Naombeni msaada kurudi bongo

Naombeni msaada kurudi bongo

Acheni kumkatisha tamaa huyu mzee, aje Tanzania apambane kutafuta kwanza kadi ya chama cha Ccm na kuunga mkono juhudi, atapewa U DC, au aje ajipange agombee ubunge siasa za Tanzania zinalipa..... Na zitamtoa fasta aungane na kina Le Mutuz
 
Hahaha dada, huyo yeye anataka KURUDI, wewe unamshauri ASIRUDI. Inaonekana fursa aliyokuwa nayo inaishia ukingoni, sasa anaanza kuwaza kurudi ALIKOTOKA. Labda kazi anayofanya haina hizo benefits, Maana nasikia nchi hizo za ughaibuni zinapambana na wahamiaji haramu, wale illegal, wasio na vibali vya kuishi huko kihalali. Je, ikiwa ni miongoni mwa hao, Still atapata hizo benefits au bora arudi nyumbani kama alivyoomba kushauriwa nama ya ku survive hapa kwetu.
Atajijuuu
 
Kabla ya kuchukua maamuzi ya kuja Tz, tafakari kwanza kwamba hiyo 51yrs unarudi kuanza kutafuta maisha huku bongo au kuendeleza maisha uliyonayo,,,,,,Tafakari usijefia Airport!
 
Ukila nafaka utakufa?
Huku matajiri hizo nafaka ndiyo chakula chao kikuu.
Halafu Tanzania usipokula wali,ugali utakula Nini!
Sikiliza old Pugu boy huna hela ya kuacha kula nafaka hiyo hela yako ukija nayo huku utapata nayo shida tu.

Mbona una hasira kali sana?
Hasira yote hii ni juu ya nini sasa?
You need a chillout pill bwana mdogo.
Wengine mumenipa ushauri murua asanteni sana. Na wale mumekasirika sana samahani sana.
 
Ukishapata usd 500 kwa wiki, ukishalipa tax? Na ukishalipa medicare insurance? car insurance? childcare? pocket money ya watoto? leisure activities za watoto? kula chakula kizuri? kunabaki usd ngapi?
au unataka niishi nakula nafaka nisave pesa? kama hujui maisha ya huku siyo lazima useme lolote.
Wewe unataka kudanganya watu
 
Huyo anawatania dereva anayeendesha Basi kama UDA analipwa £500 kwa wiki bado overtime. Na nyumba kodi 75 kwa wiki ya serikali na binafsi ni 100 asiwapotezee muda

Anatafuta kiki, hahahaha
 
M
Sikati vitunguu wala maboxi. Naendesha mabasi ya mjini. Kama UDA ya zamani.
Mkuu acha mawazo potofu, watu tunabeba box haijarishi kwa namna ipi, tuna mpango kwamba ikifika 30,000 USD ndo turudi Tanzania kusettle japo tumeshaweka vibanda tz,

Endelea kuendesha ma hekarusi ili angalau kwa miaka mingine 9 uwe na miaka 60 lakin kwa mwezi tunza angalau 500 USD ili kwa miezi 90 yaan miaka kama 8 uwe na 35,000 USD hapo utakuwa na kiburi kuenda bongo, hata Magufuli atakuwa kastaafu
 
Kabla ya kuchukua maamuzi ya kuja Tz, tafakari kwanza kwamba hiyo 51yrs unarudi kuanza kutafuta maisha huku bongo au kuendeleza maisha uliyonayo,,,,,,Tafakari usijefia Airport!
Kama kashindwa kusaka maisha huko aje afe tu huku.Si mda mrefu atatamani arudi Uko,huku kila kitu ni feki,kuanzia maisha mifumo yote nk.
 
Dar karibu sana Bongo hyo 1500 mbona ndogo. Ila bora urudi tu nyumbani uanze upya ungejuaga ungerudi ukiwa na nguvu. Sisi wenyewe twapambana kibishi bishi maisha yakaendelea.
Makengeza upo?
Miss you xoow much
 
Mkuu,usirudi Bongo komaa huko huko ikiwezekana lirudi jeneza na mwili wako lakn siyo kurudi ukiwa hai...Tz kwa hivi sasa ni jehanamu heri uwe mbwa kwenye nchi za wenzetu kuliko kuwa mwanadamu Tanzania
By the way,unamfaham John? siyo John Malecela huyo ndyo ametutoa Kanaani (kwenye nchi ya maziwa na asali) na kutupeleka utumwani (Misri)
Nakuomba usirudi vimba juu kwa juu!
 
Habari wana jf.
Mimi ni mbongo ambaye nipo ughaibuni tangu 1992 na sijawahi kurudi bongo. Nilikuja huku kutafuta maisha na kusoma, lakini kutokana na gharama za maisha na gharama za elimu sikuweza kusoma. Sasa nina miaka 51 na natamani kurudi bongo. Elimu yangu ni ya form 4 ya pugu secondari 1988. Benki nina dola 1800 tuu. Jee naweza kurudi bongo na kuishi comfortably? Yaani kunywa maziwa, kulala pazuri, kutotumia madaradara kwa usafiri, kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu
Hiyo $1800 tayari ushalala ticket au nauli pia hujatoa?
 
Habari wana jf.
Mimi ni mbongo ambaye nipo ughaibuni tangu 1992 na sijawahi kurudi bongo. Nilikuja huku kutafuta maisha na kusoma, lakini kutokana na gharama za maisha na gharama za elimu sikuweza kusoma. Sasa nina miaka 51 na natamani kurudi bongo. Elimu yangu ni ya form 4 ya pugu secondari 1988. Benki nina dola 1800 tuu. Jee naweza kurudi bongo na kuishi comfortably? Yaani kunywa maziwa, kulala pazuri, kutotumia madaradara kwa usafiri, kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu
Hongera kwa maamuzi mema,

Nashauri.

Jipe muda wa kujiweka sawa ili uweze kurudi home,wekeza pesa nyingi zaidi from usd1800 to 20,000
Tanzania imebadilika.
 
Nimekumbuka...nataka nikuchape swali jingine hiyo 1800usd...na nauli ni hapo hapo....na vp ukitua bongo ndio hiyo unatumia kupanga nyumba!!... kweli maisha mbinuko...
 
Mkuu, tulia tu huko huko na hizo dola buku na mianane zako, maisha yamebadilika sana sana mambo yanaenda kasi sana tangu 1992, wewe endelea kukata vitunguu na kubeba mabox huko, game ya TZ ni mziki mwingine.
Umewahi kuishi ughaibuni?
 
Habari wana jf.
Mimi ni mbongo ambaye nipo ughaibuni tangu 1992 na sijawahi kurudi bongo. Nilikuja huku kutafuta maisha na kusoma, lakini kutokana na gharama za maisha na gharama za elimu sikuweza kusoma. Sasa nina miaka 51 na natamani kurudi bongo. Elimu yangu ni ya form 4 ya pugu secondari 1988. Benki nina dola 1800 tuu. Jee naweza kurudi bongo na kuishi comfortably? Yaani kunywa maziwa, kulala pazuri, kutotumia madaradara kwa usafiri, kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu
Pole sana mkuu....
Kwanza naomba nikupe Pole kwa kuchelewa kung'amua kwaamba una/ulipaswa urudi home ukingali mwenye nguvu. Na hiyo pesa ulioayo, ukweli ni kiduchu sana kiasi cha kwamba ukirudi Tz pesa itakwisha na utakufa haraka kwa stress na frustrations.
Mimi niliamua rasmi kurudi, Tz nikiwa na umri wa miaka 35. Na ukweli sikua na fedha taslimu, ingawa nilikua tayari nimenunua vifaa na baadhi ya vitu ambavyo leo vimenisaidia na ninakula kiulaini..... Ingawa pale mwanzo nilipata ugumu kidogo namna ya kuanza na kuzowea maisha ya kitaa.
 
Back
Top Bottom