Naombeni msaada kurudi bongo

Naombeni msaada kurudi bongo

Mkuu, tulia tu huko huko na hizo dola buku na mianane zako, maisha yamebadilika sana sana mambo yanaenda kasi sana tangu 1992, wewe endelea kukata vitunguu na kubeba mabox huko, game ya TZ ni mziki mwingine.
Huyu dingi nae anazingua mkuu,we miaka 26 ng'ambo mfukoni una $1800 sasa huko alifata nini?na hapo akisema alipe nauli akifika bongo anaishia kuwa ombaomba.
 
Habari wana jf.
Mimi ni mbongo ambaye nipo ughaibuni tangu 1992 na sijawahi kurudi bongo. Nilikuja huku kutafuta maisha na kusoma, lakini kutokana na gharama za maisha na gharama za elimu sikuweza kusoma. Sasa nina miaka 51 na natamani kurudi bongo. Elimu yangu ni ya form 4 ya pugu secondari 1988. Benki nina dola 1800 tuu. Jee naweza kurudi bongo na kuishi comfortably? Yaani kunywa maziwa, kulala pazuri, kutotumia madaradara kwa usafiri, kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu

Mkuu, pole sana ila usikate tamaa jipange na uendelee kupiga box kwa angalau miaka mingine 5 au 10.

Je umeoa na una familia?

Kama jibu ni ndio basi ongeza kazi hiyo miaka 10 kwa ajili ya pensheni yako ya uzeeni kwenye kamradi ukirudi TZ.

Pia kama una familia na nyumba haipo, basi chukua bima ya kama Euro 200000 hivi ili iwasaidie endapo utaaga dunia.

Watoto wa kiafika huko ughaibuni wakifika miaka 16 tu wanaanza kuwakoromea wazazi wao kwa kuwahoji kwamba kwanini wao ni maskini, hiyo inauma sana maana huwezi kuchapa viboko.

Kuwa wale wazazi ambao hutumia ile fedha ya watoto ya kila wiki badala ya kuwawekea akiba.

Na kama waishi kihalali huko majuu basi angalau utakuwa umewekeza kwenye mafao yao wazungu angalau kila wiki utakuwa na mshiko kidogo.

Mimi nimeishi huko kama wewe lakini nilipofika miaka 35 nikasoma alama za nyakati na sasa nashukuru Mungu namudu maisha ya pande zote.

Nilikuwa nikirudi bongo kuangalia wapi niweke kitega uchumi na imesaidia sana.

Ila hujachelewa, piga box angalau miaka 5 kama si 10 ili upate chochote kamtaji kuweka kitega uchumi ambacho ukiamua kurudi kimoja utakuwa wasimamia wewe mwenyewe.

Kuwa twarudi nyumbani mara kwa mara kunasaidia sana kupata mawazo mbadala na yale ya kupiga boksi tuu kutwa kucha.
 
Le Mutuz na yeye alirudi Bongo akiwa na umri around na huo na hivi sasa nasikia yeye ndo King of Social Networks! Sasa wewe ukitua Bongo itabidi ufungue Instagram Account na ujiite Zee la Mastory Ya Mbele! Au nikukopeshe jina langu nililokuwa natumia miaka hiyo, enzi hizo kabla ya JF... Mr. Experience, na stori zangu za kuuza Tanzanite wakati hata Arusha kwenyewe sikujui!

Dah! Ujana raha sana!!
 
kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu

Njoo uokote makopo tu hakuna namna chakula kizuri ambacho sio cha nafaka utakipata kwa akina Mama lishe!
 
Le Mutuz na yeye alirudi Bongo akiwa na umri around na huo na hivi sasa nasikia yeye ndo King of Social Networks! Sasa wewe ukitua Bongo itabidi ufungue Instagram Account na ujiite Zee la Mastory Ya Mbele! Au nikukopeshe jina langu nililokuwa natumia miaka hiyo, enzi hizo kabla ya JF... Mr. Experience, na stori zangu za kuuza Tanzanite wakati hata Arusha kwenyewe sikujui!

Dah! Ujana raha sana!!

JF raha sana,

Chige, umenichelesha sana.

Mr experience you know!
 
Kwanza aliyemwambia sisi wabongo tunakuka nafaka ni Nani? Hata Kama tunakula ila umeonyesha dharau.naona ushaharibiwa na mapepo ya kizungu Sasa nakushauri ubaki huko huko hapa bongo utaishia kuwa mzigo wa taifa
 
Kwanza aliyemwambia sisi wabongo tunakuka nafaka ni Nani? Hata Kama tunakula ila umeonyesha dharau.naona ushaharibiwa na mapepo ya kizungu Sasa nakushauri ubaki huko huko hapa bongo utaishia kuwa mzigo wa taifa

Kwani mapepo ya kizungu yakoje mkuu?

🙂🙂
 
Mkuu, pole sana ila usikate tamaa jipange na uendelee kupiga box kwa angalau miaka mingine 5 au 10.

Je umeoa na una familia?

Kama jibu ni ndio basi ongeza kazi hiyo miaka 10 kwa ajili ya pensheni yako ya uzeeni kwenye kamradi ukirudi TZ.

Pia kama una familia na nyumba haipo, basi chukua bima ya kama Euro 200000 hivi ili iwasaidie endapo utaaga dunia.

Watoto wa kiafika huko ughaibuni wakifika miaka 16 tu wanaanza kuwakoromea wazazi wao kwa kuwahoji kwamba kwanini wao ni maskini, hiyo inauma sana maana huwezi kuchapa viboko.

Kuwa wale wazazi ambao hutumia ile fedha ya watoto ya kila wiki badala ya kuwawekea akiba.

Na kama waishi kihalali huko majuu basi angalau utakuwa umewekeza kwenye mafao yao wazungu angalau kila wiki utakuwa na mshiko kidogo.

Mimi nimeishi huko kama wewe lakini nilipofika miaka 35 nikasoma alama za nyakati na sasa nashukuru Mungu namudu maisha ya pande zote.

Nilikuwa nikirudi bongo kuangalia wapi niweke kitega uchumi na imesaidia sana.

Ila hujachelewa piga box angalau miaka 5 kama si 10 ili upate chochote kamtaji kuweka kitega uchumi ambacho ukiamua kurudi kimoja utakuwa wasimamia wewe mwenyewe.

Kuwa twarudi nyumbani mara kwa mara kunasaidia sana kupata mawazo mbadala na yale ya kupiga boksi tuu kutwa kucha.
Asante kwa kumshauri, ila huwezi kufudisha mbwa mzee mbinu mpya. Unaona akili zake zilivyo za kipuuzi? Eti anawaza kuja na usd 1800 kutanua bongo kwa maisha yake yoe atakayoishi. Unamwambia akae another 5 - 10 yrs wakati keshapiga 26 yrs hata kama angekuwa anasevu nauli tu ambayo hakuitumia kuja bongo kila mwaka kwa miaka 26 angekuwa na kiasi kikubwa. yawezekana huyu ali invest kwenye papuchi.
 
Asante kwa kumshauri, ila huwezi kufudisha mbwa mzee mbinu mpya. Unaona akili zake zilivyo za kipuuzi? Eti anawaza kuja na usd 1800 kutanua bongo kwa maisha yake yoe atakayoishi. Unamwambia akae another 5 - 10 yrs wakati keshapiga 26 yrs hata kama angekuwa anasevu nauli tu ambayo hakuitumia kuja bongo kila mwaka kwa miaka 26 angekuwa na kiasi kikubwa. yawezekana huyu ali invest kwenye papuchi.

Sidhani kama yupo serious analeta gumzo la jumapili.

Ila kwa Ulaya anaweza kabisa kutengeneza kitu kwa miaka 10 ijayo hana ujanja.

Lakini tupo hapa watu wa kutoa ushauri wa bure, inapobidi.
 
Pesa yako ndogo sana.
Njoo bonde la Ruvu tafuta eneo ufuge ng'ombe wa maziwa ila lazima ukubali Kula nafaka na kusurubika kwa sasa huna hela ya kuacha kula nafaka na kuishi maisha mazuri.
 
Ni 1800 au 18'000 hujamalizia 0 ya mwisho mzee baba mbona kama 18'000 unaludi tu nyumbani na kujipanga mzee baba
 
Ni 1800 au 18'000 hujamalizia 0 ya mwisho mzee baba mbona kama 18'000 unaludi tu nyumbani na kujipanga mzee baba

Kwa boksi za Ughaibuni huyu jamaa bado ni kijana sana.

Kwa nchi za Ulaya umri wa kustaafu ni miaka 60- 65 kwa wanaume.

Uingereza wanafikiria kuongeza kabisa hadi 75 ili mtu afe akiwa kazini kwenye maboksi.
 
Habari wana jf.
Mimi ni mbongo ambaye nipo ughaibuni tangu 1992 na sijawahi kurudi bongo. Nilikuja huku kutafuta maisha na kusoma, lakini kutokana na gharama za maisha na gharama za elimu sikuweza kusoma. Sasa nina miaka 51 na natamani kurudi bongo. Elimu yangu ni ya form 4 ya pugu secondari 1988. Benki nina dola 1800 tuu. Jee naweza kurudi bongo na kuishi comfortably? Yaani kunywa maziwa, kulala pazuri, kutotumia madaradara kwa usafiri, kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu

usd 1800 duuuuu.yani nyie mkiendaga huko ni kuona mmemaliza kila kitu.unashituka kumekucha.tumia akili kama una ndugu yupo bongo fanya kuwa una tuma vitu kutoka ugaibuni kukuuzia ili upate kuishi.nimeamini wanao weza kuishi na ndugu zao ni wanzanzibari na wahindi tu.tulio baki tunapenda kuwa kama miungu.karibu uje kaburini maana ndo nchi mkitaka kufa mnakumbuka kwenu
 
Habari wana jf.
Mimi ni mbongo ambaye nipo ughaibuni tangu 1992 na sijawahi kurudi bongo. Nilikuja huku kutafuta maisha na kusoma, lakini kutokana na gharama za maisha na gharama za elimu sikuweza kusoma. Sasa nina miaka 51 na natamani kurudi bongo. Elimu yangu ni ya form 4 ya pugu secondari 1988. Benki nina dola 1800 tuu. Jee naweza kurudi bongo na kuishi comfortably? Yaani kunywa maziwa, kulala pazuri, kutotumia madaradara kwa usafiri, kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu
Mkuu kwa umri huo bora ubaki hukohuko, maana utaishia kulima vibarua tu mbaya zaidi utakapowakuta uliowaacha wanamaisha mazuri ndio utakufa kabla ya siku zako
 
Back
Top Bottom