Habarini wanajanvi,
Moja kwa moja kwenye mada, Naomba mawazo yenu lakini yawe ya kujenga.
Mimi ni mfanyakazi wa kuajiliwa kwa miaka mingi na natarajia kustaafu Mwenyezi Mungu akipenda miaka 5 ijayo, nina mke na watoto sita kati yao wanne wamemaliza chuo kikuu,
Kwa miaka yote ya kufanya kazi mawazo yangu yote ni kwenda kumalizia maisha yangu kijijini na kufungua miradi yangu huko kutokana na fulsa ambazo nimeziona huko,
Kwa uzoefu wa jamaa zangu wengi ambao waliamua kutumia pesa zao za kustaafia kufungua biashara mjini, naweza kusema 95%walikwama na maisha yao yalikuwa ni kuombaomba,
Lakini asiliamia iliyobaki waliamua kwenda kijijini na kuwekeza wote maisha yao wanatafurahia,
Mke wangu kabila lake ni tofauti na mimi, lakini kila nikimshirisha kuhusu kwenda kijijini anakuwa kama hataki kusikia habari hiyo ni kuhamisha topic,
Lakini leo tulikuwa tunazungumzia habari ya vijana wa kijijini jinsi baadhi yao wanavyopiga maendeleo kwa kasi, na mimi kumtakia kuwa sasa na sisi tutengeneze maisha ya kijijini kuanzia sasa, aliishia kunikatisha tamaa kuwa maisha ya kijijini kwetu baadaye Yatakuwa mabaya sana .
Nilipomuuliza Mara mbili yatakuwa mabaya kivipi hakutaka kunijibu.
Nitaka niendelee kumuuliza yatakuwa mabaya kivipi baadaye, ndio nikaona umuhimu wa kuwashare na nyinyi hapa.
Kijijini tayari nina nyumba na nina mpango wa kuwa na nyumba nyingine ya kisssa zaidi ya kustaafia.
Kijijini chetu kuna umeme na maji na barabara nzuri ya rami inapita hapo karibu na kiwanja kingine changu.
Vijana wangu wawili wanafanya kazi wengine bado wanabangaiza.
Mjini nina nyumba mbili tayari., na nikiamua kuziuza leo sikosi 400m,
Mama tangu bado yupo na anaishi kijijini,
Namba mawazo yenu kuhusu nia ya huyu mke wangu,
Lakini mimi binafsi maisha ya mjini sina raha nayo kabisa,
Nimeishi huku mjini huu mwaka wa 37,
Naomba kuwasilisha
Moja kwa moja kwenye mada, Naomba mawazo yenu lakini yawe ya kujenga.
Mimi ni mfanyakazi wa kuajiliwa kwa miaka mingi na natarajia kustaafu Mwenyezi Mungu akipenda miaka 5 ijayo, nina mke na watoto sita kati yao wanne wamemaliza chuo kikuu,
Kwa miaka yote ya kufanya kazi mawazo yangu yote ni kwenda kumalizia maisha yangu kijijini na kufungua miradi yangu huko kutokana na fulsa ambazo nimeziona huko,
Kwa uzoefu wa jamaa zangu wengi ambao waliamua kutumia pesa zao za kustaafia kufungua biashara mjini, naweza kusema 95%walikwama na maisha yao yalikuwa ni kuombaomba,
Lakini asiliamia iliyobaki waliamua kwenda kijijini na kuwekeza wote maisha yao wanatafurahia,
Mke wangu kabila lake ni tofauti na mimi, lakini kila nikimshirisha kuhusu kwenda kijijini anakuwa kama hataki kusikia habari hiyo ni kuhamisha topic,
Lakini leo tulikuwa tunazungumzia habari ya vijana wa kijijini jinsi baadhi yao wanavyopiga maendeleo kwa kasi, na mimi kumtakia kuwa sasa na sisi tutengeneze maisha ya kijijini kuanzia sasa, aliishia kunikatisha tamaa kuwa maisha ya kijijini kwetu baadaye Yatakuwa mabaya sana .
Nilipomuuliza Mara mbili yatakuwa mabaya kivipi hakutaka kunijibu.
Nitaka niendelee kumuuliza yatakuwa mabaya kivipi baadaye, ndio nikaona umuhimu wa kuwashare na nyinyi hapa.
Kijijini tayari nina nyumba na nina mpango wa kuwa na nyumba nyingine ya kisssa zaidi ya kustaafia.
Kijijini chetu kuna umeme na maji na barabara nzuri ya rami inapita hapo karibu na kiwanja kingine changu.
Vijana wangu wawili wanafanya kazi wengine bado wanabangaiza.
Mjini nina nyumba mbili tayari., na nikiamua kuziuza leo sikosi 400m,
Mama tangu bado yupo na anaishi kijijini,
Namba mawazo yenu kuhusu nia ya huyu mke wangu,
Lakini mimi binafsi maisha ya mjini sina raha nayo kabisa,
Nimeishi huku mjini huu mwaka wa 37,
Naomba kuwasilisha
