprint cv/picha au kutuma personal email do you go to the Internet cafe?..si unatumia ya ofisi?...mfano mwingn ni simu ya ofisi,lazima kuna siku utajiibaiba and make personal calls....my point is umueleweshe tu huyo mdada kwamba awe anabakisha walau ela ya msg au ku beep
 

Akili za usiku...!
 
Uuwwwiiiiii, wewe ndo umekuja na mjadala mwingine kabisaaaaaaa, nje ya nilichoombea mwongozo.....
kama wewe ndo Spika, tunapiga kura ya kutokuwa na imani nawe

Nimeelewa ulichosema ndo mana nikaongeza point hapo
 
anajua kutumia bundle ila sasa hela yooote inaishia kupiga simu zake anazozijua

ndugu zangu, simu ni sumu kwa beki 3. kuna 1 nilimtoa huko kijijini alikuwa ametulia lakini baada ya kumpa simu imekuwa balaa. ameshoboka na hivyo vivulana mpaka natamani nimnunulie land line ya ttcl. akiwekewa salio halichukui muda kuisha na ameingiza caller tunes kwenye simu sijui hata nani kamfundisha--nadhani vitakuwa hivyo vivulana vyake.

sasa simuwekei salio lolote kwenye simu. majina ya 'mama' na 'baba' nimeyasevu kwa kutumia kanuni ya TAFADHALI NIPIGIE. ikitokea emergency akipiga simu hata kama haina salio napata ujumbe kwenye simu yangu ninampigia. nimefunga (bar) all outgoing calls na nataka niende Vodacom wafunge incoming SMS (SMT) kuzuia wavulana wake wasimtumie sms ili atulie alee mtoto--najua hawawezi ku-afford kumpigia daily. nadhani hii itasaidia.
 
Asante rafiki.
Ila sasa nikiiblock kupiga namba nyingine si nitakuwa namwonea? akitaka kuongea na wazazi wake au ndugu wengine itakuwaje?

akitaka kuongea na ndugu asubiri ukitoka kazini awapigie kwa simu yako. hao 'ndugu' unao-entertain ndio watamfanya akose umakini wa kufanya kazi kwa ufasaha.
 
Bwana tpaul hii picha yako inanipaga burudani sana... Ukiona mwanaume amelia hivyo... ni hataree aiseee!!!

simu ya home ndiyo hiyohiyo ya beki 3 au wewe unaongelea simu ya home ipi?
 
Reactions: BAK
wanawake wengi wapo hivo....unaweza mtumia vocha ya elf 5 akakuandikia msg moja tu ya 'thanx'. baada ya hapo husikii chochote mpaka vocha uliyompa iishe ndo atabeep then anaomba vocha

MAJANGA! Tena wakati anakuomba airtime ndipo utasikia akikuita 'BABY' baada ya kumtumia vocha hakuna cha babe wala mjusi. Hawa viumbe wewe waone hivohivo, hawafai kabisa!
 

hahaha! umenikumbusha mbali na hiyo terminology ya MUGRO. hiyo term tumeitumia sana tukiwa chuoni-- kampasi ya mazimbu (now Solomon Mahlangu Campus).
 

mkuu inaonekana huwajui mabeki 3 wewe--huna uzoefu nao hata kidogo. ngoma usiyoijua, usiicheze!
 

swadakta! hii njia nayo iko poa sana. au unaweza kuwa unamwachia hata 1000 kwa ajili ya hiyo dharula--maana yake ni kwamba hiyo itaendelea kuwepo hadi dharula itakapojitokeza, kuliko ukiiweka kwenye cm halafu beki 3 anaitumia kuwasiliana na vibuzi vyake badala ya kuzingatia kazi.
 

unaona sasa? ngoja wale wanaodhani beki 3 wanaonewa waone shughuli yao ilivyo pevu. mnaona mambo haya?
 
Huyo mfanyakazi hana ndugu?Tuseme dharula unazo wewe tu ila yeye hana dharula?Wewe umewekewa masharti ya kutumia simu na nani na shilingi ngapi kwa wiki?

elewa somo kwanza kabla ya kutema povu. hakuna mtu aliyemzuia kuwasiliana ila aweke fedha zake, asitumie vibaya mali ya mwajiri.

imagine umemtumia mwanao karo halafu amechukua amekula yote kisha akarudishwa home. unapomuuliza anakuambia alichukua pesa ya karo akachezea kamari! utamuelewa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…