Maumivu ya mapenzi hayatakwisha mpaka pale kila mmoja wetu atakapokuwa anajua anataka nini penzini na tukiwa na subira na uvumilivu,kila mmoja wetu yupo ambaye ameumbwa maalumu kwa ajili yake,yupo ambaye nyoyo zenu zimeunganishwa automatic na nguvu ya penzi na ukikutana nae haihitaji hata kuambiwa kwani moyo wako wenyewe utakuambia kwani ndiye hitaji lake.
Jambo la hekima ni kuwa na uvumilivu na subira kwani tamaa za kimwili ndizo ambazo hutupelekea tunaangukia sehemu ambazo zinatufanya tulie kwa kuendekeza mahitaji ya miili yetu,lazima utambue kuwa safari ya kuelekea kumpata yule atakaye ujaza moyo wako furaha na raha ni ndefu sana inayohitaji subira kwani hapo kati kati ya safari utakutana na walaghai wengi sana ambao wote wanazungumza lugha moja inayofanana hivyo kukupa wakati mgumu wa kumtambua yupi mkweli na yupi muongo.
Tusiwapime wenzi wetu kwa maneno yao matamu kwani si mara zote maneno hutoka moyoni bali matendo na ila kama unatafuta hela penzini basi maumivu ni halali yako na kama unatafuta furaha penzini,ukivuta subira na ukivumilia hatimaye utaipata furaha ya kweli,kwani muumba kamwe hajawahi kumtupa au kumjaalia kitu kibaya mja mwenye subira na mvumilivu na wakati ukifika utampata wako.