Naomba ushauri

Kbd

JF-Expert Member
Oct 9, 2009
1,260
447
Wanajukwaa nawasalimu wote kwa heshima na taadhima. Mimi Ninaishi kwenye nyumba ya kupanga mahali fulani na baba na mama mwenye nyumba wanaishi hapo hapo. Sasa huyu baba mwenye nyumba anatabia ya kumpiga mke wake sana esp anapolewa. Hiyo tabia imekuwa ikiniudhi sana sana na nilishawahi kuongea nae kuhusu hiyo tabia akaahidi kujirekebisha. Alijirekebisha kwa muda lakini naona sasa imeanza upya.................. Yaani ni mkorofi sana, anambonda mkewe na matusi na maneno ya kashfa mengi mno mpaka aibu. Huyu mdada kipindi fulani aliondaka kwao, na huyu mume akaomba samahani kwa wazee na kuwaahidi kuwa kitendo hicho hakitajirudia lakini naona mambo ni yale yale................................................................................................................................................................................................................... Sasa nilikuwa nauliza mimi kama raia mwema, naweza kwenda polisi kumshtaki huyu baba au nikaenda japo kwa tamwa kupata uongozi wa kisheria...........................mimi niko kinyume na talaka lakini ningetamani kumfundisha huyu mwanaume kitu ili asirudie kitendo kama hiki tena. Naomba kuwasilisha.
 
KBD... Inatakiwa uongee na huyo mama... kama huyo baba imeshindikana...

Yeye atacho amua ndio itakua msingi sababu waweza enda mbele na huyo mama akakukana.
 
KBD... Inatakiwa uongee na huyo mama... kama huyo baba imeshindikana...

Yeye atacho amua ndio itakua msingi sababu waweza enda mbele na huyo mama akakukana.


Asante sana dia.........huyo dada kwa kweli anateseka sana. Ila nilifikiria labda wakati wa pulukushani mi ndio niwaite polisi.
 
mkuu...kaa mbali na maisha ya watu.
kama huyo mama anapigwa na hachukui hatua zozote basi ujue kuna jambo.
 
1. Wakati unatafakari njia ya kumsaidia huyo mama pia ufikirie namna ya kupata nyumba nyingine kwani huyo baba akikustukia unakula "notice."

2. Uwe mwangalifu huyo jamaa anaweza kukuzulia jambo ukashangaa.

3. Muelimishe huyo mama achukue hatua huyo bwana awekwe kikao ama na wazazi wa pande zote 2 kabla ya kulifikisha swala hilo kwenye vyombo vya sheria. Polisi unaweza kwenda mkamwekea mtego ila kwa polisi wetu sidhani kama utapata ushirikiano wa kutosha....
 
mkuu...kaa mbali na maisha ya watu.
kama huyo mama anapigwa na hachukui hatua zozote basi ujue kuna jambo.


Asante kwa ushauri. Ila huoni kama binadamu mwenzetu anaumia na sisi tunaangalia. Akija akifa!!!
 
1. Wakati unatafakari njia ya kumsaidia huyo mama pia ufikirie namna ya kupata nyumba nyingine kwani huyo baba akikustukia unakula "notice."

2. Uwe mwangalifu huyo jamaa anaweza kukuzulia jambo ukashangaa.

3. Muelimishe huyo mama achukue hatua huyo bwana awekwe kikao ama na wazazi wa pande zote 2 kabla ya kulifikisha swala hilo kwenye vyombo vya sheria. Polisi unaweza kwenda mkamwekea mtego ila kwa polisi wetu sidhani kama utapata ushirikiano wa kutosha....


Nashukuru kwa ushauri dia.

Hapo kwa bluu, kama hio ndio itakuwa gharama ya kumsaidia huyo mama.............niko tayari.
 
Sangara ukute huyo mama hajui kua kuna sehemu ya kulilia??

Sio amshauri then ndio aachane nae??


Unajua huyu dada aliolewa kijijini akaletwa kwa mume........sasa inawezekana hajui aanzie wapi na aishie wapi.
 
Unajua huyu dada aliolewa kijijini akaletwa kwa mume........sasa inawezekana hajui aanzie wapi na aishie wapi.


Sijui kwa kweli, ila it is beta umshauri.... sio kwamba kutaka talaka but atleast kumuonesha mwanaume kua she understands her rights....
 
Jambo la kwanza, jaribu kuongea na muathrika namaanisha mkewake...haingii akilini kwenda polisi wakati mlengwa hujamshirikisha...na kwa sbb umesema inatokea anapolewa nadhani mngejaribu/wajaribu jinsi ya kumfanya aache pombe.....Lakini mkitaka kulichukulia the way unavyotaka liende kaka unageuziwa kesi sasa hv na nyumba utaiona chungu...
 
Sijui kwa kweli, ila it is beta umshauri.... sio kwamba kutaka talaka but atleast kumuonesha mwanaume kua she understands her rights....


Asante dia, nitazingatia.
 
Jambo la kwanza, jaribu kuongea na muathrika namaanisha mkewake...haingii akilini kwenda polisi wakati mlengwa hujamshirikisha...na kwa sbb umesema inatokea anapolewa nadhani mngejaribu/wajaribu jinsi ya kumfanya aache pombe.....Lakini mkitaka kulichukulia the way unavyotaka liende kaka unageuziwa kesi sasa hv na nyumba utaiona chungu...


Asante kwa ushauri.
 
Wanajukwaa nawasalimu wote kwa heshima na taadhima. Mimi Ninaishi kwenye nyumba ya kupanga mahali fulani na baba na mama mwenye nyumba wanaishi hapo hapo. Sasa huyu baba mwenye nyumba anatabia ya kumpiga mke wake sana esp anapolewa. Hiyo tabia imekuwa ikiniudhi sana sana na nilishawahi kuongea nae kuhusu hiyo tabia akaahidi kujirekebisha. Alijirekebisha kwa muda lakini naona sasa imeanza upya.................. Yaani ni mkorofi sana, anambonda mkewe na matusi na maneno ya kashfa mengi mno mpaka aibu. Huyu mdada kipindi fulani aliondaka kwao, na huyu mume akaomba samahani kwa wazee na kuwaahidi kuwa kitendo hicho hakitajirudia lakini naona mambo ni yale yale................................................................................................................................................................................................................... Sasa nilikuwa nauliza mimi kama raia mwema, naweza kwenda polisi kumshtaki huyu baba au nikaenda japo kwa tamwa kupata uongozi wa kisheria...........................mimi niko kinyume na talaka lakini ningetamani kumfundisha huyu mwanaume kitu ili asirudie kitendo kama hiki tena. Naomba kuwasilisha.

Bahati yake wewe siyo mimi maana ingekuwa mimi ningemshughulikia mwenyewe kwa mikono yangu. He is a complete jackass.

Ila unaweza kumdunda mumewe halafu mke akakuchenjia kwa nini umempiga mumewe. Haya mambo bana....sometimes they have no rhyme or reason to them.
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
Asante sana dia.........huyo dada kwa kweli anateseka sana. Ila nilifikiria labda wakati wa pulukushani mi ndio niwaite polisi.

Hicho kituo cha polisi kipo mbali kiasi gani na unapoishi? Manake hizi nyumba zetu za Uswazi bana.....mpaka polisi wafike...kwanza sijui watafikaje. Nyumba ina address?
 
I think ushauri wa da Asha hapo juu nimeupenda zaidi..Kujaribu kuongea na huyo dada kwanza kabla hujachukua uamuzi wowote!
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
Wanajukwaa nawasalimu wote kwa heshima na taadhima. Mimi Ninaishi kwenye nyumba ya kupanga mahali fulani na baba na mama mwenye nyumba wanaishi hapo hapo. Sasa huyu baba mwenye nyumba anatabia ya kumpiga mke wake sana esp anapolewa. Hiyo tabia imekuwa ikiniudhi sana sana na nilishawahi kuongea nae kuhusu hiyo tabia akaahidi kujirekebisha. Alijirekebisha kwa muda lakini naona sasa imeanza upya.................. Yaani ni mkorofi sana, anambonda mkewe na matusi na maneno ya kashfa mengi mno mpaka aibu. Huyu mdada kipindi fulani aliondaka kwao, na huyu mume akaomba samahani kwa wazee na kuwaahidi kuwa kitendo hicho hakitajirudia lakini naona mambo ni yale yale................................................................................................................................................................................................................... Sasa nilikuwa nauliza mimi kama raia mwema, naweza kwenda polisi kumshtaki huyu baba au nikaenda japo kwa tamwa kupata uongozi wa kisheria...........................mimi niko kinyume na talaka lakini ningetamani kumfundisha huyu mwanaume kitu ili asirudie kitendo kama hiki tena. Naomba kuwasilisha.

Mapenzi ni kitu cha ajabu sana unaweza kumsaidia huyo mama kila kitu den siku ya kesi akakugeuka na kusema wewe ndo ulimshawishi kufanya hivyo ila bado mume wake anampenda sana utatatamani ardhi ipasuke uingie maana huyo baba kibano kitakugeukia. unaweza kumpa tu ushauri afanye mwenyewe au kumuonyesha njia nina mfano hai ndo maana nimesema hivyo.
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
Hicho kituo cha polisi kipo mbali kiasi gani na unapoishi? Manake hizi nyumba zetu za Uswazi bana.....mpaka polisi wafike...kwanza sijui watafikaje. Nyumba ina address?


Hahahahhahahahhahahaha......................hilo nalo tatizo lingine. Ukweli kituo cha polisi kiko mbali kidogo.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom