Mkuu
Chief-Mkwawa kumekua na post nyingi sana za watu kuja kuomba msaada baada ya simu zao au laptop kuibiwa
Binafsi sio mtaalamu wa maswala haya ila naamini iwapo zitachukuliwa hatua stahiki mapema kabla simu haija potea, kwa kufanya settings kadhaa na kuinstall app fulani na kuhifadhi serial no kadhaa basi nafasi ya kuifuatilia na kuipata simu iliopotea inakua kubwa
With all due repect nikuombe uandike bandiko maalum kuhusu ni namna gani unaweza kuiandaa simu yako kabla haijapotea ili uwe kwenye nafasi nzuri ya kuitrack pindi ikitoweka
Then tutawaomba Mod waiweke hapo juu hiyo thread iwe stick ili kuwasaidia wengi
Nawasilisha mkuu