Naomba ushauri baada ya matokeo ya mdogo wangu

Naomba ushauri baada ya matokeo ya mdogo wangu

asipoteze muda chuo kikuu hawezi pata hana D mbili katika tahasusi yake CBG nashauri kama form 4 ana D kwenye Fizikia Kemia na Biolojia aende kusoma Clinical Officer au Diploma ya Nursing ndiyo
fani zenye ajira na kujiajiri pia.
I also recommend this.
 
kaka hapo chuo kikuu apana aendi ana cutpoint ya 4 hapo kaka angalau angekua na D 2 ZA MASOMO YA COMBI YAKE ondoa hiyo ya gs ahiesabiki
Hivi siku hizi principal pass ni D eeh? Sisi enzi zetu (kuanzia miaka 10 iliyopita) ilikuwa E. Yaani ukiwa na E E E au E E S unaenda Chuo na wakuipata hiyo walikuwa wachache pia. Ila siku hizi naona kila familia watoto wao wamepata div one.
 
Ndugu samahani, najua mko bize na kutafuta mkate wa siku! Nilikua naomba ushauri wenu baada ya matokeo kutoka Mdogo wangu yeye amepata kama ifuatavyo katika tahasusi yake ya CBG.

GS.D .CHEM . E BIOS .E NA GEO. D BAM F.
DIVISON 3 YA 14.

Je, ningependa mnishauri akasomee kitu gani? Na je, anaweza kupata nafasi ya chuo kikuu kweli kwa hapa Tanzania private hasa hasa maana kwa ufaulu ninavouona sidhani kama kwa serikali anaweza kutoboa. Natanguliza shukurani.

NB: Vyuo gani anaweza kujaribu kuomba?
huyo diploma degee apati amekosa pricipal mbili
 
Chuo kikuu anaenda Ila awe tayar kusoma course yoyote ya ajabu ajabu
Sijui kama ilikua zamani ila kwakwel kwa Guidbook ya Mwaka jana na Mwaka huu bila D mbili husomi dgree hata ya Uhuni, Labda upigwe badae utumbuliwe na TCU
 
Sema ada zake huwa sio za kitoto aisee! hapo kumbuka anakua anajigharamia kila kitu na huyu mtoto wa kike mambo ya chuo unayajua aisee! ngoja kwanza tujipange hii pia ni aidea nzuri.

Sent from my TECNO BD4j using JamiiForums mobile app
Kumbe Manzi, mbona unataka kumtesa hivyo atafute Chuo tu under NACTE apige nursing basi hiyo Bachellor ataitafutaga Mwenyewe.
 
Nisikilize mimi achana na wote waliocomment mwanzo, akapige diploma ya macho (Optometry) ipo Mvumi Dodoma, au diploma ya Radiology. Usisahau kuja kunishukuru.
Ofcoz kama 3M+ kwa Mwaka zinapatikana aende mvumi
 
Huyu tangu mwanzo mlikosea kumpeleka A level ya science. Kwa matokeo haya alipaswa kusoma diploma baada ya form four, au kama ni A level angesoma arts. Option pekee iliyobaki ni kurudi kutafuta diploma kwa zile credentials zake za form four.
Yeah ulipofikia ni sahih lakini usimlaum kwan hakuamin kwamba hawez. Ni fighter singependeza kusoma arts kisa uoga. Bwana alitoa bwana Katwaa.
 
Back
Top Bottom