mdida
JF-Expert Member
- Jul 14, 2011
- 1,607
- 772
Mimi ni mwanamke wa aged 30 nina watoto watatu ambao umri wao ni 10, 8 and 10.
Tatizo lililosababisha mpaka kuamua kuandika hili ni kwamba niko njia panda katika mahusiano yangu na mzazi mwenzangu. Huyu mwanaume amekuwa akiyapuuza majukumu yake ya msingi hasa ya kutunza familia, mwanzoni tulipoana alikuwa anatunza familia kwa muda miaka mitatu hivi alibadilika na kuanza kurudi saa sita usiku, siku nyingine anarudi saa kumi asubuhi akiwa amelewa sana, nikajitahidi sana kumwomba aache hiyo tabia lakini hakuacha. Kipato tulichokuwa nacho kikaishia kwenye pombe mie nikabaki ninahangaika na biashara ndogo ndogo ya kuuza karanga na ubuyu nilichokipata watoto tunakula wote, akawa hashikiki akirudi nyumbani anasearch ndani akikuta kamtaji kangu anaondoka nako atapombeka mpaka kesho yake. Basi nikawambia familia yangu kuhusu huu mwanendo lakini niliambiwa vumilia, baadae nilipata hela kidogo kutokana na biashara yangu nikajiendeleza kusoma computer sikumaliza program zote hela ikaisha, basi ilipofika mwaka 2008 nikapata kibarua kwenye Company furahi (Jina sitataja) nikaimarisha maisha yetu pale nyumbani. Tatizo linalonishangaza ni kwamba huyu mwanaume kila nikimpa mtaji afenye biashara anakula, nimeshampa kama mara tatu hivi, watoto nawahudumia mm , JE NIKIMWACHA NITAKUWA NIMEFANYA VIBAYA? Kwa sababu hata nikiongela juu ya maisha yetu anasema mm niamue nitakavyo , yaani uamuzi ni juu yangu kuachana au kuendelea kuishi.
Tatizo lililosababisha mpaka kuamua kuandika hili ni kwamba niko njia panda katika mahusiano yangu na mzazi mwenzangu. Huyu mwanaume amekuwa akiyapuuza majukumu yake ya msingi hasa ya kutunza familia, mwanzoni tulipoana alikuwa anatunza familia kwa muda miaka mitatu hivi alibadilika na kuanza kurudi saa sita usiku, siku nyingine anarudi saa kumi asubuhi akiwa amelewa sana, nikajitahidi sana kumwomba aache hiyo tabia lakini hakuacha. Kipato tulichokuwa nacho kikaishia kwenye pombe mie nikabaki ninahangaika na biashara ndogo ndogo ya kuuza karanga na ubuyu nilichokipata watoto tunakula wote, akawa hashikiki akirudi nyumbani anasearch ndani akikuta kamtaji kangu anaondoka nako atapombeka mpaka kesho yake. Basi nikawambia familia yangu kuhusu huu mwanendo lakini niliambiwa vumilia, baadae nilipata hela kidogo kutokana na biashara yangu nikajiendeleza kusoma computer sikumaliza program zote hela ikaisha, basi ilipofika mwaka 2008 nikapata kibarua kwenye Company furahi (Jina sitataja) nikaimarisha maisha yetu pale nyumbani. Tatizo linalonishangaza ni kwamba huyu mwanaume kila nikimpa mtaji afenye biashara anakula, nimeshampa kama mara tatu hivi, watoto nawahudumia mm , JE NIKIMWACHA NITAKUWA NIMEFANYA VIBAYA? Kwa sababu hata nikiongela juu ya maisha yetu anasema mm niamue nitakavyo , yaani uamuzi ni juu yangu kuachana au kuendelea kuishi.